Posts

Showing posts from September, 2013

MAENDELEO YAHIMIZWA PWANI.

MAENDELEO YAHIMIZWA PWANI. Ben Komba/Pwani-Tanzania/17-09-2013/10:58 Mkuu wa Mkoa wa Pwani,BIBI.MWANTUMU MAHIZA amekemea tabia ya watendaji kusababisha migogoro ya ardhi katika jamii kutokana na utendaji wao kuongozwa na maslahi binafsi hali ambayo inatishia hali ya ulinzi na usalama nchini.  BIBI.MAHIZA amewaambia watendaji katika kikao cha kuhimiza maendeleo ya Mkoa wa Pwani kilichofanyika mjini Kibaha kuwa wanachoponzwa nacho ni tamaa ya vifedha vidogo vidogo wanavyopokea ndio kichocheo cha uvinjifu wa amani katika wilaya, Kata na Mitaa/vijiji.  BIBI.MAHIZA ameonya kuwa iwapo atabaini viongozi ndio wanahusika katika kuchonganisha raia, basi atahakikisha mhusika anachukuliwa hatua za kisheria bila kujali yeye ni chama gani au ni nani ili kuendeleza utamaduni wa kutii sheria bila shuruti.  Amewachukulia watu wanaowachonganisha wananchi katika masuala ni wabaya ambao wanasababisha uvinjifu wa amani.  Akiongea katika kikao hicho Mwenyekiti wa serikali Mkoani  A, BW.TITUS SA

WAZAZI WATAKIWA KUSAIDIANA WALIMU

Ben Komba/Pwani-Tanzania/17-09-2013/10:22 Wazazi nchini wametakiwa kusaidiana na Walimu katika kuhakikisha wanafunzi wanapata mafanikio ya kielimu na kijamii ili kuweza kujenga jamii yenye maarifa na nidhamu ambayo itawasaidia katika maisha yao ya baadaye. Akizungumza katika mahafali ya kumaliza elimu ya msingi Katika shule ya KIBAHA INDEPENDENT mjini Kibaha, Mke wa Mbunge wa Jimbo la uchaguzi Kibaha mjini, BIbi.SELINA KOKA amewaasa wazazi kutowaachia Walimu pekee jukumu la kuwalea watoto kielimu. BIBI.KOKA amefafanua kutokana na wakati mwingi wanafunzi kuwa Walimu katika suala zima la kupatiwa elimu na ulezi wanapokuwa shuleni, na wazazi nao hawana budi kuwajibika katika kuhakikisha mara mwanafunzi anaporudi kutoka shule wanangalia maendeleo yao katika kuhakikisha malengo ya kuwapatia wanafunzi elimu bora yanafikiwa. Aidha BIBI.KOKA ameutaka uongozi wa shule hiyo kuingiza masomo ya upishi na kudarizi katika silabasi yao katika kuhakikisha wanapanua wigo wa utoaj

ULINZI SHIRIKISHI JAMII.

ULINZI SHIRIKISHI JAMII. Ben Komba/14-09-2013/12:11 Katika hali inayoonyesha wananchi wameanza kupata mwamko kuhusiana na suala zima la ulinzi shirikishi, vijana waendesha bodaboda mjini Kibaha wakitumia mbinu za Polisi jamii wamefanikiwa kumkamata kijana anayetuhumiwa kujihusisha na vitendo vya kiuhalifu dhidi ya madereva wenzake na abiria. Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi ya waendesha Bodaboda mjini hapa BW.JOHN JOSHUA, Amesema kutokana na kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa wateja na madereva wenzie kuhusiana na Kijana aliyekamatwa BW.SIFAEL BOLEGOLE  aka MWIBA ambaye ana makazi katika maeneo ya Kibaha-Nyumbu na Kimara. BW.JOSHUA amebainisha kuwa siku moja BW.SIFAEL BOLEGOLE aliufikia uongozi na kuwataarifu kuwa kuna mtu amemwendea na kumpa mpango wa wizi wa pikipiki, kitu ambacho binafsi alikuwa hajafurahishwa nacho, na ndipo wakamwelekeza mtuhumiwa kwenda kwa Aliyempa mpango huo ambaye ni BW.SEIF na kujifanya kukubaliana naye. Mwenyekiti huyo wa Kamati ya ulinzi ya waendesha bodaboda

