Posts

Showing posts from November, 2013

NYUKI MKOMBOZI KIUCHUMI

Ben Komba/Pwani-Tanzania/29-11-2013/10:41 Taasisi wa masuala ya haki za binadamu na maendeleo WAHABIMA wanuia kusaidia wajasiriamali wa mjini wa Kibaha katika suala zima la ufugaji wa nyuki wa asali ili kuongeza kipato cha familia. Akizungumza katika uzinduzi wa warsha inayohusiana na ufugaji nyuki wa asali, Mshauri mwelekezi, BW.DOMINIC KIWELE amewaeleza washiriki kuwa ufugaji wa nyuki ukifanywa kwa kuzingatia ushauri wa kitaalamu unaweza   kukikomboa familia na umaskini wa kipato ambao ndio tatizo kubwa miongoni mwetu. BW.KIWELE amebainisha kuwa gharama za kuanzisha ufugaji wa nyuki ni ndogo kulinganisha na ufugaji mwingine wowote kwani ili kuweza kufuga nyuki itakubidi kuingia gharama kidogo kwa ajili ya kutengenezea mzinga ambao utatumika kutegea nyuki ukiwa na chambo chake ambacho ni nta inayozalishwa na nyuki. Mshauri mwelekezi huyo, BW.DOMINIC KIWELE amefafanua kuwa watu wengi wamekuwa wanaogopa kufuga nyuki wakihofiwa kushambuliwa nao kitu ambacho sio loazim

MAJANGA YA AJALI BARABARANI.

SIKU YA MAJANGA YA AJALI ZA BARABANI Ben Komba/Pwani-Tanzania/26-11-2013/10:35 Katika maadhimisho ya siku ya majanga ya ajali za barabarani ulimwenguni ambayo inafanyika kila jumapili ya tatu ya mwezi wa Novemba ya kila mwaka na nchi mbalimbali zimekuwa zinaadhimisha siku hiyo na mwaka huu maadhimisho hayo kitaifa yamefanyika mjini Kibaha katika mkoa wa Pwani. Akizungumza katika maadhimisho hayo Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani nchini, Kamishna msaidizi  MOHAMED MPINGA amesema ikumbukwe kuwa ajali za barabarani ni janga la kiulimwengu katika sekta ya afya, na zinachangia kiasi cha vifo vya watu milioni 100.3 kwa mwaka na kusababisha majeruhi watu milioni 20 mpaka milioni 50 kwa mwaka. Kamanda MPINGA amebainisha ajali za barabarani zinashika nafasi ya nane kwa kusababisha vifo kilimwengu,na kama hatua madhubuti hazitachukuliwa kama tafiti zinavyoonyesha mpaka mwaka 2020 kuna uwezekano mkubwa wa ajali kushika namba tano kuwa ndio chanzo kikubwa kinachosababisha ajali ulimwenguni

WANANCHI PWANI WASHAURIWA KUTHAMINI ELIMU

Ben Komba/Pwani-Tanzania/24-11-2013. Wananchi Mkoa wa Pwani wametakiwa kutumia fursa ya kupata elimu kutokana nauwepo wa taasisi za kutoa elimu katika suala zima la kuhakikisha kila mwananchi mwenye uwezo na kujitambua anapata elimu ambayo itaweza kumsaidia maishani. Akizungumza katika mahafali ya nane ya Chuo cha Ufundi Masakamali kilichopo Msata wilayani Bagamoyo katika mkoa wa Pwani, Mkaguzi msaidizi wa Polisi usalama Barabarani wilaya ya Bagamoyo, INNOCENT SULLE amewataka wazazi kuhakikisha kuwa wanawapeleka watoto wao shule ili waweze kuja kuwasaidia na kujisaidia maishani. BW.SULLE amewaambia wanafunzi hao wahitimu kutokubali kuishia hapo walipofikia na kuwataka wajiongeze ili kupiga hatua kubwa katika masomo kwa kujiunga na vyuo vingine vyenye kutoa tunzo za juu zaidi. Mkaguzi huyo wa usalama barabarani ametoa mfano wa waendesha bodaboda wa Msata ambao wengi wao hawana leseni ya kuendesha chombo hicho cha moto pamoja na uwepo wa karibu wa chuo cha ufundi Msa

WAKALA WA HALMASHAURI AKWAA KISIKI.

