Posts

Showing posts from October, 2013

TFF WAPYA WAPONGEZWA

Thursday, October 31, 2013/Ben Komba/Pwani-Tanzania/17:28:06 Mdau wa soka mkoa wa Pwani ambaye pia ni kiongozi wa vilabu amewapongeza wajumbe wa kamati ya utendaji na Rais wapya   waliochaguliwa katika uchaguzi mkuu wa shirikisho la soka Tanzania uliofanyika hivi karibuni. Akiongea na mwandishi wa habari hizi mdau mkubwa wa soka katika Mkoa wa Pwani, BW. MRISHO SWAGALA amewapongeza viongozi wapya waliobahatika kuchaguliwa katika kinyang’anyiro hicho. BW.SWAGALA amefafanua kuwa wanachotakiwa kufanya uongozi mpya ni kutumia fursa hiyo adimu kunyanyua kiwango cha mchezo wa soka nchini ambao umekuwa ukilegalega siku hadi siku kwa sababu ya kukosekana viongozi makini. Aidha ameelezea Jinsi anavyomjua Rais wa sasa wa TFF, JAMAL MALINZI kama ni mchapakazi wa ukweli na amemshuhudia mara kadhaa akitumia uwezo wake wa hali na mali kusaidia mchezo huo hususan katika Mkoa wa Pwani. END.

SUMATRA YAOMBA USHIRIKIANO.

Image

HALMASHAURI YA MJI KIBAHA YAENDELEA KULALAMIKIWA

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/29/10/2013-09:41 Halmashauri ya mji wa Kibaha imeshauriwa kuangalia njia njia mbadala ya kuhakikisha kuwa pikipiki na wenye magari wanakuwa na maeneo maalum ya kuegesha magari yao. Hayo yamezungumzwa na diwani Kata ya Maili moja, BW.ANDREW LUGANO kufuatia malalamiko ya madereva wa vyombo hivyo kufuatia halmashauri kubandika mabango kuzuia uegeshaji wa magari maeneo mbayo yamezoeleka kwa shughuli hiyo. BW.LUGANO ameongeza kuwa yeye kama diwani wa Kata ya Mailimoja hakubaliani kabisa na hatua aliyochukua Mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Kibaha, BI.JENIFA OMOLO wa kutoa tangazo hilo. Bw.LUGANO amemtaka Mkurugenzi kabla ya kuanza kubandika matangazo ya makatazo ya uegeshaji wa magari na pikipiki maeneo ambayo yamezoeleka, angefanya utaratibu wa kutengeneza miundombinu ambayo itasaidia kupunguza tatizo hilo yaani maegesho. Naye dereva wa bodaboda BW. RAMADHAN SAID wa mjini Kibaha ameeleza kusikitishwa kwake na halmashauri kutunga sheria

SUMATRA NA WANANCHI.

Image
Ben Komba/29-Oct-13/10:36:08 AM Mamlaka way a usafiri wan chi kavu na baharini SUMATRA wamewasisitizia wananchi kuto ushirikiano kwao katika kuhakikisha mazingira ya usafirishaji wa abiria na mali zao unakuwa salama na uhakika. Afisa mwandamizi wa SUMATRA mkoa wa Pwani, BW.NASHON IROGA ameyasema alipokutana na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha ambapo amesema wamekuwa wanakutana na changamoto mbalimbali wakati wa utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku. BW.IROGA amesema mara nyingi wamekuwa wakikutana na abiria ambao hawaelewi umuhimu wa magari yao kukaguliwa, kitu ambacho ni jukumu kubwa la SUMATRA katika kuhakikisha vyombo hivyo vya usafiri   vinakuwa katika viwango vinavyostahili kusafirsha abiria na mali zao. Ameongeza kuwa abiria wengi ulalamika kwamba wanacheleweshwa safari zao ambapo wakati mwingine mabasi hayo yakionekana dhahiri ni mabovu, na hivyo kuwataka abiria kuelewa dhana nzima ya SUMATRA ya kukagua magari hayo na kuhakikisha hayakatis
Image

WAZAZI WASAIDIANE NA WALIMU

Image

BIG RESULTS NOW

Image

MTOTO WA UMRI WA MIAKA 3 AUWAWA KATIKA MAZINGIRA TATA

Image

MAREFA WAASWA KUTIMIZA MAJUKUMU YAO KWA UAMINIFU.

Image

MGOGORO WA ARDHI SOFU.

Image

MGOMO WA MAGARI MADOGO YA MIZIGO

Image
Image

AJITOKEZA KUGOMBEA UJUMBE KAMATI UTENDAJI TFF

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/24-10-13/10:52 Mgombea wa nafasi ya ujumbe wa kamati ya utendaji ya shirikisho la soka nchini kutoka Kanda namba 11 ya Pwani na Morogoro, anayetoka mkoa wa Pwani RIZIKI MAJALA ameelezea nia yake ya kufufua soka la Tanzania mara atakapochaguliwa nafasi hiyo. RIZIKI MAJALA ambaye hapo awali alienguliwa katika kinyang,anyiro hicho na hatimaye jina lake kurudishwa baadaye kama mmoja wa wagombeaji, amebainisha kuanzisha program maalum ya soka itakayohusisha vijana katika suala zima la kuinua kiwango cha soka. MAJALA kwa sasa ni Katibu wa COREFA ambaye mwenye elimu ya chuo kikuu kwenye ualimu, ameawahi kushika nyadhifa mbalimbali katika vyama vya waamuzi, makocha na soka. Amejitosa kugombea ikiwa ni wajibu kwa mikoa ya Pwani na Morogoro kutoa mwakilishi na amewaomba wajumbe wa mikoa ya Pwani na Morogoro na Kanda nyingine kumpa kura za ndiyo ili akichaguliwa aungane na wenzie katika kuongoza shirikisho hilo la soka nchini. END.