CHADEMA WAZINDUA OPERESHENI ZINDUKA KIBAHA

CHADEMA KUZINDUA OPERESHENI ZINDUKA KIBAHA. Ben Komba/Pwani-Tanzania/13-09-2013/03:39 Chama cha Demokrasia na maendeleo mjini Kibaha mkoa wa Pwani wameanzisha mpango mkakati maalum wa kutembelea mitaa, katika operesheni itayokwenda na jina la ZINDUKA. Mwenyekiti wa Chama hicho wilayani Kibaha, BW.BUMIJA SENKONDO amesema msukumo wameupata kutokana na kushuhudia ushirikishwaji mdogo wa wananchi katika maamuzi muhimu yanayowahusu na hivyo watatumia opersheni hiyo kuwazindua wananchi juu ya mambo yanayofanywa na chama tawala. BW.BUMIJA amebainisha kuwa katika Bajeti ya halmashauri ya mji wa Kibaha asilimia 90 ya  miradi iliyotekelezwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2013/2014 haikuwahusisha wananchi katika uibuaji wa miradi kulingana na mahitaji yao kama inavyoelekezwa na sheria za serikali za mitaa. Mwenyekiti huyo wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, BW.BUMIJA SENKONDO amefafanua kuwa operesheni hiyo itaenda sambamba na kupokea wanachama wapya na kujenga uhai wa Chama. Aidha ameongeza

VIKWAZO VYAMKWAMISHA MWEKEZAJI SEKTA YA SUKARI

ECOENERGY YAOMBA KUONDOLEWA VIKWAZO. Ben Komba/Pwani-Tanzania/13-09-2013/09:50 Waziri wa nchi ofisi ya Waziri mkuu uwekezaji na uwezeshaji, BIBI.MARY NAGU amesema serikali itahakikisha inaondoa vikwazo vinavyokabili wawekezaji katika sekta ya sukari ili waweze kupata tija wao na ustawi wa uchumi. Ameyasema hayo kufuatia ziara ambayo ameifanya kutembelea mradi wa shamba la mwekezaji ECOENERGY katika eneo la Gama wilayani Bagamoyo, ambapo Waziri NAGU amesema vikwazo vya upatikanaji wa vibali vya umiliki wa ardhi vinaondolewa. Waziri NAGU amesema lengo la kwenda kuzuru eneo hilo ni kutaka kuhakikisha ECOENERGY wamefikia wapi ili waweze kuogeza kasi ya ukamilishaji wa mradi huo na ikizingatiwa Tanzania ina upungufu mkubwa wa sukari na hivyo kwa kutumia wawekezaji tatizo hilo linaweza kukabiliwa. Mwenyekiti mtendaji wa ECOENERGY, BW.PER CUSTERED amemueleza Waziri NAGU kuhusu changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo toka wameanza mradi huo ambao ulianza rasmi mwaka 2006, lakini mpaka leo wa

TEMBEA KWA AJILI YA TEMBO

TEMBEA KWA AJILI YA TEMBO. Ben Komba/Pwani-Tanzania/12-09-2013/02:12 Wanaharakati wa kupinga ujangili kutoka Arusha ambao  umeshika kasi nchini wamefanya matembezi kuiamsha jamii kuamka kifikra kwa kujua jukumu la kulinda maliasili zetu ni jukumu la kila mtu. Kiongozi wa wanaharakati hao BW.MKAZENI MKAZENI amesama wao wanafanyakazi na AFRICAN WILDLIFE TRUST yenye maskani yake Arusha ambayo moja ya malengo yake makuu na kupambana na wawindaji haramu. BW.MKAZENI amesema safari yao wameianza tarehe 24 Agosti na kupewa Baraka zote na Mkuu wa Arusha, BW.MAGESA MULONGO na kupata ushirikiano mkubwa kutoka kwa watu mbalimbali walipokuwa katika matembezi hayo, na amesisistiza hawana itakadi za chama chochote cha siasa. Naye mmoja wa washiriki wa matembezi hayo bibi.REHEMA MSUYA amesema kwa upande wake yeye amepata msukumo kutokana na harakati za uwindaji haramu ambao siku hadi siku umekuwa ukishika kasi. BIBI.REHEMA amebainisha kuwa kinachomstua zaidi ni kuona kuwa kizazi kijacho kinahatari ya

USHIRIKA WAHUJUMIWA

USHIRKA WAHUJUMIWA Ben Komba/Pwani-Tanzania/Thursday, September 12, 2013 Wanachama wa chama cha ushirika cha wakulima wa umwagiliaji mpunga Bonde la Mto Ruvu juu CHAURU wilayani Bagamoyo,wameulalamikia uongozi wa ushirika huo kwa kufanya mambo kinyume na taratibu za ushirika. Akiongea na mmoja wa wanachama wa siku nyingi wa Ushirika huo, BW.SADALLAH CHACHA mwanacham namba,1.12.2 amebainisha  kuwepo ubadhirifu wa mali za ushirika kwa manufaa binafsi. BW.CHACHA  amesema anashudia kuona ushirika ukiendeshwa bila kufuata kanuni na taratibu zilizowekwa kupitia katiba ya ushirika huo, amebainisha katika mambo ambayo wanachama hawakubaliani nayo ni pamoja na uwepo wa Wachina bila kushirikisha wanachama. Ametoa mfano wa ghala lililokuwa linatumika kuhifadhi mazao ya wanachama wa ushirika huo ambalo Mwenyekiti wa ushirika huo, BW.ZAHOR SENG’ENGE amewakabidhi wachina ambao wamejenga uzio ili kuwanyima fursa wanachama wa ushirika kutumia. Bw.CHACHA amefafanua na mara zote wakitaka kujua kuhusian

