Posts

Showing posts from November, 2014

MABONDIA KUPAMBANA PWANI NOVEMBA 27 2014-VIDEO

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/26-11-2014 Kampuni ya GEORGE PROMOTION imeandaa Pambano la ngumi kukata na shoka kati ya Bondia anayechipukia katika mchezo huo mkoa wa Pwani, ZUMBA KUKWE na Bondia mkongwe nchini SWEET KALULU katika   pambano ambalo litafanyika kesho Novemba 27 kwenye ukumbi wa Kontena mjini Kibaha. Muandaaji wa mpambano huo, GEORGE NANGAI amesema kabla ya pambano hilo lisilo la ubingwa kutakuwepo na mapambano ya utangulizi ambapo KISOO SOLI atapambana na ISSA NAMPECHECHE, RAMA MAX atapambana na MUSTAPHA DOTTO. Bw. NANGAI amebainisha kuwa lengo la kuaanda mpambano huo ni kunyanyua mchezo wa ngumi katika Mkoa wa Pwani, kwa kutoa fursa kwa vijana kujiajiri katika mchezo huo. END.

BRITISH COUNCIL YASAIDIA VITABU SEKONDARI YA MWAMBISI-VIDEO

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/18-11-2014 Mkuu wa wilaya ya Kibaha BIBI. HALIMA KIHEMBA amepokea msaada wa vitabu vya kufundishia vya masomo ya Sayansi vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 6 kutoka shule ya LATYMER ya Nchini Uingereza kwa shule ya sekondari ya Kata ya Mwambisi katika suala zima la kukuza mshikamano kati ya shule hizo mbili. BIBI.KIHEMBA ameongeza kuwa msaada huo umekuja katika kipindi mwafaka wakati serikali ipo katika vuguvugu la ujenzi wa maabara katika kila shule ya sekondari nchini   kwa lengo la kuimarisha utoaji elimu katika masomo ya sayansi. Amesisitiza kuwa ni jambo la muhimu kuzingatia usalama wa vitu ambvyo vimetolewa ili viweze kuwasaidia na wengine ambao watabahatika kusoma shuleni hapo. Aidha Mkuu wa wilaya Kibaha BIBI.KIHEMBA ametoa ushauri kwa uongozi wa shule hiyo kuanzisha na maabara ya kompyuta ili kupanua wigo wa utoaji elimu shuleni hapo. Naye mwakilishi kutoka BRITISH COUNCIL, BI.LILIAN MSUYA akikabidhi vifaa hivyo amese

SHULE YAPATIWA VITABU VYA SAYANSI

Ben Komba/Pwani-Tanzania/18-11-2014 Mkuu wa wilaya ya Kibaha BIBI. HALIMA KIHEMBA amepokea msaada wa vitabu vya kufundishia vya masomo ya Sayansi vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 6 kutoka shule ya LATYMER ya Nchini Uingereza kwa shule ya sekondari ya Kata ya Mwambisi katika suala zima la kukuza mshikamano kati ya shule hizo mbili. BIBI.KIHEMBA ameongeza kuwa msaada huo umekuja katika kipindi mwafaka wakati serikali ipo katika vuguvugu la ujenzi wa maabara katika kila shule ya sekondari nchini   kwa lengo la kuimarisha utoaji elimu katika masomo ya sayansi. Amesisitiza kuwa ni jambo la muhimu kuzingatia usalama wa vitu ambvyo vimetolewa ili viweze kuwasaidia na wengine ambao watabahatika kusoma shuleni hapo. Aidha Mkuu wa wilaya Kibaha BIBI.KIHEMBA ametoa ushauri kwa uongozi wa shule hiyo kuanzisha na maabara ya kompyuta ili kupanua wigo wa utoaji elimu shuleni hapo. Naye mwakilishi kutoka BRITISH COUNCIL, BI.LILIAN MSUYA akikabidhi vifaa hivyo amese

