Posts

Showing posts from May, 2013

MGOGORO STENDI

Ben Komba/Pwani-Tanzania/27-May-13/19:42:08 Sakata kubwa limeibuka kufuatia amri ya kuwataka wafanyabiashara wanaotoa huduma ya kutoa na kupokea fedha kwa njia ya simu za mkononi sawa na wauza vocha na wafanyabiashara wengine kuondoa vibanda vyao vya biashara katika eneo hilo. Kamera ya SIBUKA TV imeshuhudia wafanyabiashara hao wakimsongasonga mmoja wa wanamgambo wa halmashauri ya mji kwa kiklichodaiwa kupita na kuandika vibanda vyao kutumia rangi ya mafuta ya kupuliza neno ondoka hali iliyozua ghadhabu kiasi cha kukaribia kumuadhibu mgambo huyo. Mazingira ya watu wanaofanya shughuli zao kutokubaliana hatua ya Mgambo hao kupita wakiandika kila kitu kilicho mbele yao, ONDOA hali iliyozua taharuki miongoni mwa wafanyabiashara hao ambao wanadai wanafuata taratibu zote za kisheria kuwepo katika eneo hilo. Akiongea kuhusu tujkio hilo la mgambo wa halmashauri kupita kuandika katika maeneo mbalimbali ya vibandavya stendi, Bwana afya wa Kata ya Mailimoja, BW. ABUBAKAR SHAH amesema

KANISA LAWASAIDIA WALEMAVU.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/26-May-13/9:55:05 Makanisa nchini yametakiwa kuwajenga waumini wao kwa misingi ya kuheshimu haki na amani ili kuweza kutoa fursa kwa waumini kuabudu wanachoamini kutokana na hali utulivu iliyopo kutokana na misingi imara iliyoachwa na viongozi wa mwanzo. Akizungumza katika harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kununua kiwanja cha kanisa hilo la PENTECOSTAL MISSIONARY CHURCH kutokana na kwa sasa kuwa katika eneo la hifadhi ya barabara ya kuu ya Morogoro, Mjumbe wa halmashauri kuu ya Taifa ya CCM mkoa wa Pwani BW. RUGEMALIRA RUTATINA amesema kanisa linawajibu wa kukemea na kutoa maelekezo kwa serikali kuhusiana na suala zima la kutunza amani iliyopo. BW. RUTATINA amesema Taasisi za dini zimekuwa zinaisaidia serikali katika kuhakikisha amani iliyopo inadumu bila kuvurugwa, na serikali katika hilo imekuwa ikiunga mkono juhudi hizo zinazoonyeshwa na kanisa katika kuhakikisha nchi inakuwa na ustawi. Mchungaji GERVAS MASANJA amesema Kanisa lao katika k

AKAMATWA AKIWANGA.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/26-May-13/19:36:49 Kijana mmoja anayejulikana kwa jina moja tu la UBAYA amenusurika kuuwawa kufuatia kukutwa ndani ya chumba ambacho kilikuwa kimefungwa milango na madirisha kwa umakini mkubwa bila mafanikio. Akielezea mkasa huo Mama ISMAIL ambaye mtoto wake ISMAIL mwenye umri wa miaka mitatu alikuwa ndio lengo la mtu huyo anayesadikiwa kuwa ni mshirikina kutokana na maelezo ambayo aliyatoa mara baada ya kumwagiwa maji ya baraka. Katika kumdadisi MAMA ISMAIL anadai kuwa kijana huyo siomgeni katika macho yake na alikuwa wameishi pamoja kule Mwanza katika Kota za Polisi ambapo wazazi wao walikuwa watumishi wa serikali takribani miaka 10 iliyopita. MAMA ISMAIL amebainisha siku ya tukio walistukia kijana huyo amelala Barazani akionekana amechoka na mchafu kutokana na kuona hilo wakaamua kumuwekea mlinzi maalum wakazi wote wa eneo hilo na kuamua kulala nae nje lakini hata hivyo walinzi hao walizidiwa na kujikuta wamepitiwa na usingizi. Na ndipo mara MAMA

WITO KWA VIONGOZI WA UMMA.

