Posts

Showing posts from October, 2012

MJI WA KIBAHA WAPANGA MIKAKATI

Ben Komba/Pwani-Tanzania/28-Oct-12/10:56:35 Halmashauri ya mji wa Kibaha katika robo ya kwanza ya Julai-Septemba inatarajia kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 4 milioni 230 laki mbili elfu 15 na 94, ikiwa ni makusanyo kutoka vyanzo vyake mbalimbali vya mapato ambayo ni asilimia 36 ya makisio ya mwaka 2012 mpaka 2013. Akisoma taarifa hiyo Makamumwenyekiti wa halmashauri hiyo BW. NANGULUKUTA SAID AHMAD amebainisha halmashauri katika robo ya kwanza ya Julai mpaka Septemba 2012 inatarajia kutumia shilingi milioni 323,967,413/= ambayo ni sawa na asilimia 16 ambayo ndiyo ya makisio ya mwaka wa fedha 2012/2013 ikiwa pamoja na salio anzia la Julai 01 2012. Na kati ya mambo ambayo yanatarajiwa kupewa kipaumbele ni pamoja na suala zima la utunzaji na usafi wa mazingira ya mji wa Kibaha kwa kuzindua gari la taka kwa ajili ya kukusanya taka kutoka maeneo mbali, kipaumbele kingine kitakuwa ni ununuzi wa gari la idara ya ardhi kupitia mapato ya ndani. Akizungumza katika kikao cha Baraz

VITA VYA KIDINI VYAPEWA NAFASI BAGAMOYO.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/28-Oct-12/09:35:52 Wanafunzi wakristo wa shule ya Sekondari Bagamoyo zamani maarufu kama MAGAMBANI wamefunga virago vyao na kuamua kurudi makwao kufuatia serikali kushindwa kusimamisha uasi unaofanywa na wanafunzi wa Kiislam wanaosoma katika shule hiyo ambao wamekuwa mstari wa mbele kuwakashifu wenzao wakristo na kuwatishia kuwauwa huku wakiangaliwa tu. Mmoja wa wanafunzi ambaye amerejea jana kutoka shule hiyo kutokana na hali kuzidi kuwa tete kutokana na kutochukuliwa hatua madhubuti ya kutatua mgogoro huo na serikali ya wilaya ya Bagamoyo inayoongozwa na BW. AHMED KIPOZI ambaye amewahi kuwa mwandishi wa habari na Mhadhiri katika Chuo cha Kiislam Morogoro kushindwa kutatua mgogoro huo ambao umeota mizizi wilayani hapo. Wanafunzi hao waliamua kuondoka kufuatia baadhi Waislamu wa nje kushupalia mgogoro huo na kuwatisha wanafunzi wakristo hao ambao wengi wao wakiwa ni wenye umri wa miaka 18 mpaka 25, ambapo nao wameazimia iwapo serikali itakubali ulalamis

KINAMAMA WAWEZESHWA NA INUKA.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/23-Oct-12/4:56:04 PM Wafanyakazi ambao wameajiriwa katika sekta mbalimbali za utumishi wa umma wametakiwa kujishughulisha na masuala ya ujasiria mali wanapotoka kuwajibika katika kazi zao walizoajiriwa nazo ili kuweza kukabiliana na changamoto za kiuchumi ambazo wanakumbana nazo kwa sasa na mara baada ya kustaafu. Mkurugenzi mtendaji wa kanda ya kaskazini, BW. DAVID MSUYA wa shirika hilo linaloitwa INUKA, linalowawezesha kina mama wajasiriamali bila kulazimika kuwa na amana kama ilivyo kwa taasisi nyingine za fedha, amesema katika kanda yake kuna vikundi takriban 24 na lengo kuu ni kuwajengea uwezo akinamama kuweza kutambua haki zao za msingi na kuwapatia mafunzo ya ujasiriamali ili kumfanya Mama nae awe chanzo cha mapato. BW. MSUYA amesema katika Mkoa wa Pwani wameanza kwa ktengeneza vikundi viwili ambavyo kimoja kipo katika Kata nya Magomeni mjini Bagamoyo na kingine kikiwa Ruvu darajani, amebainisha vikwazo kadhaa kujitokeza wakati wa utekelezaji wa zo