WAFUGAJI WALALAMIKA KUVAMIWA MAENEO YAO

Ben Komba/Pwani-Tanzania/18-11-2014 Wananchi wa kijiji cha wafugaji cha Mindu Tulieni kilichopo wilaya ya Bagamoyo wameitaka serikali kuwasaidia katika suala zima la wakulima kuvamia maeneo yao ilihali wakijua kuwa eneo hilo kuptia mpango wa matumizi bora ya ardhi limetengwa kwa ajili ya jamii ya wafugaji. Mwandishi wa habari hizi akizungumza na MWmwenyekiti wa kijiji cha Mindu tulieni,BW. LETEMA SUNGUYA amebainisha kuwa imekuwa ni kawaida kwa wakazi kutoka maeneo ya Lugoba kuvamia maeneo tengefu ya wafugaji hali ambayo inasababisha uvunjifu wa amani hasa kipindi ambacho Ng”ombe kwa bahati mbaya akiiingia katika shamba la mkulima. BW.SUNGUYA ameongeza kuwa suala zima la serikali kuleta mpango wa matumizi bora ya ardhi umelenga katika kujaribu kuepusha migogoro iliyokuwa inajitokeza mara kwa mara kati ya wafugaji na wakulima ambapo mara nyingi imesababisha vifo ambavyo vingeweza kuzuilika. Naye Mwenyekiti wa kitongoji wa NADANYA,BW.ALOYCE PAUL ameelezea changamoto kubwa wanayokabiliana

UJENZI MAABARA WAPAMBA MOTO PWANI-VIDEO

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/12-11-2014 Katika utekelezaji wa agizo la Rais la ujenzi wa maabara kwa kila shule, Wananchi katika Kata ya Kongowe wamefanikiwa kupata vyumba vitatu vya maabar kupitia nguvu za wananchi na mchango kutoka mfuko wa Jimbo. Diwani wa Kata ya Kongowe,BW.SLOUM BAGMESH amesema wao kwa upande wamejipanga toka mapema katika kuhakikisha wanatekeleza agizo la Rais la kutaka kila shule ya sekondari kuwa na maabara tatu ifikapo Desemba mwaka huu. BW.BAGMESH ameongeza kuwa anamshukuru Mbunge wa Kibaha mjini, BW.SYLVESTRY KOKA kwa kuweza kutoa mabati 110 kwa ajili ya kuezekea shule ya Kata ya sekondari ya Mwambisi. Amewataka wananchi kujitokeza kuchangia katika utekelezaji wa agizo hilo kwani hapo baadaye ni Taifa na jamii ambazo zitafaidika na maabara zetu, kwani zitawezesha kupatikana kwa wataalamu katika masuala ya sayansi na teknolojia. Naye mkuu wa shule ya sekondari Mwambisi, BW.JOSEPH SIMBA ameelezea kutiwa moyo kwake na juhudi mbalimbali zina

SUPER STAR YAJIANDAA NA LIGI YA MKOA DARAJA LA TATU-VIDEO

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/12-11-2014 Timu ya soka ya SUPER STAR ya wilayani Bagamoyo inayojiandaa na ligi daraja la tatu ngazi ya Mkoa wa Pwani imeifunga Timu ya LUPUMOKO ya Kwamakocho kwa magoli 4-0 katika mchezo wa kirafiki uliofanyika katika uwanja wa Bongololo mjini Bagamoyo. Mkurugenzi wa Timu hiyo ABDUL SHARRIF amesema wameanza kuiandaa timu hiyo takriban mwezi sasa, na lengo kubwa ni kuhakikisha timu hiyo inapanda daraja na kuufanya mkoa wa Pwani hususan Bagamoyo inakuwa ina timu ambayo inacheza Ligi kuu na kwa sasa safari ndio imeshaanza. Sharrif amebainisha katika kujiweka sawa ndio wakaona vyema kucheza na timu mbalimbali katika hali ya kujiweka sawa kwa ajili ya Mchezo kati yake na Timu ya Kombaini ya walimu kutoka Mkuranga Hapo Tarehe 16 novemba. Naye kocha wa SUPER STAR, Mchezaji wa zamani wa timu ya Nyota Nyekundu na Simba katika nafasi ya golikipa, MTORO MAGOSO amesema timu yake imejiandaa vizuri na mechi inayoikabili ya ligi daraja la tatu ngazi ya M