Posts

Showing posts from January, 2016

MANJI ATETEWA

Ben Komba/Pwani-Tanzania/1/27/2016 3:02:11 PM Tawi la Yanga Kibaha kwa Mfipa limepinga kauli iliyotolewa na mwenyekiti wa matawi ya Yanga Tanzania MOHAMED MSUMI kuhusiana na kumpa amri Mwenyekiti wa Yanga, YUSSUPH MANJI kufuatia  hatua ya kumuachisha kazi katibu wa klabu hiyo. Mwenyekiti wa Tawi la Yanga Kibaha kwa Mfipa, MRISHO KHALFAN SWAGALA amesema kuwa Mwenyekiti wa Yanga YUSUPH MANJI yupo sawa kuhusiana na hatua hiyo na kumtaka mwenyekiti huyo matawi ya Yanga kumuomba radhi Mwenyekiti Manji ili kuleta mshikamano klabuni. SWAGALA amebainisha kuwa katiba ya Klabu ya Yanga inatambua mamlaka aliyo nayo Mwenyekiti Manji na MSUMI akiwa kama mwenyekiti wa matawi ya Yanga Tanzania atambue kuwa yeye yupo chini ya Mwenyekiti Manji na anayo mamlaka kamili ya kutoa uamuzi kuhusiana na klabu yake. END.
https//www.youtube.com/user/misugusugu