Posts

Showing posts from January, 2013

TANESCO YANUIA KUIMARISHA UTOAJI HUDUMA PWANI.

TANESCO PWANI YAJIPANGA KUBORESHA HUDUMA. Ben Komba/Pwani-Tanzania/30-Jan-13/08:23:59 Shirika la umeme katika mkoa wa Pwani linatarajia kufikia wateja elfu 17500 kwenye kipindi cha mwaka 2013-2014 ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha wanafiki wateja wengi zaidi katika lengo la kuwafikia wateja 250,000 nchi nzima sawa na kupunguza bei ya uunganishaji wa huduma hiyo kwa wateja. ... Meneja wa TANESCO mkoa wa Pwani, BW. JOHNSON MWIGUNE amesema shirika hilo lina mikakati ya kurekebisha utoaji huduma, kwa kuhakikisha kuna kuwa na ongezeko la wateja wapya ili kuongeza makusanyo ya kila mwezi ya shirika, na katika kuvutia wateja shirika limeanza kwa kushusha bei ya kuunganisha huduma hiyo kwa wateja wa kawaida hali ambayo inatoa fursa kwa watu wenye kipato cha kati kupata huduma hiyo. BW.MWIGUNE amesisitiza kuwa shirika lake litaendelea na zoezi la ufungaji wa mita za luku kwa wateja wake katika suala zima la matumizi ya digitali na kuachana na Mita za analogia na zoezi hilo limefanikiwa kwa asi

KIBAHA TC YAPATA GREDA NA GARITAKA

Ben Komba/Pwani-Tanzania/29-Jan-13/19:10:34 Halmashauri ya mji wa Kibaha imezindua Greda la kutengenezea barabara na gari la kubeba taka katika suala zima la uboreshaji wa usafi wa mazingira na uimarishaji w mipango miji kutokana na maeneo yote ambayo hayajapasuliwa barabara kutarajiwa kufikiwa. Akizungumza katika uzinduzi huo Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Kibaha, BI. LEAH LWANJI amebainisha kuwa gari la kubeba taka limetolewa na manispaa ya mji wa GOTLAND kwa ajili ya halmashauri ya mji mara baada ya ujumbe wa viongozi na madiwani kutembelea nchini SWEDEN na wenyeji wao kuwapatia zawadi ya gari hilo ili kusaidia kutunza mazingira ya mji wa Kibaha. BI. LWANJI amesema greda kwa ajili ya kuchonga barabara katika halmashauri ya mji na kukodisha hilo limepatikana kutokana mapato ya ndani ya halmashauri na limegharimu takriban shilingi milioni 528/= za kitanzania, akizungumzia juu ya vitendea kazi vingine kama gllovu, viatu na vinginevyo vimekuja pamoja na gari kwa ajili
Image
WAKALIMANI WA LUGHA YA ALAMA WATAKA SERIKALI IWAAJIRI. Ben Komba/Pwani-Tanzania/27-Jan-13/17:31:20 Serikali nchini imetakiwa kuajiri wakalimani katika nyanja mbalimbali ikiwa sehemu ya kutambua uwepo wa walemavu wa kusikia, ambao kutkana na tatizo linalowakabili inakuwa ngumu kwao kupata taarifa juu ya maambo mbalimbali kutokana na kukosa nyenzo za kujimudu ikiwa pamoja na wakalimani. Mwandishi wa habari hizi nimebahatika kuzungumza na Mwanachama wa chama cha Tanzania Association of Sign Language Interpreters (TASLI), au chama cha wakalimani wa lugha ya alama Tanzania, BW. HABIB UPURUTE ambae amesema wamekuwa wakifanya kazi katika mazingiora magumu kutokana na watu wengi kufikiri kazi hiyo ni nyepesi, na hivyo kuifanya hata serikali kutotupia macho kada hiyo. BW. UPURUTE amebainisha walemavu wa kusikia wamekuwa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali hasa kunakosababishwa na watu wengi katika jamii kutoifahamu barabara lugha ya alama na hivyo kuchangia kuwanyima fursa mbalimbali

SERIKALI YATAKIWA KUAJIRI WAKALIMANI WA LUGHA YA ALAMA.

