Posts

Showing posts from 2013

AJALI MWISHONI MWA MWAKA.

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/12/31/2013 10:39:12 AM Pamoja na jitihada mbalimbal;I zinazofanywa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani kupunguza ajali zisizo na lazima, baadhi ya madereva wameonyesha kupuuza kwa tahadhari hizo na kusababisha ajali ambazo zinawasababishia vifo au ulemavu. Mwandishi wa habari hizi ameshuhudia ajali iliyosababishwa na mwendo wa kasi baada ya gari ndogo aina ya TOYOTA iliyokuwa inasafiri kati ya Bagamoyo na Mlandizi kuacha njia na kuvamia vibanda vya wafanyabiashara. Mwenyekiti wa serikali ya mtaa Mbwawa, BW.RAMADHAN KONDO amebainisha kuwa gari hiyo iliacha njia na kugonga vibanda vya wafanyabiashara, na aliyejeruhiwa ni mtu mmoja, BW.JAFFAR YOHANA ambaye alikimbizwa kituo cha afya Mlandizi. BW.KONDO amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo. END.

TAARIFA YA UTEKELEZAJI JESHI LA POLISI PWANI

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/12/26/2013 9:41:12 AM Takwimu za Jeshi la Polisi mkoa wa Pwani zimebainisha kuwa katika kipindi cha mwaka 2013, jumla ya matukio 3705 yameripotiwa katika vituo mbalimbali vya Polisi, kati ya makosa hayo ni Mauaji, Kubaka, Kulawiti, Wizi wa watoto na utupaji wa watoto. Akisoma taarifa ya utekelezaji ya Jeshi hilo katika mkoa wa Pwani, Kamishna msaidizi mwandamizi, URLICH MATEI amebainisha kuwa makosa hayo yamegawiwa katika makundi manne, makosa dhidi ya ubinadamu, makosa dhidi ya kuwania mali, Makosa dhidi ya maadili ya jamii na makosa ya usalama barabarani. Kamanda MATEI   amezungumzia upande wa makosa ya kuwania mali ambayo yametokea katika kipindi cha mwaka 2013 ni pamoja na kukamatwa kwa noti bandia zenye thamani ya milioni 3,040,000/= huko Chalinze katika wilaya ya Bagamoyo ambazo zilikuwa zimehifadhiwa ndani ya bahasha. Kwa upande wa uhalifu dhidi ya maadili ya jamii, Kamanda MATEI ameongeza kuiwa Jeshi la Polisi limeweza kudhibiti mae

SOGA WAJIPANGA VYEMA KULINDA MISITU.

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/12/23/2013 10:53:31 AM Wananchi katika Kata ya Soga wilayani Kibaha wametakiwa kusaidiana na wakala wa serikali wa misitu- TFS- kwa kuziunga mkono kamati za maliasili wakati wa utekelezaji majukumu yao badala ya kuwa kikwazo. Mtendaji wa Kata ya Soga, BW. BERT MFALAMAGOHA amesema kamati za maliasili za vijiji zimekuwa zinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa na wananchi kuanza kuwanyooshea vidole wanapotekeleza wajibu wao. BW.MFALAMAGOHA amepongeza hatua ya wakala misitu Tanzania kwa kutoa elimu kwa jamii inayozungukwa na msitu wa Ruvu kusini, ili waweze kuitunza na kuilinda misitu kwa faida ya maeneo husika. Amefafanua kuwa kumekuwepo na mafanikio makubwa toka kuanzishwa kwa mradi wa mama misitu katika ukanda huo wa Ruvu   Kusini ambapo sasa wananchi wametambua wajibu wao katika kulinda na kutunza misitu ya maeneo yanayowazunguka. Mratibu wa Mama misitu Ruvu Kusini, BW.YAHYA MTONDA   amesema kuwa anaamini wananchi wa Soga wana n