Taarifa hii iliyotolewa kwa hisani ya Jeshi la Polisi mkoa wa Pwani kupitia msemaji wake HASSAN JUMA imebainisha kuwa Viongozi wa Serikali za Mitaa wameaswa kufanya kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu iliyopo kwa watumishi wa umma wakati wa kutekeleza wajibu wao kwa wananchi. hayo yamesemwa na Bw. Daniel Machunda kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Pwani katika Warsha ya siku moja iliyohusisha makundi mbalimbali ya kijamii kwa lengo la kukuza uelewa wa wananchi kuhusu rushwa na kuhimiza uwajibikaji kwa maendeleo ya nchi. Bw. Machunda ameeleza kuwa suala la uwajibikaji kwa viongozi wa Serikali za mitaa ni jambo la wajibu na wanapaswa kuhakikisha wanatenda haki katika maeneo wanayoyasimamia pamoja na kuhakikisha rushwa haina nafasi kwenye maeneo yao wakati wa kutoa huduma kwa wananchi. Ameongeza kuwa watumishi wa umma wanatakiwa kuelewa kuwa kwa sasa wananchi wana uelewa mkubwa na wanajua haki zao, hivyo wanapaswa kutimiza wajibu wao kwa mujibu wa sheria ili kuepush

CCM WATISHA MJINI KIBAHA MWISHONI MWA WIKI.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/12-May-13/9:49 PM Vijana wa chama cha mapinduzi mkoa wa Pwani wametakiwa kuwa kitu kimoja katika kuhakikisha wanaimarisha umoja na mshikamano katika Chama chao na kuepuka mifarakano isiyo ya lazima. Akiongea katika ziara yake kuzungukia Kata 11 zilizopo mjini Kibaha Mwenyekiti wa CCM, BW. IDD KANYALU kwa lengo la kutoa shukrani kwa wanachama wa chama hicho ambao walimpigia kura wakati wa uchaguzi wa ndani wa chama hicho. BW. KANYALU amesema akiwa kata ya Mailimoja katika kipindi cha uchaguzi kulikuwa kuna changamoto mbalimbali ambazo zimejitokeza kiasi cha kuzua makundi ambayo hayawezi kukisaidia chama kwa namna yoyote ile. BW. KANYALU amebainisha kuwa kwa sasa ni vyema kwa vijana kusahau tofauti zao za kipindi cha uchaguzi ili kuweza kutekeleza majukumu yao kwa umakini wa hali ya juu na kukipatia chama mafanikio. Akiongea katika mkutano huo katika kata ya Mailimoja, Mwenyekiti wa chipukizi Kata ya Mailimoja, Binti mdogo IMRAN MOHAMED amesema kwa upande wa

SOMALIA SITUATION LIKE.

AM IIN SOMALIA OR?

Arusha Yetu: WALIOFARIKI KWENYE TUKIO LA MLIPUKO WA BOMU KANISA...

<a href="http://arusha-yetu.blogspot.com/2013/05/waliofariki-kwenye-tukio-la-mlipuko-wa.html?spref=bl">Arusha Yetu: WALIOFARIKI KWENYE TUKIO LA MLIPUKO WA BOMU KANISA...</a>: Mapadri wa kanisa katoliki wakiwa wamebeba jeneza lenyenye mwili wa mmoja wa waliokufa katika tukio la kutupwa kwa bomu la mkonok...