UDINI WAFUKUTA BAGAMOYO SEKONDARI.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/23-Oct-12/16:14:56 Hali ya sintofahamu imeyakumba mazingira ya Shule ya sekondari Bagamoyo kufuatia wanafunzi wa Kiislamu kutaka shule hiyo iendeshwe kwa misingi ya Kiislamu, na wakisusia taratibu za kawaida za shule kwa kisingizio cha kutekeleza nguzo za Kiislamu ya Uislam wao kwa kuamua kumlazimisha Mwalimu Mkuu aachie nafasi hiyo eti kuwa amekuwa akiwanyanyasa sana wao. Kutokana na hali hiyo wanafunzi wa Kikristo nao wakaamua kuvunja ukimya kwa kuamua kukabiliana na wanafunzi wenzao wa Kiislam ambao walikuwa wanataka kumshambulia Mwalimu Mkuu kwa kumsogelea na kumweka kati, na kuona hivyo wanafunzi wakristo nao wakasogelea eneo hilo wakiwa wamewazunguka Wanafunzi hao Waislamu wakiawaangalia kujua watamfanya nini Mwalimu Mkuum ili kujibu mapigo dhidi ya wenzao wa Kiislamu. Taarifa ya chanzo chetu ndani ya eneo la tukio kinasema hali hiyo imefuatiwa kwa kufanyika kwa uchaguzi wa viongozi wa wanafunzi kama ilivyo ada, na ndipo ilipobainika kuwa wenzao

VIJANA WAPATIWA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI KUPITIA ilo NA ypc

Ben Komba/Pwani-Tanzania/22-Oct-12/05:44:31 PM Mkuu wa wilaya Kibaha BIBI. HALIMA KIHEMBA amekemea tabia ya wanajamii kuwaita vijana kuwa ni bomu ambalo linasubiriwa kulipuka muda wowte bila kutafuta mbinu mwafaka za kuwaondoa katika ukosefu wa kazi kwa kuwapatia mafunzo na mtaji wa kuanzisha biashara na miradi ya kilimo na ufugaji. Mkuu huyo wa wilaya ya Kibaha, BIBI HALIMA KIHEMBA amesema juhudi ambazo zinaonyeshwa na mashirika yasiyo ya kiserikali kama ambavyo YOUTH PARTNERSHIP COUNTRYWIDE ambalo limewapatia vijana mafunzo kuhusiana masuala ya ujasiriamali ambapo kutasaidia kuwafanya vijana kubadilisha mtazamo kutoka kwa uliopo sasa wa kuwa vijana ni bomu linalongojea kulipuka mpaka kuwa wazalishaji wakuu ambao nguvu kazi yao itakuwa tegemeo kwa Taifa. Hayo ameyazungumza katika uzinduzi wa awamu ya pili ya mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana wa Kibaha ambvayo yanmefadhiliwa kwa asilimia kubwa na shirika la kazi ulimwenguni -ILO-, Na amekataa kukubaliana na dhana ya kuwa vijan

VIONGOZI WA DINI WAKUTANA NA JESHI LA POLISI.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/12/10/22/04:29:49 PM Jeshi la Polisi mkoa wa Pwani limeelezea kushangazwa kwake na hatua ya wahuni kuchoma makanisa na kuharibu mali za serikali kwa kisingizio cha muungano. Katika taarifa ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani kwa viongozi wa dini katika suala zima la kutambua mchango wao katika kuleta amani na utulivu katika jamii, Kaimu Kamanda wa mkoa wa Pwani, SALEH MBAGA amesema vitendo vinavyofanyika hivi sasa hapa nchini vinatia doa amani na usalama wa nchi yetu. BW. MBAGA amewashukuru viongozi wa dini hususan ya Kiislamu kwa kuweza kuwashika waumini wao wasifanye maandamano ya vurugu kama ilivyotokea Mkoa wa Dar es Saalam na Zanzibar, na kwa kutambua hilo Jeshi la Polisi liumeona vyema kukaa pamoja na viongozi wa dini ili kupata njia ya pamoja za amani ili kuendeleza ushirikiano wetu uliodumu kwa muda mrefu. Amebainisha kuwa Jeshi la Polisi kwa upande wake wanaamini kuwa kuna misingi ambayo ikifuatwa vyema italiweka Taifa pazuri, kwa kuifikia jamii

UNITED WITH ISRAEL.

Israel Alert Newsletter 26 Tishrei 5773 October 12, 2012 Israeli Vaccine to Stop Cancer from Returning to Patients (Nes Ziona, ISRAEL) An Israeli company is developing a new cancer drug which aims to stop cancer from coming back. Every year millions of people are diagnosed with cancer worldwide. Although modern medicine has made huge progress in treating this disease, what often happens is that the cancer is treated and the patient goes into remission or is even "cured" - but then it becomes a waiting game to see if the cancer comes back. Imagine if there was a new treatment option that would stop cancer from returning! An Israeli medical team is attempting to do just that, to offer a new treatment with the potential for long-term maintenance - to stop the cancer from coming back. Click here to read more>> Israel Nuclear Facility Receives 'Spiritual Protection' (Dimona, ISRAEL) The Israeli Dimona nuclear reactor facility now has an extra laye

BLESSED NATION RESPECT IT, and LEAVE BEHIND CAIN JELOUS AGAINST HIS BROTHER ABEL.