WAKALIMANI WA LUGHA YA ALAMA WATAKA SERIKALI IWAAJIRI. Ben Komba/Pwani-Tanzania/27-Jan-13/17:31:20 Serikali nchini imetakiwa kuajiri wakalimani katika nyanja mbalimbali ikiwa sehemu ya kutambua uwepo wa walemavu wa kusikia, ambao kutkana na tatizo linalowakabili inakuwa ngumu kwao kupata taarifa juu ya maambo mbalimbali kutokana na kukosa nyenzo za kujimudu ikiwa pamoja na wakalimani. Mwandishi wa habari hizi nimebahatika kuzungumza na Mwanachama wa chama cha Tanzania Association of Sign Language Interpreters (TASLI), au chama cha wakalimani wa lugha ya alama Tanzania, BW. HABIB UPURUTE ambae amesema wamekuwa wakifanya kazi katika mazingiora magumu kutokana na watu wengi kufikiri kazi hiyo ni nyepesi, na hivyo kuifanya hata serikali kutotupia macho kada hiyo. BW. UPURUTE amebainisha walemavu wa kusikia wamekuwa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali hasa kunakosababishwa na watu wengi katika jamii kutoifahamu barabara lugha ya alama na hivyo kuchangia kuwanyima furs

WALEMAVU WA KUSIKIA WAHITAJI WAKALIMANI ZAIDI.

Image
WAKALIMANI WA LUGHA ZA ALAMA WAHITAJIKA KUWASAIDI VIZIWI. Ben Komba/Pwani-Tanzania/26-Jan-13/18:11:47 Chama kinachofanya utafiti juu ya watu wasiosikia nchini, (TADERE} kimefanya warsha maalum kwa wazazi na walimu wenye watoto walemavu na maofisa watendaji wa vijiji katika kuboresha mazingira ya kijamii kwa watu wasiosikia ambao wamekuwa wakipitwa na mambo mbalimbali kutokana na hali yao. Mkurugenzi wa TADERE, BW. NIDROSY MLAWA amesema watu wenye matatizo ya kusikia wamekuwa wakiachwa nyuma katika masuala mbalimbali kutokana na ukosefu wa wakalimani wa kutosha kuwatafsiria matamko mbalimbali yanayotolewa na serikali na kusababisha ushiriki wao kuwa mdogo kama katika mchakato wa katiba mpya unaooendelea. BW. MLAWA amebainisha jamii lazima ikumbuke kuwa walemavu wa kusikia nao wana wajibu wa kupata huduma za kiroho na hivyo ameshauri wakati sasa umefika kwa madhehebu ya dini mbalimbali kuweka mazingira ambayo yatamuwezesha mtu asiyesikia kupata huduma hiyo ya kiroho. Naye kami

JUST IN:WANANCHI WAVAMIA KITUO CHA POLISI KIBITI, WACHOMA NYUMBA ZA ASKARI ~ Father Kidevu

JUST IN:WANANCHI WAVAMIA KITUO CHA POLISI KIBITI, WACHOMA NYUMBA ZA ASKARI ~ Father Kidevu

DALILI ZA NEON MAJIMAJI, ENZI ZILEEEE

DHARAU HAZITOSAIDIA KUTATUA MGOGORO WA GESI. ~ Father Kidevu

MSURUR WA KODI WAWACHOSHA MAMA NTILIE.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/22-Jan-13/16:16:23 Wafanyabiashara katika kata ya Mailimoja wamelalamikia hatua ya ofisi ya kata ya kuwaambia kupima afya na kuwatoza fedha shilingi 5000/=, eti ikiwa ni ada ya upimaji kwa kila mfanyabiashara, jambo ambalo wamelipinga na kushangazwa na hatua hiyo. Mmoja wa Kinamama mfanyabiashara wa chakula BI. FATUMA LAMBA amelalamika kuwa wamekuwa wakibugudhiwa na Bwana afya ya Kata na mgambo wake kwa kutumia muda mwingi kuwatishatisha wafanyabiashara hao ambao wanasema wanachokipta katika biashara hiyo ni kidogo, kulinganisha na halmashauri inavyowachukulia kama vile wanapata mafedha mengi. Mfanyabiashara huyo ameshangazwa na kuzuka kwa msururu wa kodi ambao unamkandamiza mwananchi kisawasawa kiasi cha kuwafanya wananchi kuzua migomo ya hapa na pale, kutokana kujikuta wanawafanyia watu wengine kazi na kuwafaidisha huku familia zao zikiwategemea kwa hali na mali. BI.LAMBA amefikia hatua ya hata kufikiria kuacha biashara hiyo kutokana na usumbufu wa

