Posts

Showing posts from July, 2012

WANAFUNZI WAANDAMANA KUFUATIA MGOMO WA WALIMU-KIBAHA.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/7/31/2012/15:07 Katika hatua inayoashiria kuwa hali inayosababishwa na mgomo wa walimu unaoendelea nchi nzima athari zake sasa zimefika mbali baada ya wanafunzi wa shule za msingi za Mailimoja na Maendeleo za mjini Kibaha kuandamana wakidai haki yao ya kufundishwa kama ilivyo ada. Wanafunzi hao ambao walikuwa wakijiongoza wenyewe huku wakipita barabara kubwa ya Morogoro wakiimba nyimbo za kudai haki ya kufndishwa na wakiitaka serikali iwalipe fedha walimu ambazo wanataka ili waweze kuendelea na masomo. ... Mmoja ya wanafunzi ambaye nimeongea naye amesema wameamua kuandamana baada ya kuona walimu wao wanasini halafu tena wanaondoka bila kwenda madarasani kama ilivyo ada. Kutokana na kadhia hiyo ilimbidi Diwani wa Kata ya Mailimoja kufanya kazi ya ziada akishirikiana na askari kata ili kujaribu kuwaongoza wanafunzi hao ambao walionekana kupagawa na kuchoka kutokana umbali mrefu waliotembea bila wahusika wa elimu wa kata au mji kujitokeza kuwaeleza neno lolot

VIONGOZI WA DINI WAOMBWA KUSAIDIA SENSA

Ben Komba/Pwani-Tanzania/12/07/27/8:43:24 Mkuu wa Mkoa wa Pwani BIBI. MWANTUMU MAHIZA amewataka viongozi wa dini kukemea kuporomoka kwa maadili miongoni mwa wanajamii kunakosababishwa na changamoto mbalimbali za kimaisha zinazokabili ulimwengu. BIBI. MAHIZA amesema vitendo vya uporomokaji wa maadili vimekuwa vinaongezeka kila uchao, mpaka kufikia watu ambao wanaaminika katika jamii kujikuta nao wametubukia katika vitendo vya uvunjaji wa maadili, akitoa mfano kuwa siku hizi kusikia Padri kambaka muumini si kitu cha ajabu au mwalimu / Shekhe kabaka imekuwa kitu cha kawaida. Amewaomba viongozi wa dini kutumia nafasi waliyonayo kuwapatia elimu waumini wao katika suala zima la kujenga jamii ambayo itakuwa inaheshimu maadili, hususan katika kupambana na vitendo vya ubakaji ambavyo vinatoa nafasi kubwa ya kuongezeka kwa maambukizi ya ugonjwa hatari wa UKIMWI. Akizungumzia suala la Sensa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, BIBI. MWANTUMU MAHIZA amewaomba viongozi wa dini na wazee maarufu kutumia naf

MAONI KATIBA KATA YA MAILIMOJA.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/2012-07-22/1:54:32 PM Shirika lisilo la kiserikali la Pwani-DPA kwa kushirikiana na ofisi ya serikali ya Mailimoja wametoa mafunzo ya awali kwa wakazi wa mtaa huo tayari kukutana na tume ya kukusanya maoni juu ya uandikaji wa katiba mpya ili kutoa fursa yakuwepo na ufahamu juu ya katiba angalau kidogo kwa wakazi hao. Mwezeshaji katika mazungumzo hayo yanayohusiana na utoaji wa elimu ya uraia kwa jamii katika kuwajengea uwezo wananchi wa kujadili kuhusiana na uandikaji wa katiba mpya, kutoka shirika lisilo la kiserikali la YOUTH PARTNERSHIP COUNTRYWIDE, BW. MARTIN MUNG'ONGO amesema kuwa mageuzi ya kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni ni jambo ambalo haliepukiki toka wakati ndio unaozungumza na hivyo wananchi hawana budi kutumia fursa hii adimu kuamua mambo yatakayokuwa na manufaa kwa kizazi kijacho. Ameongeza kwa jamii kukubali kufanya mabadiliko ambayo yananuia kuleta mabadiliko ya kiuchumi, kisiasa na kitamaduni ndipo hapo nchi inapopiga hatua kuelekea

MAANDALIZI YA SENSA YAPAMBA MOTO PWANI.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/17-Jul-12 9:46 AM Mafunzo ya sensa ngazi ya pili kwa ajili ya kuwaandaa makarani na wasimamizi ambao wamelengwa kwenda kulisimamia zoezi hilo katika maeneo watakayopangiwa. Kiongozi wa timu ya wakufunzi wa sensa Mkoa wa Pwani, DOKTA. SIMON MSANJILA ambaye pia ni mkuu wa kitivo cha Sayansi na Teknolojia, chuo kikuu cha Mzumbe amesema mafunzo hayo ni zoezi ambalo limelenga kuboresha ukusanyaji wa takwimu. DOKTA. SIMON amefafanua kundi hilo ambalo linapatiwa mafunzo ni kutoka katika idara mbalimbali ikiwa elimu, mipango na uwakilishi wa makundi maalum likiwemo la walemavu. Akizungumzia changamoto zinazokabili maandalizi ya zoezi la sensa katika mkoa wa Pwani, BW. MSANJILA amesema ni kuchelewa kwa vifaa muhimu kwa ajili ya zoezi hilo, kuchelewa kwa uwezeshaji kwa washiriki wa mafunzo, ambavyo baadhi wameweza kuzishinda. Amesisitiza kuwa zoezi la kuhesabu limegawanyika katika makundi manne ambayo ni kaya za kawaida ambao watakutwa nyumbani, kaya maalum yaan