September 23, 2012 Israel Revolutionizes Liver Disease Treatment! Israeli scientists are developing a treatment for people suffering from liver disease. Nonalcoholic steatohepatitis (NASH) is a "silent" liver disease which affects two to five percent of Americans - approximately six to fifteen million people. Another ten to twenty percent of Americans, thirteen to twenty three million people, have fat in their livers but have not yet developed NASH. Tens of millions of people around the world also are at risk of suffering from NASH. Click here to read more>> Koch Urges Obama To Be Firm Over Israel Former New York City Mayor Ed Koch stood before over 1,000 people to deliver his annual Rosh Hashana sermon at the Park East Synagogue. Koch, who has talked openly about his close ties to President Obama, lambasted the president and current US policy towards Israel: "I'm distressed. President Obama is refusing to publicly make clear to Iran that 'I

FIRE SOCIAL CLUB YAPATA VIONGOZI.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/10/07/2012/16:32:18 FIRE SOCIAL CLUB ya mijini Kibaha imefanya kikao chake cha uchaguzi mkuu na kufanikiwa kupata viongozi watakaoiongoza kwa kipindi cha miaka mitatu, ambapo uongozi huo umenuia kufanya mambo mabalimbali katika kuhakikisha michezo inakuwa ajira ya kutegemewa na vijana. Katika uchaguzi huo Mwenyekiti amechagulia kuwa JUMA MBWANA, na nafasi ya Katibu ikichukuliwa na RICH KIBAJA, Mweka hazina akiwa KESSY PONSI na mtunza vifaa akichaguliwa kuwa ni MESHAKI KAIRA. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Katibu wa FIRE SOCIAL CLUB, RICH KIBAJA amebainisha kuwa lengo ni kukuza michezo hususan timu ya soka ambayo tayari ipo, kwa kuibua vipaji vya vijana ambao wanahitaji usaidizi mdogo ili waweze kusonga mbele katika medani ya michezo. KIBAJA ameongeza kuwa michezo ina umuhimu mkubwa kwa binadamu toka michezo ni starehe, afya na burudani. END

KIBAHA INDEPENDENT SCHOOL.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/12/10/07/12:04:46 PM Shule ya msingi ya Kibaha independent iliyopo mjini Kibaha imeazimia kuwaandaa wanafunzi kuishi kulingana na maendeleo na mabadiliko ya sayansi ya teknolojia ya utandawazi ili kuweza kukua kitaaluma, kiakili, kijinsia na kimaono. Ameyazungumza hayo Mkuu wa shule ya Kibaha Independent, BW. HEZRON MUSALALE wakati akimkaribisha mgeni rasmi katika mahafali ya darasa la saba, Lengo kuu la shule yao ni kuhakikisha vijana wanaopita hapo wanakuwa matunda ambayo yatachangia kwa njia moja au nyingine maendeleo ya Taifa. BW. MUSALALE amebainisha makakati wa shule kuvipa nuru ya kielimu vizazi vingi kwa kuvipatia elimu ya hali ya juu, na hasa shule ikiwa ina malengo mahsusi ya kuhakikisha wanafunzi wanaweza kusoma na kuandika kwa kutumia lugha mbalimbali hususan Kiswahili na Kiingereza, kuhakikisha wanafunzi wanajenga uwezo wa hali ya juu ya mahesabu na pamoja na kuwajenga wanafunzi katika kujiamini na kuwa na mawazo yakinifu. Akizungumza

WAJASIRIAMALI VIJANA WAONYESHA BIDHAA KIBAHA.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/12/10/07/11:05:32 Waziri wa utamaduni, habari, vijana na michezo BIBI. FENELA MKANGARA amewahimiza vijana kujikusanya katika vikundi kwa lengo la kujiendeleza katika kazi za kijasiriamali kwa kuwawezesha kuaminika katika umoja wao na kuweza kukopesheka kwa kudhaminiana wenyewe kwa wenyewe. BIBI. MKANGARA amesema vijana kwa kujikusanya katika vikundi na kuanzisha miradi ya uzalishaji mali kutasaidia kwa kiasi kikubwa vijana wanaoamka na kukaa vijiweni bila kujishughulisha na kazi yoyote ya uzalishaji mali, na kuwataka vijana kutumia kilimo kwanza kujiajiri binafsi na hasa kutokana na maisha ya sasa kuhitaji vijana kuwa wabunifu ili waweze kujiepusha na umaskini. BIBI. MKANGARA amewahimiza kila kijana wa Kitanzania kuanzia miaka 18 aweze kuchangia chakula mezani kwao kwa kuwajibika kikamilifu katika shughuli za kijasiriamali ambazo zitawaingizia tija, na Wizara ya utamaduni, habari, vijana na michezo itajitahidi kwa hali na mali kutafuita masoko kwa ajili