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/11/20/2013 10:22:20 AM Wakala wa ukusanyaji wa ada ya maegesho mjini Kibaha ya MSOLOPA INVESTMENT COMPANY LTD, imewataka wananchi kuelewa lengo la zoezi wanaloliendesha katika suala zima la uboreshaji wa mazingira ya mji wa Kibaha. Akiongea na mwandishi wa habari hizi mjini Kibaha, BW. IBRAHIM MAULID MSOLOPA amesema wao kazi yao kubwa ni kukusanya madeni ya taasisi mbalimbali kwa makubaliano maalum. BW.MSOLOPA ameongeza wajibu wao mjini Kibaha ni kuhakikisha wanasimamia mpango mzima wa kuupanga mji wa Kibaha ,ikiwa pamoja na kukusanya ada ya maegesho ambayo imepingwa vikali na wakazi wenye magari na w asio na magari kutokana na halmashauri kutotenga eneo la maegesho, ingawa kuna maeneo ambayo yangeweza kutumika kama maegesho ya muda. Akitetea hatua ya Kampuni yake kukusanya ada ya maegesho, BW.MSOLOPA amebainisha yeye yupo pale kisheria ikiwa pamoja na kuingia mkataba na halmashauri wa kukusanya ada ya maegesho na takataka. Amebainisha k

WANANCHI WACHUKUA MAAMUZI MAGUMU

Image
WAKOKOTA MAGARI WA JIJI WASHAMBULIWA Ben Komba/Pwani-Tanzania/11/13/2013 12:41:27 PM Hali ya uwepo wa vurugu za mara kwa mara im eanza kuota mizizi kufuatia uwepo kwa sheria ndogo ambazo zinaleta utata mkubwa wa wananchi, kiasi cha kusababisha wananchi kuamua kuchukua hatua mikononi katika suala zima la kutetea na kulinda haki zao. Leo mwandishi wa habari hizi ameshuhudia kushambuliwa kwa mfanyakazi mmoja wa gari la kukokota magari, mara baada ya mtu huyo ambaye jina lake halikupatikana kufunga mnyonyoro gari la Mam,a mmoja ambaye alipaki gari lake mbele ya soko ili kwenda kupata mahitaji ya nyumbani. Ndipo gari hiyo maarufu kama BREAKDOWN liliposegea karibu na gari lilokuwa limeegeshwa mbele ya soko na mmoja wa watumishi wa kampuni hiyo alitoa mnyonyoro na kulifnga gari hiyo kitu ambacho wananchi walioshuhudia tukio hilo hawakukubaliana nacho na kuanza kuwashambulia wahusika. Katika harakati za kutuliza hali ya mambo, Diwani wa Kata ya Mailimoja, BW. ANDREW LUGANO amewatak
Image
MBONDE FOUNDATION YASAIDIA WANAFUNZI KIBAHA Ben Komba/ Pwani-Tanzania.12-Nov-13 10:34:25 AM Taasisi isiyo ya kiserikali ya MBONDE FOUNDATION inayoshughulika na watoto wanaoishi katika mazingira magumu na yatima imetoa vifaa vya shule kwa wanafunzi zaidi ya 40 wa shule ya msingi Boko Timiza,halmshauri ya mji wa Kibaha katika suala zima la utekelezaji wa shughuli za kijamii. Msemaji wa Taasisi ya  MBONDE FOUNDATION yenye maskani yake mjini Dar es Saalam, BW. WILSON EZEKIEL amesema msaada huo kwa watoto ambao ni viatu, madaftari, Kalamu na Peni ni mwanzo wa usaidizi kwa watoto hao mpaka watakapofikia elimu ya sekondari. BW.EZEKIEL ameongeza watoto hao ambao kila mmoja amepatiwa namba maalum ya utambulisho na tayari wameshatengewa bajeti ya mwaka mzima kwa ajili ya mahitaji yao muhimu ya shule. Mmoja wa wanafunzi ambao wamefaidika na msaada huo ameishukuru taasisi hiyo kwa kuwapatia msaada huo ambao utawasaidia kufanya vizuri katika masomo yao na halikadhalika wamewasaidia wazazi wao kw
Image
MBONDE FOUNDATION YASAIDIA WANAFUNZI KIBAHA Ben Komba/ Pwani-Tanzania.12-Nov-13 10:34:25 AM Taasisi isiyo ya kiserikali ya MBONDE FOUNDATION inayoshughulika na watoto wanaoishi katika mazingira magumu na yatima imetoa vifaa vya shule kwa wanafunzi zaidi ya 40 wa shule ya msingi Boko Timiza,halmshauri ya mji wa Kibaha katika suala zima la utekelezaji wa shughuli za kijamii. Msemaji wa Taasisi ya  MBONDE FOUNDATION yenye maskani yake mjini Dar es Saalam, BW. WILSON EZEKIEL amesema msaada huo kwa watoto ambao ni viatu, madaftari, Kalamu na Peni ni mwanzo wa usaidizi kwa watoto hao mpaka watakapofikia elimu ya sekondari. BW.EZEKIEL ameongeza watoto hao ambao kila mmoja amepatiwa namba maalum ya utambulisho na tayari wameshatengewa bajeti ya mwaka mzima kwa ajili ya mahitaji yao muhimu ya shule. Mmoja wa wanafunzi ambao wamefaidika na msaada huo ameishukuru taasisi hiyo kwa kuwapatia msaada huo ambao utawasaidia kufanya vizuri katika masomo yao na halikadhalika wamewasaidia wazazi wao kw