WAKAZI KIBAHA WATAKA BARABARA YAO.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/07/15/2012/09:00:39 Wakazi wa mtaa wa Mkoani Kitalu "b" katika halmashauri ya mji wa Kibaha wameshangazwa na hatua ya mhandisi wa barabara kuonyesha katika nyaraka zake kuwa baarbara ambazo zimechongwa ni kilometa 11, ili hali kazi ambayo imefanyika ni uchongaji wa kilometa 4, na kuwafanya wananchi kuhoji ni wapi kilometa 7 nyingine zilizobaki zimechongwa wapi. Diwani wa kata ya Tumbi BW. RAJAB MBENA MAKALA akizungumumza na wakazi wa eneo hilo amesema suala la kuchongewa kilometa pungufu ya mahitaji kumeleta sintofahamu kubwa kati ya wenyeviti wa mtaa katika halmshauri ya mji wa Kibaha hususan katika mtaa MKOANI BLOCK B, kutokana na halmashauri kuchonga barbara ambazo hazikuwa katika mradi ambao umeibuliwa na wananchi. Hata hivyo Diwani MAKALA ambaye amepitia tiketi ya chama cha demokrasia na maendeleo, amechukua nafasi hiyo kuwapa wananchi habari njema kuhusiana na miradi ya maendeleo ambayo imepitishwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2012/2

MATREKTA YAPUNGUA BEI, KILIMO JUU?

Ben Komba/Pwani-Tanzania/13-Jul-12/18:33:10   Mkuu wa wilaya ya Kibaha BIBI. HALIMA KIHEMBA amewataka wawekezaji katika kilimo kutumia fursa ambayo imetolewa na serikali ya kupunguza bei ya matrekta katika kuwawezesha wakulima kuzalisha chakula kwa wingi katika harakati za suala zima la kukuza uchumi unaotegemea kilimo katika sehemu kubwa toka kuna ardhi yenye rutuba ya kutosha.   BIBI. KIHEMBA ameongea hayo akizindua shamba la kilimo mseto katika kijiji cha Lukenge kwenye kata ya Magindu wilayani Kibaha mkoa wa Pwani, ambalo linamilikiwa na mwekezaji wa ndani ambaye ni mfugaji BW. TANGONO MAHOMBELO KASHIMBA kupitia kampuni yake ya uwekezaji ya TWO BROTHERS INVESTMENT, ambapo amesema amefurahishwa na jinsi mwekezaji huyo alivyoweza kujenga miundombinu katika eneo lake hilo, ikiwa pamoja na kuchimba bwawa la maji ambalo kwa sasa limekuwa tegemeo kwa jamii ya hapo.   BIBI. KIHEMBA ameongeza kwa kuwekeza katika kilimo mseto imewezesha uwepo wa matumizi bora ya ardhi mpango ambao ume

WAKAZI WA MAILIMOJA WACHANGISHANA KUJENGA BARABARA

Ben Komba/Pwani-Tanzania/08-07-2012/10:30 Wakazi wa mtaa Muheza katika halmashauri ya mji wa Kibaha, wamekusanya jumla ya shilingi milioni 1.3, kwa ajili ya kurekebisha eneo korofi katika bonde la Mkatajika, baada ya kilio cha muda mrefu kwa halmashauri kukarabati barabara katika kata ya Mailimoja kugonga mwamba. Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Muheza BW. MOHAMED LINGOWECHE amesema wakazi wa mtaa wake wamechukua hatu hiyo kufuatia maombi yao ya kuchongewa barabar katika Kata kama kipaumbele katika kata yao kutopata majibu maridhawa, ili hali wao wakiendelea kutaabika katika msimu wa mvua. BW. LINGOWECHE amebainisha wengi wa wakazi wake ni wakulima na wafanyabiashara ndogondogo, na baada ya kuchangishana na kupatikana kiasi cha fedha, wameweza kununua mawe makubwa lori mbili,sementi mifuko 19, mchanga lori 2 na kokoto lori moja. Naye Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Tawi la Muheza, BW. AURELIUS MBENA amesema kila mwaka wao wamekuwa wakipeleka suala la kutengenezewa Barbara kama kipaum

MWEKEZAJI ASAIDIA KIJIJI/ JENGO LA PCCB PWANI LAZINDULIWA

Ben Komba/Pwani/Tanzania/7/6/2012 9:31:29 AM Wakazi wa kijiji cha Lukenge Kata ya Magindu wamewezeshwa kupata maji safi ya kunywa , josho na bwawa la kufuga samaki ambalo halitakauka katika kipindi chote cha mwaka. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Kaimu Mkurugenzi wa kampuni ya TWO BROTHERS INVESTMENT, inayomilikiwa na wawekezaji wa ndani, BW. YUSUPH MJEMA amesema kampuni yao inajihusisha na kilimo mseto, ufugaji wa samaki, kunenepesha ng,ombe na kilimo kwanza. BW. MJEMA amebainisha kuwa huduma hizo zinatarajiwa kuzinduliwa rasmi na mkuu wa mkoa wa Pwani, BIBI. MWANTUMU MAHIZA siku ya Jumanne Julai 10 mwaka huu katika shamba hilo lenye eka 400. Amefafanua kati ya eka hizo 400, bwawa pekee lina urefu na urefu wa mita 186 na kina cha futi 40, na mpaka sasa wameshaotesha mbegu za samaki 500 ambazo wamezinunua kutoka SUA za samaki aina ya Sato. BW. MJEMA ameongeza kuhusiana na suala la kilimo kwanza mpaka sasa wamelima mahindi ambayo yanatarajiwa kuvunwa wakati wowote katika ek