AKADEMI YA SOKA YA AMAZON MKURANGA

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/10-12-2013/11:20 Akademi ya mchezo ya mchezo wa   soka ya AMAZON iliyopo katika halmashauri ya wilaya ya Mkuranga imeanzisha mashindano maalum ya umri wa miaka 17 na 14 kwa lengo ya kuvitambua viapaji vinagli vichanga. Mkurugenzi wa akademi ya soka ya AMAZON, SHUKURU NGWESHANI amesema mashindano hayo yatatumika kutambua na kukuza vipaji vya vijana ambao watakaoonyesha uwezo wa kusakata kabumbu kwa kiwango kinachostahili. NGWESHANI amesema mashindano hayo yatashirikisha timu nane, ambapo timu nane kati ya hizo nne zitakuwa za vijana chini ya miaka 14 na nne nyingine chini ya miaka 17. Aidha NGWESHANI amewaomba wadau wa mchezo wa soka wilayani Mkuranga na Mkoa wa Pwani kuunga mkono hatua ambazo ameaanza kuchukua kupitia akademi ya AMAZON katika suala zima la kuibua vipaji. END.

MAMA MISITU YAWAPATIA ELIMU WANANCHI JUU YA UVUNAJI AMAZAO YA MISITU.

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/10-12-2013 Wananchi wa kijiji Chakenge wamepatiwa elimu maalum kuhusiana na utaratibu mzima unaohusiana na mazao ya misitu kuepusha ukataji holela misitu na  kupunguza malalamiuko kutoka kwa wananchi wa maeneo ya uvunaji. Akiongea na wanakijiji wa Chakenge, Mratibu wa mradi wa mama misitu msitu wa Ruvu kusini, BW.YAHYA MTONDA amesema kuwa utaratibu wa uvunaji wa mazao ya misitu unaambatana na mambo makuu manne. BW. MTONDA amefafanua kuwa mambo hayo ni kukata leseni ambayo inatolewa bure, kibali cha halmashauri ambacho kitategemea ujazo wa mazao ya misitu itakayovunwa, kibali cha kusafirisha mazao ya misitu na kibali cha ushuru cha serikali kuu na kibali cha mwenyekiti wa serikali ya mtaa/kijiji. BW.MTONDA amebainisha kuwa utoaji elimu huo una lengo kuleta mageuzi chanya  katika suala uwajibikaji wa jamii ili kuwajenga katika kutambua umuhimu wa utunzaji misitu na kufahamu taratibu  zinazohusiana na utunzaji wa misitu. Aidha amewataka viongozi wa vijiji na ka

MGOGORO USHIRIKA WA CHAURU.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/12/3/2013 11:52:32 AM Wanaushirika wa shamba la umwagiliaji CHAURU Ruvu wilaya ya Bagamoyo katika mkoa wa Pwani, wameendelea kuwalalamikia maofisa wanaohusika na masuala ya ushirika kutoka hatua stahili panapotokea migogoro katika ushirika. Hivi karibuni mwandishi wa habari hizi amebahatika kuzuru katika ushirika wa umwagiliaji CHAURU na kukutana na baadhi ya wanachama wa ushirika huo na kubahatika kuongea na Mkulimwa mwasisi wa ushirika huo, BW.DAUD KINDAMBA ambaye amesema mambo yanayoendelea katika ushirika huo hayastahili kufumbiwa macho na maofisa ushirika. BW.KINDAMBA amesema yeye shamba lake lipo mfereji namba nne, toka kufika kwa katika eneo hilo shamba hilo ambalo mwanzo lilikuwa chini ya Wachina na baadaye kukabidhiwa kwa wazawa baada ya Wachina kuondoka na kukabidhiwa kila kitu kilichokuwepo eneo hilo. Ameshauri mamlaka ya ushirika kuwasaidia wanachama wa ushirika huo kwa vitendo vinavyofanywa na mtu mmoja na huku wanachama wakien