RC AVALIA NJUGA MIGOGORO KATI YA WAKULIMA NA WAFUGAJI.

Image

MAGARI YAKWAMA NJIA YA TANGA

Image

WAFUGAJI WAILILIA SERIKALI

Image

MASAHIHISHO WAFUGAJI WAILILIA SERIKALI

WAFUGAJI WAILILIA SERIKALI Ben Komba/PWANI-TANZANIA/11/7/2013 9:33:09 AM Wafugaji nchini wamemtaka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DKT.JAKAYA KIKWETE Awabebeshe  dhamana viongozi wa mkoa Morogoro juu ya watu waliokufa kufuatia mapigano kati ya ushirika unaosimamia masuala ya maliasili na uhifadhi wa misitu ya MWANU na wafugaji. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Katibu wa wafugaji Tanzania BW.GEORGE KIFUKO amesema tatizo hilo linasababishwa na viongozi wa mkoa wa Morogoro kutokana na uanzishaji wa kamati ambayo inatekeleza operesheni ya kukamata mifugo. BW. KIFUKO amesema kuwa Mkuu wa wilaya ya Mvomero ndio ameanzisha zoezi hilo kwa maslahi binafsi kwa kukamata ng’ombe na kuwalazimisha wafugaji kulipa shilingo milioni 10 ili kuweza kukomboa ng’ombe hao takriban 300, Jambo ambalo wafugaji hawajakubaliana nalo na kutaka waende mahakamani kwa hatua zaidi  jambo ambalo wakamataji hao wa mifugo walikataa. Amemtaka Rais KIKWETE afikie hatua achukue maamuzi ya kuzuia unyang’any

WAFUGAJI WAILILIa SERIKALI

Ben Komba/PWANI-TANZANIA/11/7/2013 9:33:09 AM Wafugaji nchini wamemtaka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DKT.JAKAYA KIKWETE wabebe dhamana juu ya watu waliokufa kufuatia mapigano kati ya ushiriki unaosimamia masuala ya maliasili na uhifadhi wa misitu ya MWANU. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Katibu wa wafugaji Tanzania BW.GEORGE KIFUKO amesema tatizo hilo linasababishwa na viongozi wa mkoa wa Morogoro kutokana na uanzishaji wa kamati ambayo inatekeleza operesheni ya kukamata mifugo. BW. KIFUKO amesema kuwa Mkuu wa wilaya ya Mvomero ndio ameanzisha zoezi hilo kwa maslahi binafsi kwa kukamata ng’ombe na kuwalazimisha wafugaji kulipa shilingo milioni 10 ili kuweza kukomboa ng’ombe hao takriban 300, Jambo ambalo wafugaji hawajakubaliana nalo na kutaka waende mahakamani kwa hatua zaidi   jambo ambalo wakamataji hao wa mifugo walikataa. Amemtaka Rais KIKWETE afikie hatua achukue maamuzi ya kuzuia unyang’anyi wa mali za wananchi, mauaji na kila aina uvunja