Posts

Showing posts from September, 2014

WANAKIJIJI WAANDAMANA BAGAMOYO

Ben Komba/Pwani-Tanzania Wananchi wa Kijiji cha Kinzagu kata ya Lugoba Tarafa ya Msoga wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwania wameandamana kudai utekelezaji wa makubaliano kati ya kijiji na mwekezaji. Wananchi hao waliokuwa wakiimba nyimbo za kudai haki zao kufuatia kuchoshwa na ahadi ya mwekezaji katika madini ya kokoto kijijini hapo kutototekeleza ahadi walizokubaliana wakati walipofika kuomb ardhi kwa ajili ya uchimbaji wa madini ya kokoto kwa matumizi ya ujenzi wa mabasi yaendayo kasi jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa kiji hicho BW. WILLIAM MAKUMU akizungumza kwa niaba ya wakazi amesema kuwa wanaungana na wanakijiji hao kutokana na Kampuni STRABAG kuchukua ardhi kwa makubaliano wa ujenzi wa zahanati lakini baada ya kuchelewa kufanya hivyo moja ya makampuni yanayoenbdesha shughuli za uchimbaji ikajenga hivyo wakaingia makubaliano mengine ya kuwapatia umeme na kununua trekta. MAKUMU amebainisha kuwa Mkandarasi huyo kampuni ya STRABAG imekuwa ikizunguka katika utekelez

WAKULIMA WALALAMIKIA HATUA YA MKUU WA MKOA

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/25/09/2014 12:09:59 Mgogoro wa ardhi uliokuwa unafukuta kwa kipindi kirefu kati yaUshirika wa kilimo cha umwagiliaji Kitomondo na uongozi wa kijiji hicho umeazimia kuitisha kikao cha wananchama wote kujua hatma ya shamba hilo. Akizungumza na waandishi wa habari Mwenyekiti wa wakulima hao,BW.EDWIN MUTAYOBA amesema wao walifika   k atika Bonde hilo ikiwa ni sehemu ya mkakati kuendesha ukulima wa kisasa. BW.MUTAYOBA amedai lakini muda mfupi baada ya wakulima hao kuanza kuliweka shamba hilo katika mpangilio kwa kuingiza greda katika kuhakikisha mashamba yote yanakuwa na miundombinu ya barabara likufanya usafirishaji wa mazao kuwa rahisi. BW.MUTAYOBA anabainisha baada ya Mkuu wa Mkoa aliyeondolewa BI.AMINA MRISHO ndio alipoamuru uendelezaji wa shamba hilo ukome na kupelekwa kwa shauri mahakamani kwa madai ya shamba kutolewa kwa kinyume cha taratibu. Hata hivyo baada ya kesi hiyo kufika mahakamani, wakulima wa ushirika huo takriban 600 walifani

NAFASI ZA POLISI KWA WALIOMALIZA 2014

KUITWA KWENYE USAILI. JESHI LA POLISI MKOA WA PWANI LINAPENDA KUWAKUMBUSHA WAHITIMU WOTE WA KIDATO CHA NNE KWA MWAKA 2013 NA WALE WA KIDATO CHA SITA KWA MWAKA 2014 KTK SHULE ZA SEKONDARI ZILIZOPO MKOA WA PWANI AMBAO WAMEITWA KWENYE USAILI NA MAJINA YAO YAPO KWENYE TOVUTI YA POLISI www.policeforce.go.tz na ile ya TAMISEMI www.pmorlag.go.tz KUFIKA KTK OFISI YA KAMANDA WA POLISI MKOA WA PWANI KUANZIA 23/09/2014 HADI 26/09/2014 MUDA WA SAA 2.00 ASUBUHI HADI SAA 10.00 ALASIRI BILA YA KUKOSA WAKIWA NA VYETI VYAO HALISI. KWA WALE WALIOMBALI WANAWEZA KUFIKA KWENYE USAILI HUO KWENYE MIKOA MINGINE KWA MUJIBU WA SIKU ZILIZOANISHWA KWENYE MIKOA HIYO KUPITA TOVUTI YA POLISI AU YA TAMISEMI. TAARIFA HII IMETOLEWA NA KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA PWANI SSP ATHUMANI MWAMBALASWA u

WAHIMZWA KUCHANGAMKIA UJASIRIAMALI.

