Posts

Showing posts from March, 2014

KABALUME GENERAL BUSINESS SUPPLY /KIBAHA

Image
59342vhlqw4e@youtube.com

KONGAMANO LA MAFUTA NA GESI

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/21-03-2014/11:33 Watanzania wametakiwa kutobweteka kutokana na taarifa za kugunduliwa gesi na mafuta maeneo mbalimbali ya nchini kwani rasilimali hiyo haibaki milele, na kutoa msisitizo kuendelea kufanya kazi za uzalishaji mali kwa bidii katika sekta zote ili kujenga uchumi endelevu. Katibu kiongozi Ikulu, BALOZI OMBEN SEFUE ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa kongamano la viongozi wa Mkoa wa Pwani kuhusu Rasilimali   gesi asilia, Mafuta na madini kwa amani na maendeleo ya Tanzania lililofanyika mjini Bagamoyo mkoa wa Pwani. BALOZI SEFUE amewakumbusha Watanzania kuwa Tanzania bado ni nchi maskini na tukipata tamaa kuwa tupuuzie sekta nyingine kama elimu, kilimo na harakati nyingine za kiuchumi au kila eneo ambalo linakuwa na rasilimali za gesi na mafuta kuamua kuhodhi utajiri huo nako kunaweza kuleta magawanyiko kama taifa. BALOZI SEFUE amekubaliana na dhana ya rasilimali inayopatikana eneo husika kuanza kunufaisha wakazi wa hapo lakini sio

WAPONGEZA UTEKELEZAJI ILANI.

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/15-03-2014 Jumuiya ya Wazazi wa Chama cha Mapinduzi kimeanza ziara kuzunguka kila kata kuelezea mafanikio yaliyopatikana kutokana na utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM kunakofanya na Rais DKT.JAKAYA MRISHO KIKWETE katika kipindi chake cha uongozi. Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi Kibaha vijijini, BI.SIWEMA TUWA amesema kwa upande wao kama moja ya Jumuiya ya Chama Cha Mapinduzi wamejipanga kuunga mkono juhudi zilizofanywa na Mwenyekiti wa CCM Taifa anavyotekeleza ilani ya uchaguzi wa chama hicho. BI.SIWEMA amebainisha kwa kuanzia wameanza kufanya ziara yao katika kata ya Soga ambapo wamefungua matawi mawili ya wakereketwa, Ofisi ya Chama Kata na mradi wa kuku wa kufuga. Akizungumza katika ziara hiyo, Mgeni rasmi Mwenyekiti wa CCM Kibaha vijijini, BW.HAMIS KANESA akijibu risala mbalimbali zilizosomwa kwake na Vikundi ambavyo amevikagua amesema Chama kimejipanga kusaidia wanajamii ambao wanajishughulisha na ujasiriamali. BW.KANESA ameongeza kuwa kw

RIDHIWAN ARUDISHA FOMU

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/927/13-3-215 Mjumbe wa NEC wa chama cha Mapinduzi BW.RIDHIWAN KIKWETE ambaye pia ni mgombea wa ubunge wa Jimbo la uchaguzi Chalinze kupitia tiketi ya Chama cha mapinduzi amerejesha fomu za   kuwania nafasi hiyo.   Akipokea fomu hizo Msimamizi wa uchaguzi wa Jimbo, BW.SAMWEL SALIANGA amesema mpaka sasa ofisi yake imeshapitia fomu ambazo zimerajeshwa na kujiridhisha na mchakato unavyoendelea na hivyo kutoa fursa rasmi kwa BW.KIKWETE kuanza kampeni muda wowote.   BW.SALIANGA amebainisha kuwa mpaka sasa vyama ambavyo vimeshachukua fomu kugombea nafasi iliyo wazi Ubunge wa Jimbo hilo ambayo imeachwa wazi kufuatia kufariki kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo, BW. SAID MDOGO.   Amewataja vyama vitano ambavyo tayari vimechukua fomu mbali ya CCM, ni CUF wamemsimamisha BW.ZAHOR PANDU, CHADEMA ni BW. MATHAYO TOLONGEI na NRA mgombea wao ni BW.HASSAN ALMAS.   Akizungumza mara baada ya kurudisha fomu hizo, Mgombea huyo wa CCM BW.RIDHIWAN KIKWETE a

NISHATI MBADALA

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/06-03-2014 Wananchi wilayani Kibaha wametakiwa kutumia nishati mbadala katika shughuli zao za kila siku ili kupunguza wimbi la uharibifu wa mazingira kama inavyojidhihirisha sasa. Kaimu mkuu wa wilaya ya Kibaha, BI. HADIJA MRUMA akifungua uzinduzi wa kituo hicho cha kuzalisha mkaa bila kukata miti amesema kuanzishwa kwa mradi huo wa nishati mbadala na hatua muhimu katika kupunguza ukataji wa miti holela. BI.MRUMA ameitaka jamii kuchangamkia teknolojia ya matumizi ya nishati mbadala ili kuweza kuleta mapinduzi ya misitu ambayo itasaidia kuokoa misitu yetu na uharibifu. Akiongea katika uzinduzi wa Kituo cha kuzalisha mkaa mbadala bila kukata miti  kilichopo Mlandizi Msufini, Mkurugenzi wa TaTEDO, BW. ESTOMIH SAWE amesema kuna ongezeko kubwa la matumizi ya mkaa ambalo linatishia kusababisha jangwa. BW.SAWE ameongeza kuwa kumekuwa na ongezeko kubwa la ukataji miti kutokana na Jiji la Dar es Saalam kutegemea nishati ya mkaa ambao unatoka katika mkoa wa Pwani na h

NYUKI NA FAIDA ZAKE.