TRA na WALIPA KODI WAUNDA KAMATI YA PAMOJA PWANI.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/21-Jan-13/15:53:58 Wadau wa kulipa kodi katika mkoa wa Pwani wamechagua kamati ya utendaji katika suala zima la ulipaji kodi kwa maendeleo ya nchi ambayo itakuwa na jukumu la kusimamia na kuratibu maazimio yote yanayofikiwa na kikao cha kila baada ya miezi mitatu chenye lengo la kutathimini masuala mbalimbali kati ya wadau na mamlaka ya kukusanya mapato {TRA}. Uchaguzi huo uliosimamiwa na Meneja wa TRA mkoa wa Pwani ambaye pia ni mwenyekiti wa kikao cha wadau, BIBI. HIGHNESS CHACKY, Ambapo Mwenyekiti wa kamati ya utendaji amekuwa BIBI. HIGHNESS CHACKY, makamu Mwenyekiti BIBI. KAASA MLONJA, katibu ni BW. BAKARI KAPERA, wakati wajumbe wengine wa kamati hiyo ya utendaji ya wadau wa kulipa kodi ni BW. SEHEL ABOUD, BW. WAKIL MURO, BW. ELISANTE NGURE, BW. LAMSON TULYANJE na BW. MAGARE MURYA. Akizungumza mara baada ya uchaguzi huo wa kamati ya utendaji ya wadau wa kulipa kodi, Meneja wa TRA katika mkoa wa Pwani, BIBI. HIGHNESS CHACKY amesema katika mwongozo

South Africa start with a whimper - Football - Al Jazeera English

South Africa start with a whimper - Football - Al Jazeera English

PHOTOS?

POLICE FAMILY DAY NA SHERIA KANDAMIZI.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/17-Jan-13/14:04:59 Katika siku ya kuadhimisha POLICE FAMILY, Jeshi la Polisi katika mkoa wa Pwani limefanya maandamano ya amani ambayo yaliishia katika kituo cha afya Mkoani katika halmashauri ya mji wa Kibaha na kufanya shughuli za usafi katika maeneo ya kituo cha afya. Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Pwani, Kamishna msaidizi wa Polisi ULRICH MATEI akizungumza katika maadhimisho hayo amesemaleo ndio siku ambayo Jeshi la Polisi katika mkoa wa Pwani linaadhimisha siku ya Familia na Polisi na kati ya mambo ambayo walipanga kuyafanya ni kufanya usafi maeneo ya kituo cha afya Mkoani ikiwa pamoja na kujadili changamoto na mafanikio ya kiutendaji waliyoyakabili katika mwaka 2012. Ambapo Kamishna msaidizi MATEI amebainisha kuwa mkoa wa Pwani umeonyesha kupata mafanikio ya kuridhisha katika nyanja ya kiuslama ingawa palikuwa na matishio kadhaa ambayo yaliweza kutokea katika nyakati tofauti, akatoa vurugu kati ya wakulima na wafugaji wilayani Rufiji ambazo zilisabab

SHERIA ZA KAZI.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/14-Jan-13/18:59:14 Kukosekana kwa elimu juu ya sheria za kazi imesemekana ni kikwazo kikubwa kwa upatikanji wa haki sehemu za kazi kunakosababishwa kwa kiasi kikubwa wa uwepo wa vyama vya wafanyakazi. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Msuluhishi mwandamiziwa tume ya utetezi na usuluhishi katika mkoa wa Pwani, BW. MWANGATA MAKAWA amesema viongozi wa vyama vya wafanyakai wanajua juu ya ukosefu wa elimu juu ya sheria za kazi kwa wanachama na waajiri. BW, MAKAWA amebainisha kuwa ni wajibu wa Bwana kazi ambaye anapata wasaa kukagua maeneo ya kazi kumshauri mwajiri au mwajiriwa hatua za kuchukua anapoona haki yake inakiukwa, lakini ukosefu wa mafungu ya kuwezesha kutolewa elimu juu ya mfanyakazi, ndiyo kikwazo kikubwa kinachokwamisha uimarishaji wa haki za wafanyakazi. Msuluhishi mwandamizi huyo wa tume ya usuluhishi na utetezi, BW. MAKAWA ameweka wazi kuwa utoaji wa mafunzo ni kitu muhimu kwani uzoefu unaonyesha sehemu ambazo zinatoa elimu juu ya sheri