MAMLAKA YA HALI YA HEWA WAKUTANA NA WAHARIRI

Ben Komba/Pwani-Tanzania/04-09-2013/16:26 Mkuu wa mkoa wa Pwani BIBI. MWANTUMU MAHIZA ameitaka mamlaka ya hali ya hewa nchini kuvitumia vyombo vya habari kwa makini ili viweze kusaidia wananchi kuelewa umuhimu wa mamlaka hiyo katika utekelezaji wao wa majukumu ya kila siku. Akiongea katika semina ambayo imewahusu wahariri wa vyombo vya habari nchini iliyoandaliwa na mamlaka ya hali ya hewa, BIBI. MAHIZA amesema baadhi ya wananchi wengi wananchi wengi wa nchi yetu wanajifanya hamnazo kwa kupuuza taarifa inayotolewa na mamlaka ya hali ya hewa. Ameishauri mamlaka ya hali ya hewa kuweka sheria zitakazowabana wananchi ambao watapuuza maelekezo yanayotolewa na mamlaka ya hali ya hewa, kama mamlaka inatangaza bahari imechafuka lakini kuna baadhi yao wanaingiza vyombo baharini na matokeo ya karibuni yalisababisha vifo vya watu 18. BIBI. MAHIZA amesema kutokana na upuuzi hali imekuwa mbaya zaidi na wakati mwingine kusababisha majanga, ameishauri mamlaka hiyokupeleka muswada

WAKULIMA WA MBOGA WAPATIWA PAMPU

Ben Komba/Pwani-Tanzania/04-09-2013/11:09 Mbunge wa Jimbo la uchaguzi Kibaha mjini MH. SYLVESTER KOKA akatika mfululizo wake wa kutekeleza ahadi mbalimbali alizozitoa wakati wa kampeni ya ya uchaguzi mkuu uliopita kwa kutoa pampu kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji katika mtaa wa Mbwawa halmashauri ya mji wa Kibaha. Kabla ya kukabidhi pampu hizo kwa wananchi wa Mbwawa na Miswe MH. KOKA alitoa fursa kwa mtendaji wa Kata ya Mbwawa, BW.TIZESA FARIS NTIRUGEREGWA ambaye amesema tatizo kubwa linalowakabili ni maji. BW.NTIRUGEREGWA amefafanua kuwa wamekuwa wakikabiliwa na ukosefu mkubwa wa maji kwa takriban miezi miwili sasa na kutokana na changamoto hiyo na nyingine kama ukosefu wa zahanati. MH.KOKA amebainisha kuwa kwa upande wa kero ya maji suala hilo linashughulikiwa ambapo kwa sasa serikali imeanzisha mradi maalum wa kuhakikisha kunapatikana maji ya kutosha kwa wananchi wanaoishi kati ya Ruvu na Kimara. Amefafanua kuwa ujenzi huo wa bomba kubwa la maji lenye kipenyo

KATIBU UWT ASAIDIA WAJASIRIAMALI.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/01-09-2013/10:59 Katibu wa Jumuiya wa wanawake wa chama cha mapinduzi Taifa BI.AMINA MAKILAGI amekipatia kikundi cha kinamama wajasiriamali cha WANAWAKE KWANZA, kilichopo mtaa wa Maili Moja ka tika halmashauri ya mji wa Kibaha shilingi laki tano kwa ajili ya kuwasaidia katika uboreshaji wa kazi zao.   Akikitembelea kiwanda kidogo cha kusindika chakula na vinywaji baridi kinachomilikiwa na kinamama wajasiriamali wa kikundi cha MWANAMKE KWANZA, Katibu huyo wa UWT Taifa BI.MAKILAGI amesema wanachokifanya ni kutekeleza katiba ya jumuiya hiyo. Na anaamini kwa kufanya hivyo kinamama wanaweza kujikomboa kwenye matatizo ya kisiasa,kijamii na kiuchumi kama inavyoelekeza ilani ya uchaguzi ya chama hicho. Naye mmoja wa wanakikundi Mama wa Shamba wajasiriamali akisoma taarifa kwa mgeni rasmi amesema kikundi chao cha STK MAMA KWANZA   ni kikundi cha wanawake wajasiriamali kinachoshughulika na na usindikaji wa vyakula mbalimbali ikiwemo juice za matunda,li