MJUMBE AOMBA KURA TFF

Ben Komba/Pwani-Tanzania/24-10-13/10:52 Mgombea wa nafasi ya ujumbe wa kamati ya utendaji ya shirikisho la soka nchini kutoka Kanda namba 11 ya Pwani na Morogoro, anayetoka mkoa wa Pwani RIZIKI MAJALA ameelezea nia yake ya kufufua soka la Tanzania mara atakapochaguliwa nafasi hiyo. RIZIKI MAJALA ambaye hapo awali alienguliwa katika kinyang,anyiro hicho na hatimaye jina lake kurudishwa baadaye kama mmoja wa wagombeaji, amebainisha kuanzisha program maalum ya soka itakayohusisha vijana katika suala zima la kuinua kiwango cha soka. MAJALA kwa sasa ni Katibu wa COREFA ambaye mwenye elimu ya chuo kikuu kwenye ualimu, ameawahi kushika nyadhifa mbalimbali katika vyama vya waamuzi, makocha na soka. Amejitosa kugombea ikiwa ni wajibu kwa mikoa ya Pwani na Morogoro kutoa mwakilishi na amewaomba wajumbe wa mikoa ya Pwani na Morogoro kumpa kura za ndiyo ili akichaguliwa aungane na wenzie katika kuongoza shirikisho hilo la soka nchini. END.

MGOMO WA VYOMBO VYA MOTO VYA MIZIGO

Ben Komba/Pwani-Tanzania/21-10-2013/13;30 Madereva wa Magari madogo ya mizigo,na Pikipiki aina ya Toyo na Bajaj wamefanya maandamano ya amani kuelekea ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Kibaha kushinikiza kuwekewa kwa miundombinu katika eneo ambalo wanafanya shughuli zao. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi akizungumza na mmoja wa Viongozi wao, BW.ABDALLAH ZANDA amesema kitu kikubwa kilichowafanya wachukue hatua ya kuandamana ni Polisi kuwakamata wakiwa wanatekeleza majukumu yao ya kila siku. BW.ZANDA amebainisha kwa kipindi kirefu halmashauri walitoa agizo la magari na pikipiki za kubeba mizigo kuhama eneo hilo, jambo ambalo wao kwa upande wao hawana kipingamizi nalo, lakini tatizo ni kukosekana kwa miundo mbinu ya uhakika katika eneo hilo. Amefafanua baadhi ya vitu muhimu ambavyo vinakosekana ni pamoja na huduma ya choo katika sehemu ambayo inakaa karibu watu 100, mabanda ya mamalishe, kukosekana kwa mabanda ya kupumzikia madereva na wateja na hivyo

UBADHIRIFU IDARA YA ARDHI.

WANANCHI WADHULUMIWA FIDIA MRADI WA VIWANJA 500 SOFU. Ben Komba/Pwani-Tanzania/14:10:2013/11:31 Katika hali inayoonyesha udhaifu mkubwa kwa katika Idara ya ardhi halmashauri ya mji wa Kibaha, mamia ya wananchi walio katika mradi wa viwanja 500 ambao uligharimu fedha za mkopo kutoka wizara ya ardhi wa shilingi milioni 470. Mmoja wa walalamikaji BW.JUMA MUYOMBE amekana kulipwa fidia yoyote na halmashauri ya mji kuhusiana na ardhi, wakati kwenye kumbukumbu za malipo zinaonyesha kuwa wameshalipwa na hivyo kutumia ujanja kupora maeneo ya wananchi kwa manufaa yao  binafsi. BW.MUYOMBE  amesema hatua ya Afisa ardhi halmashauri ya mji wa Kibaha, BW.EDWARD MBALA kudai wananchi wote waliohusika katika mradi wa viwanja 500 vya SOFU kulipwa fidia ni ujanja unaofanywa na baadhi ya viongozi wa halmashauri ili waweze kutumia fedha hizo kwa manufaa yao. Naye BIBI.ASHA JUMA NDWELA ameshangazwa na hatua ya halmashauri ya miji wa Kibaha, kuonyesha watu mbali eneo lake analomiliki toka mwaka 1977, alipofi

AUWA MTOTO WA MIAKA 3, AJARIBU KUTOROKA LAKINI AKAMATWA

Ben Komba/Pwani-Tanzania/09-10-2013/13:38 Kibaha tarehe 09 Oktoba, 2013. Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani linamshikilia Bahati Andulile maarufu kama  Ester umri miaka 18 mfanya kazi wa ndani kwa Bw. Alan Mziray kwa kosa la mauaji ya  mtoto wa bosi wake. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishina Msaidizi Ulrich Matei amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na ameeleza kuwa mwili wa marehemu aitwaye Arafat Alan umri miaka 3 na miezi 4 ulikutwa kwenye dimbwi la maji machafu katika eneo la kiwanja cha mpira Maili Moja majira ya saa 07:20 asubuhi Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani. Kamanda Matei ameongeza kuwa mfanyakazi huyo wa ndani kwa Bw. Alan aliondoka na mtoto huyo tangu tarehe 06/10/2013 majira ya saa 4.00 asubuhi baada ya kutumwa kwenda sokoni kununua mahitaji lakini hakurudi tena na mtoto huyo hadi mwili wake ulipokutwa kwenye dimbwi la maji machafu akiwa amekufa. Mwili wa marehemu baada ya kufanyiwa uchunguzi na Daktari ulikutwa ukiwa na majeraha Kichwani eneo la utosini na baada

NOTI BANDIA

Image