MVAMIZI AUWAWA

AUWAWA KWA UVAMIZI Ben Komba/Pwani-Tanzania/14/01/2013/16:13:17 Mtu mmoja ameuwawa na watu wenye hasira kali kufuatia kuvamia nyumba ya BI. MWAJUMA SHAABAN katika eneo la Kwa Mathias mjini Kibaha leo majira ya alfajiri baada ya kukamatwa akiwa ndani ya nyumba. Mwandishi wa habari hizi akiongea na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Kamishna msaidizi ULRICH MATEI amesema tukio hilo limetokea alfajiri ya leo ambapo Jambazi huyo akiwa na wenzie walivamia nyumba ya Dada hiyo. Kamanda MATEI amebainisha kuwa mtu huyo ambaye hajulikani jina lake wala mahali anapoishi anakadiriwa kuwa na umri ya miaka 20 mpaka 25 aliuwa kwa kwa kupigwa na wananchi waliojichukulia sheria mkononi baada ya mwizi huyo na wenzie watatu kuvamia nyumba ya BI. MWAJABU SHAABAN ambaye ni mfanyabiashara. Ambapo walifanikiwa kuingia ndani kwa mfanyabiashara hiyo anayeishi maeneo ya UMWERANI kwa MATHIAS kwa kuvunja mlango kwa kutumia jiwe la FATUMA, waliiba DVD PLAYER moja yenye thamani ya shilingi ya 65,000, fedha t

IS IT TRUE? tell us

MUHAMMAD AND THE SATANIC VERSES Muhammad Spoke the Satanic Verses - The Evidence and Proof INTRODUCTION MUHAMMAD SPOKE THE SATANIC VERSES - THE EVIDENCE AND PROOF THE EVIDENCE: THE EARLY ISLAMIC SOURCES DISCUSSION / REVIEW OF THE SIRA MATERIAL ON THE SATANIC VERSES. EVIDENCE FROM SAHIH HADITH THAT MUHAMMAD SPOKE THE SATANIC VERSES FROM THE QURAN AN ISLAMIC SCHOLAR'S COMMENTARY (TAFSIR) OTHER COMMENTS FUNDAMENTALIST MUSLIM'S COMPLAINTS AND DENIALS CONCLUSIONS BIBLIOGRAPHY INTRODUCTION One of the most embarrassing events in Muhammad's life occurred when Satan put his words in Muhammad's mouth. Muhammad spoke Satan's words as the word of God. This event is documented by several early Muslim scholars and referenced in the Hadith and Quran. Later Muslims, ashamed that their self declared prophet spoke Satan's words, denied the event occurred. A myriad of excuses and denials have been put forth by these later Muhammadans to cover up Muhammad's

SKAUTI MKUU KUPATIKANA KARIBUNI.

MCHAKATO WA KUMPATA SKAUTI MKUU. Ben Komba/Pwani-Tanzania/1/13/2013/19:21:17 Kamishna wa skauti katika mkoa wa Pwani, BW. HAMIS MASASA amempongeza mkuu wa mkoa wa mkoa wa Pwani kwa kuweza kushinda nafasi ya kwanza katika mchakato wa kumpata Skauti mkuu wa Tanzania. Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi mjini Kibaha, Kamishina wa skauti mkoa wa Pwani, BW. MASASA amesema kitendo cha BIBI. MWANTUM MAHIZA kuongoza katika kinyang'anyiro hicho kwa kuwashinda wagombea wengine wawili ambao wamepata kura 22 kila mmoja ambao ni BW.ABDULKARIM SHAH Mbunge wa Mafia na BW. KAJUNGUMJULI kutoka Mkoa wa Mwanza, ambapo BIBI.MAHIZA ameibuka na kura 47. BW. MASASA amesema baada ya hatua hiyo majina matatu yatawasilishwa kwa Rais wa Chama cha skauti Tanzania, ambaye ni Waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi BW. SHUKURU KAWAMBWA kama utaratibu unavyoelekeza ambaye naye atayawakilisha kwa mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania, Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, DOKTA JAKAYA KIKWETE ambaye yey