KINAMAMA WAPATIWA MSAADA WA PAMPU

Ben Komba/Pwani-Tanzania/10-May-13/19:33:06 Mlezi wa Jumuiya ya kinamama wa CCM mjini Kibaha ametoa msaada wa pampu ya kumwagilia maji kwa akinamama kutoka katika Kata ya Tumbi yenye thamani ya shilingi laki tano na kumi elfu kwa ajili yakuwasaidia katika shughuli zao za kilimo na kujipatia kipato. Akikabidhi pampu hiyo kwa akinamama hao, Mlezi wa UWT BIBI.SELINA KOKA ambaye pia ni Mke wa mbunge wa Kibaha mjini, BW. SYLVESTER KOKA amesema kuwa hatua hiyo kuwasaidia kinamama hao kitendea kazi hicho kufuatia ahadi aliyowapa kinamama hao siku ya maadhimisho ya siku ya wanawake ulimwenguni. BIBI.KOKA amebainisha kwamba anaamini kwa kuwasidia kinamama hao kutawawezesha kupunguza umaskini kwa njia moja au nyingine toka kikundi chao kinafanya shughuli za ukulima wa mboga mboga, na kwa kuwapatia kifaa hicho uzalishaji wa mboga utaboreka na kuwa rahisi kutokana na kupata nyenzo hiyo. Akizungumzia kuhusiana na soko la mbogamboga ambazo kikundi hicho cha kinamama kata ya Tumbi kitazalish

UKUAJI WA KASI WA UDINI IKIWA IMEBAKI 3ERS TO LEFT.

MAMBO YA MABOMU MAMBO YA KUANDALIWA HAYO, HAYA KAENI MKAO WA KUFA TENA WAHALIFU WAKUBWA WANAFUNGWA KIFUNGO CHA NJE.

MAMLAK YA MJI MDOGO MLANDIZI HOI.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/ Wananchi katika mamlaka ya mji mdogo wa Mlandizi wamelalamika hatua ya uanzishaji wa mji huo na kuutelekeza bila kuiwezesha kifedha hali inayoathiri utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya kila siku. Nikiongea na mmoja wa wajumbe wa baraza la mamlaka ya mji mdogo wa Mlandizi ambaye alikataa jina lake kutajwa , amebaiinisha kuwa kumekuwepo na changamoto mbalimbali zinazoikabili mamlaka ya mji mdogo wa Mlandizi. Mjumbe huyo amesema kutokana na kukosekana kwa fedha kutoka halmashauri kunakosabishwa na baadhi ya watendaji ya halmashauri kuchelea wao kupunguza fedha za uendeshaji wa halmashauri kutokana na kutojiamini. Mjube huyo amebainisha kutokuwepo kwa vikao vya kisheria vya kila mwaka vinavyofanywa na baraza la mamlaka ya mji mdogo wa Mlandizi kwa madai ya kukosekana kwa fedha na kuhoji serikali inawezaje kupanga mipango ambayo haiwezi kuitekeleza. Naye Mwenyekiti wa mamalaka ya mji mdogo wa Mlandizi, BW. ABDALLAH KIDO amesema ni

UONGOZI WA ZIMAMOTO WAKABIDHIWA ZAWADI.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/Monday, 06 May, 2013/06:58:25 PM Uongozi wa Kikosi cha uokoaji na zimamoto katika Mkoa wa Pwani umekabidhiwa rasmi zawadi ya mshindi tatu ya Kombe la SUPER CUP michuano yake iliyomalizika hivi karibuni,   Akikabidhi zawadi hiyo kwa Kaimu Kamanda wa Kikosi cha uokoaji nazimamot Pwani, Kamishna msaidizi JUMA ATHUMAN YANGE, Mwenyekiti wa timuya FIRE FC, BW. RICH KIBAJA amebainisha kuwa wamefanya hivyo kutpokana na mchango mkubwa unaotolewa na Kikosi cha zimamoto na uokoaji kwa timu hiyo.   Aidha Kibaja amekiomba kikosi hicho kukipanua kiwanja chao cha mazoezi ili kutoa fursa ya kuwepo angalau kiwanja kimoja chenye vipimo stahili kwa ajili ya kutumika kwa michezo mbalimbali tofauti na ilivyo hivi sasa ambapo hakuna kiwanja chamichezochenye sifa mjini Kibaha.   Akipokea zawadi hiyo ya jezi seti moja waliyopata timu hiyo ya FIRE FC, Kaimu Kamanda wa Kikosi cha uokoaji na zimamoto Kamishna msaidizi JUMA ATHUMAN YANGE amewapongeza wachezaji kwa jitihada walizoon