Posts

Showing posts from January, 2014

KWAYA YA MTAKATIFU DON BOSCHO YAFANYA HARAMBEE.

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/29-01-2014/12:28 Jumla ya shilingi Milioni tatu zimepatikana katika harambee ya kuiwezesha kwaya ya MTAKATIFU.DON BOSCHO ya mjini Kibaha katika Mkoa wa Pwani kuweza kufanya ziara yake katika mji wa Namugongo nchini Uganda kwa ajili ya ziara ya Kitume. Akizungumza wakati wa harambee iliyofanyika katika ukumbi wa TRIPPLE J, Katibu wa kwaya MTAKATIFU DON BOSCHO, BI.PHILOMENA SHIJA amesema lengo la kuaandaa harambee hiyo ni kutafuta shilingi milioni 25 kwa ajili ya safari ya Namugongo, Uganda. BI.SHIJA ameongeza kuwa mbali ya kutafuta nauli ya kwenda Uganda, harambee hiyo pia ilikuwa na jukumu la kuchangisha fedha kwa ajili ya ununuzi wa basi ambalo litawawezesha kusafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine lenye thamani ya shilingi milioni 70. Katibu huyo wa Kwaya ya MTAKATIFU DON BOSCHO,. Bi.PHILOMENA SHIJA amebainisha kwa hiyo ambayo ina miaka 30 kutoka kuanzishwa kwake, mpaka sasa imetoa albamu sita. Naye Mgeni Rasmi   katika hafla hiyo B

MWEKEZAJI ALALAMIKIWA

MWEKEZAJI AHARIBU MIUNDOMBINU YA UMWAGILIAJI. Ben Komba/Pwani-Tanzania/24-01-2014/10:15 Wakulima wa ushirika wa umwagiliaji Ruvu CHAURU wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani,wamelalamikia hatua ya mwekezaji wa Kichina katika shamba hilo kuvunja tuta linalozuia maji kufurika maeneo ya makazi wakati Mto Msua unapojaa. Mmoja wa wakulima ambaye nimeongea naye,BW.SADALAH CHACHA amesema hatua ya kupasua ukingo wa kuzuia maji yasisambae maeneo ya makazi na kilimo inatishia usalama wa wakulima na mali zao kutokana tabia ya Mto Msua kufurika kipindi cha mvua za msimu na kuwa hatari kwa mustakabili wa shamba hilo. BW. SADALAH amemwonyesha mwandishi wa habari hizi eneo maji yanaofikia wakati wa mafuriko ambapo yanajaa hadi kufiki futi 16 kutoka mkondo halisi wa maji na hivyo kuwepo na hatari ya kutokea mafuriko wakati wowote kutoka sasa. Naye mkulima mwingine amebainisha kuwa tatizo la shamba hilo la ushirika ni kuendeshwa kibabe bila kushirikisha wananchi na hayo ndiyo matokeo yake, toka wa

BAJETI 2014/2015 WILAYA YA KIBAHA

Ben Komba/Pwani-Tanzania/22-01-15/12:08 Halmashauri ya wilaya wilaya Kibaha katika mwaka wa fedha 2014 mpaka 2015 inatarajia kutumia shilingi 18,045,984,815/=   bila kuhusisha michango ya wananchi. Hayo yamebainishwa na Ofisa mipango wilaya ya Kibaha, BW.ENOCK KIVELEGE wakati akiwasilisha makisio ya bajeti ya halmashauri ya wilaya ya Kibaha katika kikao cha Baraza la wafanyakazi wa halmashauri, BW.KIVELEGE amesema kati ya fedha hizo shilingi 15,713,153,623/= ni mchango toka serikali kuu. BW.KIVELEGE ameongeza na fedha nyingine shilingi 2,332,831,192/= ikiwa ni mapato ya ndani ya halmashauri,na katika mwaka 2014 mpaka 2015 halmashauri ya wilaya ya Kibaha imekadiria kukusanya kiwango hico kikiwa ni mapato ya ndani. BW. KIVELEGE ameongeza kuwa halmashauri imekuwa ikikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni uhaba wa fedha wa kutekeleza shughuli zilizopangwa kufanyika, ufinyu wa mapato ya ndani na mchango wa wananchi kuwa mdogo kulinganisha na mahitaji ya halashauri.