SACCOS YA WALIMU YASOTESHA WANACHAMA.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/ Wanachama wa SACCOS ya walimu wilayanai Kibaha kwa takiban wiki mbili wamekuwa wakisotea mikopo kutoka katika SACCOS kwa ajili ya kutaka kutumia fedha hizo kwa matumizi mbalimbali bila mafanikio. Mmoja wa walimu nilioongea naye ambaye hakupenda jina lake kuwa wazi, amesema wamekuwa wakifia katika Ofisi hizo za na kumbiwa bado hawajapata mrejesho kutoka halmashauri na hasa kutokana na fedha hizo kukata moja kwa moja katika mshahara. Mwalimu huyo anashangazwa kwa nini kuwepo na mizunguko ili hali wanachama wamekuwa wanaweka akiba kama wanavyostahili iweje leo wanahitaji kuchukua fedha za kwa ajili ya kutumia kwa ajili ya maandalizi ya watoto shule wanazikosa katika wakati na kuambulia kuzungushwa hali ambayo inawatia wasiwasi iwapo akiba zao zipo katika mikono salama. Mwalimu mwingine naye ameongeza yeye amesikia kuwa halmashauri ya mji imeshatoa fedha shilingi milioni 11 kwa SACCOS hiyo ikiwa marejesho ya makato yaliyofanywa na halmashauri kutokana na m

UWT WAHIMIZWA UPENDO

UWT WAHIMIZWA UPENDO NA MSHIKAMANO. Ben Komba/Pwani-Tanzania/09-01-2013 Wanawake nchini wametakiwa washikamane kwa umoja wao kwani uchaguzi umeshakwisha na kilichobaki sasa ni kujenga chama kwa ajili ya kukiimarisha chama kuelekea chaguzi zijazo. Hayo yamezungumzwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya wanawake Mkoa wa Pwani, BI. ZAINAB VULU katika baraza la mkoa la jumuiya hiyo, ambalo kati ya mambo mengine alisisitiza kuvunjwa kwa kambi. BI.VULU amebainisha ili wanawake waweze kuyfikia malengo yao hawana budi kupendana, kushikamana iliu wakiwezeshe chama chao kufanya vizuri katika uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi kwa kuhakikisha maeneo yanayoshikiliwa na wapinzani yanarudi mikononi mwao. Amefafanua kuwa katika kuhakikisha wanarejesha maeneo yanayoshikiliwa na wapinzani watahakikisha wanatekeleza ahadi zilizotolewa wakati wa kampeni ya uchaguzi, ikiwa pamoja na kuwashughulikia watendaji ambao watakuwa hawatimizi majukumu yao ipasavyo. Mwenyekiti huyo wa Jumuiya ya wanawak

BARAZA LA BIASHARA LAZINDULIWA KIBAHA.

BARAZA LA BIASHARA LAZINDULIWA KIBAHA. Ben Komba/Pwani-Tanzania/ Halmashauri ya wilaya ya Kibaha imezindua rasmi baraza la biashara katika kuweesha majadiliano na mijadala ya mashauriano ya mara kwa mara kwa watu binafsi na serikali ikiwa pamoja na kuboresha mazingira ya shughuli wanazofanya. Akizungumza katika uzinduzi huo Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kibaha, BIBI. TATU SELEMANI amesema kuwa Baraza hilo litajumisha sekta binafsi, Asasi zisizokuwa za kiserikali na sekta za umma wale wote wanaohusika na utoaji wa huduma kwa jamii. BIBI. SELEMANIameongeza hatua hiyo kuonyesha kuwa serikali inatambua kuwa changamoto ya kuleta maendeleo ya nchi haiwezi kuachiwa sekta moja, bali malengo yanaweza kufikiwa kwa sekta hizo kila mmoja ikimuweesha mwenzake, na ametaja kuwa ni ubia ambao ni mfumo sahihi wa kufikia malengo ya Taifa ya kutoa huduma ya kukidhi mahitaji ya jamii ambayo yasingeweza kufikiwa pasipo nguvu ya pamoja. Awali akisoma taarifa ya kwa niaba ya mkuu

Muslim clerics warned against hate sermons | Magazetini - Soma Magazeti ya Tanzania - Read Tanzania Newspapers