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/11:19 Wakulima na wafugaji nchini wametakiwa kuzingatia kutumia mbinu mpya za kufanya shughuli zao ili kuwezesha kwa wakati huohuo kutunza mazingira na utunzaji wa uoto wa asili. Mwakilishi wa mkuu wa wilaya ya Kibaha, Afisa Tarafa wa Kibaha, BW.ANATOLY MHANGO amesema kuwa wafugaji wamekuwa wakikata majani mengi kwa ajili ya kulishia mifugo yao na kutumia kiasi kidogo cha majani kama asilimia 20 na asilimia 80 iliyobaki yanatupwa. Bw. MHANGO ameshauri wafugaji kukata majani ya kulishia mifugo kwa kadri ya mahitaji na kuyakata kata katika vipande vidogovidogo na kuyatia chumvi, kwa kufanya hivyo mifugo watakula malisho yao bila kusaza na huku majani mengine yakiwa kama akiba. Amewaasa wazee kujiunga na mafunzo ya mifugo na kilimo ili waweze kutumia muda wao kwa manufaa, badala ya kukalia kucheza bao na kurandaranda mitaani bila madhumuni yaliyo bayana. Naye mkufunzi wa mafunzo ya ufugaji na kilimo, BW.MHEGELELE MDUDA amesema Chuo chao ki

CHADEMA WAUNGURUMA VIGWAZA

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania Chama cha demokrasia na maendeleo kimewataka wananchi katika Mkoa wa Pwani kubadilika na kuchagua upinzani katika chaguzi zijazo ili kuharakisha maendeleo yao ya kiuchumi, kijamii na kitamaduni. Akizungumza katika ziara yake aliyofanya katika Jimbo la uchaguzi Chalinze, Mbunge wa Iringa mjini, MCHUNGAJI. PETER MSIGWA amesema tatizo la watu wa Pwani kila siku kazi yao ni kuchagua watu walewale na hivyo kuwaona wao kama wateja wao. Na kuwataka wananchi katika uchaguzi wa serikali ya mitaa kutofanya makosa kuwachagua watu walewale kwani ni watu ambao hawana uchungu na wananchi wan nchi hii. Mchungaji.MSIGWA amesema kuwa kinachoendelea sasa kwa viongozi wa Chama Tawala kuwabeba watoto wao na kuwapachika nyadhifa mbalimbali na hivyo Chama hicho kukosa sifa ya kuwaongoza kwa misingi ya haki na usawa na kuamua kuweka mbele maslahi binafsi badala ya wananchi. Naye mmoja wa Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Pwani,BW.MBENNA MAKALA amewataka wakazi wa R

MWEKEZAJI APIGWA STOP RUVU DARAJANI

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania Wakazi wa Ruvu Darajani wilayani Bagamoyo kwa kauli moja wameamua kumsimamisha mwekezaji kuendeleza eneo ambalo inadaiwa amelipata kinyume cha taratibu. Uamuzi huo umefikia baada ya kufanyika mkutano wa kijiji kujadili ugawaji holela wa ardhi na kusimamiwa na mtendaji wa Kata ya Vigwaza BW.MASKUZI MASKUZI ambaye kwa upande alikiri kuwa makosa yamefanyika katika utoaji wa ardhi katika eneo hilo ambalo wananchi wanalalamikia. BW.MASKUZI alitoa fursa kwa wananchi kutoa maoni yao kuhusu hatua gani zichukuliwe katika kuhakikisha suala hilo linatatuliwa kwa haraka bila kuleta uvunjifu wa amani katika kijiji cha Ruvu Darajani kama hali inavyojionyesha kwa sasa. Wananchi wakichangia kuhusu suala hilo, BW.ATHUMAN MKALI alikumbushia ujio wa Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, BW.AHMED KIPOZI wakati wa mkutano wa kuondoa uongozi uliopita kutokana matatizo ya ardhi ambapo alionya uongozi wa mpito usiguse kabisa masuala ya ardhi mpaka hapo utakapopatikana u