MRAJIS ATANZUA MGOGORO

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/1/9/2014 11:05:07 PM Bodi ya wajumbe wa Chama cha ushirika wa umwagiliaji-CHAURU- uliopo Bagamoyo mkoa wa Pwani wamekosa sifa ya kuendelea kushikilia nafasi zao kutokana na kushindwa kuwasilisha ukaguzi wa mahesabu kwa wakaguzi wa vyama vya ushirika nchini kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo. Akizungumza katika Mkutano mkuu maalum wa ushirika huo, Mrajis msaidizi wa vyama vya ushirika Mkoa wa Pwani, BIBI.HADIJA MANG’ELA amesema taratibu za vyama vya ushirika zipo wazi, iwapo hesabu hazijakaguliwa na mkaguzi wa nje kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo bodi itapoteza uhalali. BIBI.MANG’ELA ameongeza kuwa mbali ya kupoteza hadhi ya kuwa wajumbe wa bodi, pia watasimamishwa kugombea uongozi kwa kipindi cha miaka sita kama adhabu yao ya kushindwa kutimiza majukumu yao basi sheria namba 48 kifungu kidogo cha 7 ya sheria ya vyama vya ushirika itabidi kutumika. Akijitetea mbele ya mkutano huo maalum, Mwenyekiti wa Ushirika wa umwagiliaji CHAURU

MFUKO WA RAIS WA KUJITEGEMEA UMEBAKI JINA TU.

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/1/5/2014 10:32:56 AM Wanachama wa mfuko Rais mjini Kibaha wamelalamikia hatua ya kusumbuliwa na watendaji wa mfuko huo kutokana nakutopewa miko[po wanayohitaji pamoja na kulipa fedha za akiba walizotakiwa kutoa kabla ya kupatiwa mkopo huo. Mwandishi wa habari hizi akiongea na mmoja wa mmoja wa wanakikundi wa kikundi cha Kiluvya B, Mama EUNICE MACHA ambaye amebainisha kuwa kwa sasa ana takriban miaka isiyopungua sita toka ametoa fedha za akiba kwa ajili ya kupatiwa mkopo huo, lakini imekuwa wakizungushwa mpaka sasa. Mama.MACHA amebainisha kutokana na hali hiyo biashara zake zimekuwa zikiyumba na kumsababishia maisha magumu na yasiyo na uhakika na akiwa hajui kama fedha zake zikirudishwa zitakuwa na riba au la. Mama.MACHA ameongeza kuwa amekuwa mteja wa mfuko huo wa Rais kwa kipindi cha miaka 5, na wameanza kudai amana zao toka mwaka 2008, lakini hakuna kilichofanyika kuhusiana na malipo ya akiba za wanachama baada ya mfuko huo wa Rais kush

MFUKO WA RAIS HOI

MFUKO WA RAIS WA KUJITEGEMEA UMEBAKI JINA TU. Ben Komba/Pwani-Tanzania/1/5/2014 10:32:56 AM Wanachama wa mfuko Rais mjini Kibaha wamelalamikia hatua ya kusumbuliwa na watendaji wa mfuko huo kutokana nakutopewa miko[po wanayohitaji pamoja na kulipa fedha za akiba walizotakiwa kutoa kabla ya kupatiwa mkopo huo. Mwandishi wa habari hizi akiongea na mmoja wa mmoja wa wanakikundi wa kikundi cha Kiluvya B, Mama EUNICE MACHA ambaye amebainisha kuwa kwa sasa ana takriban miaka isiyopungua sita toka ametoa fedha za akiba kwa ajili ya kupatiwa mkopo huo, lakini imekuwa wakizungushwa mpaka sasa. Mama.MACHA amebainisha kutokana na hali hiyo biashara zake zimekuwa zikiyumba na kumsababishia maisha magumu na yasiyo na uhakika na akiwa hajui kama fedha zake zikirudishwa zitakuwa na riba au la. Mama.MACHA ameongeza kuwa amekuwa mteja wa mfuko huo wa Rais kwa kipindi cha miaka 5, na wameanza kudai amana zao toka mwaka 2008, lakini hakuna kilichofanyika kuhusiana na malipo ya akiba za wanachama baada y

MCHELE BEI CHINI.

Image
Ben Komba/PWANI-TANZANIA/1/2/2014 10:47:38 AM Serikali nchini imetakiwa kujenga mazingira mazuri kwa wajasiriamali wazawa ili waweze kupambana na changamoto mbalimbali zinazosababishwa na sheria ambazo hazizingatii mazingira ya halisi ya kiuchumi. Mjasiriamali BW.OTTO KINYONYI mkazi wa Mlandizi wilayani Kibaha ambaye anamiliki kampuni ya KINYONYI INVESTMENT ambayo inashughulikia mazao ya nafaka katika soko la Mchele Mlandizi amesema sheria nyingi zinazotumgwa na serikali zimekuwa zinambana mjasiriamali. BW.KINYONYI ametoa mfano wa mrundikano wa kodi mbalimbali ambazo mfanyabiashara anapaswa kulipa ambazo zinaambatana na makadirio batili, ongezeko la bei ya umeme ambayo itasababisha mlipuko wa bei ambao hivi karibuni   ulipoa, kutokana na gharama za uzalishaji kupanda. Pamoja na changamoto hiyo BW. KINYONYI ameongeza pia kuna nyingine ikiwa pamoja na kukosekana kwa mvua za kutosha ambapo wakati mwingine inawabidi kuagiza mpunga kutoka Morogoro hasa inapotokea ku