Muslim clerics warned against hate sermons | Magazetini - Soma Magazeti ya Tanzania - Read Tanzania Newspapers

MGANGA AFUNGA KITUO AWAACHA HOI WANANCHI.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/01-Jan-13/15:42:58 Katika hali ya kushagngaza katika kijiji cha Milo kata ya Vigwaza wilayani Bagamoyo, mganga wa kituo cha afya kijijini hapo amefunga kituo na kuondoka na funguo kwa kile ambacho amedai kufuatilia mafao yake na kuacha wananchi bila huduma hiyo muhimu. Daktari huyo BW. ELIAS FELICIAN ambaye alikuwa akisaidiwa na wahudumu wawili wa kijiji hicho, BW. MICHAEL MAJALIWA na mwenzie BI. ASHURA MWINYI, wamebaki wamepigwa butwaa baada ya Mganga huyo wa kituo kufunga kituo hicho cha afya na kuondoka na funguo tofauti na alivyokuwa akifanya awali ambapo walikuwa wanaachiwa funguo na kuendelea kutoa huduma hiyo muhimu. Mmoja wa Wahudumu hao, BW. MICHAEL MAJALIWA amebainisha wao walichaguliwa na mkutano mkuu wa kijiji kuwa wahudumu wa afya ya msingi kijiji hapo, na wamekuwa wakilipwa shilingi 15000/= kwa mwezi katika nyakati za mwanzo, lakini kila muda ulivyokuwa unasonga mbele, wakawa hawapati stahili zao kutoka serikali ya kijiji lakini kwa sasa wan

WAZABUNI FEKIO CHANZO CHA KUZOROTA MAENDELEO.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/01/01/2013/15:03:22 Kampuni iliyopewa zabuni ya kujenga matanki ya maji katika kijiji cha Milo kata ya Vigwaza wilayani Bagamoyo imewatelekeza wafanyakazi wake wake bila kuwapatia stahili zao na kuwafanya kuishi katika maisha ya mashaka hali ambayo inatishia ubora wa kazi wanayofanya. Mwandishi wa habari hizi akizungumza na wafanyakazi wa mzabuni huyo ambaye amepewa kazi ya kujenga matanki katika kijiji hicho, kupitia mradi wa maji unaofadhiliwa na Benki ya Dunia wenye lengo la kusambaza maji maeneo ya vijijini ambapo kupitia fedha idara za maji za halmashauri wanasimamia utafutaji wa vyanzo vipya na maji na kusambaza.. Mwandishi ameshuhudia ujenzi wa kusuasua wa matenki makubwa ya kuhifadhia maji katika kijiji cha Milo, hali inayosababishwa na mkandarasi kutokuwa makini katika utekelezaji wa shughuli hiyo ambayo imenuia kumaliza tatizo la maji katika kijiji hicho kilichopo umbali wa kilometa 25 kutoka barabara ya Morogoro. Mmoja wa wafanyakazi wa kampu

VIONGOZI WANG'OLEWA BAGAMOYO.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/1-1-2013 Wimbi la wananchi kung'oa viongozi wao kwa sababu mbalimbali limeshika kasi wilayani Bagamoyo na kwa wananchi kuchukua hatua ya kuwawajibisha viongozi wao kwa kukiuka taratibu za utumishi wa umma kwa kuweka mble maslahi binafsi badala ya wananchi kwa ujumla. Mwandishi wa habari hizi ameshuhudia katika kipindi cha wiki moja wanachi wakichukua hatua ya makusudi ya kuwang'oa viongozi hao, wa Vijiji vya Ruvu Darajani na kijiji cha Milo vilivyopo katika Kata ya Vigwaza wilayani Bagamoyo katika mkoa wa Pwani mbele ya diwani wa kata ya Vigwaza, BW. MBEGU DILUNGA na mtendaji wa Kata BW. MASKUZI MASKUZI. Baadhi ya madai ambayo yamewagharimu uongozi katika vijiji vyote viwili ni matatizo ya uuzaji wa ardhi kiholela kinyume na taratibu za sheria, ambapo katika kijiji cha Ruvu Darajani wananchi waliujia juu wa uongozi kwa kutowashirikisha kikamilifu katika ugawaji wa maeneo na walipohojiwa katika kikao cha dharura cha kijiji hawakusema ukweli pamoj