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/3/7/2014/10:00:49 Watanzania wameshauriwa kufuga nyuki wadogo ili waweze kujikomboa kiuchumi kutoka na asali ya nyuki hao kuwa na faida ya kiuchumi na kiafya kwa jamii. Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la MATRIX lenye maskani yake mjini Kibaha, BW. MHEGELELE MDUDA amesema ufugaji wa nyuki hao ni muhimu kwa jamii kwani inasaidia kuongeza kipato kwa jamii na vilevile katika suala zima la uimarishaji afya. BW.MDUDA ameongeza kuwa kufuga Nyuki wadogo ni rahisi kutokana na nyuki hao kutokuwa wakali na hivyo kutoweza kudhuru watu kulinganisha na nyuki wakubwa ambao wenyewe upenda kuweka maskani yao sehemu zenye utulivu. Mkurugenzi huyo wa MATRIX, BW.MDUDA amefafanua kuwa nyuki hao ili waweze kuzalisha asali kwa wingi kinachotakiwa ni uwepo wa miti ya maua mbalimbali, kama milonge, Mastaferi na maua mbalimbali ya mwitu. AIDHA amebainisha kuwa hali ya uwepo wa maji maji nayo ni muhimu kwa uzalishaji asali wa nyuki hao wadogo ambao wanapatikana na mizinga y

BAGAMOYO YAZIZIMA

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/09:17/11-03-2014 Hoi hoi na vifijo zilianikiza mji wa Bagamoyo wakati mjumbe wa halmashauri kuu ya Taifa ya CCM, BW. RIDHIWAN KIKWETE kuchukua rasmi fomu ya kugombea nafasi ya ubunge Jimbo la uchaguzi Chalinze kupitia tiketi ya chama hicho. Akizungumza mara baada ya kupokea Fomu hiyo BW. RIDHIWAN KIKWETE ambayo imemthibitisha rasmi  kuwa yeye kuwa ndio mgombea wa nafasi hiyo kupitia Chama Cha Mapinduzi ambapo amesema lengo la kugombea nafasi hiyo ni kuliletea maendeleo Chalinze. Amebainisha kuwa amegombea nafasi hiyo ili aendeleze yale ambayo marehemu SAID BWANAMDOGO aliazimia kufanya katika jimbo hilo, nay eye kwa upande wake atatekeleza yale yote yaliyoachwa na marehemu. Zaidi shuhudia hali ilivyokuwa wakati akichukua rasmi fomu hiyo baada ya Jina lake kupitishwa na Kamati Kuu ya CCM…… END

ZAHANATI YAPANULIWA MJINI KIBAHA

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/01-3-2014:11:51 Zahanati  ya Mkoani inafanyiwa upanuzi kuwezesha kuchukua kinamama wajawazito wapatao 250 mpaka 300 kwa mwezi na ujenzi huo unatarajia kutumia shilingi Milioni 250 ikiwa ni mapato ya ndani ya halmashauri ya mji wa Kibaha. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mganga mkuu wa halmashauri ya mji wa Kibaha, BW.ISSA KANIKI amesema kuwa Zahanati ya Mkoani imekuwa na tatizo kubwa linapokuja suala la kinamama wajawazito, ambapo kwa sasa Zahanati ina vitanda  vya kujifungulia kinamama wajawazito. BW.KANIKI ameongeza ujenzi huoo utawanufaisha zaidi kinamama na watoto wachanga, Mpaka sasa mkandarasi ameshapatikana na ujenzi unatarajia kukamilika Mei 30, moja ya majengo yatakayojengwa ni holi la kupumzikia, holi la kinamama ambao wamejifungua na wanaporudi nyumbani wanapata matatizo na kulazimika kurudi hospitali. aidha amefafanua kuwa kila kitu kimekamilika na hakuna tatizo lolote na mkandarasi yupo eneo la ujenzi

WANAWAKE KIBAHA WAJIANDAA KWA SHEREHE ZAO

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/01-03-2014 Katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani, Jumuiya ya wanawake wa Chama cha Mapinduzi mjini Kibaha, wametumia nafasi hiyo kutengeneza sare ya maadhimisho hayo ikiwa ni njia ya kinamama wengine kujifunza kwa kutumia mbinu ya ujasiriamali kujikwamua kiuchumi. Kamera ya mpiga picha iliwakuta kinamama hao nyuma ya ofisi za chama hico wilaya wakitengeneza vitenge maalum kwa ajili ya siku ya kilele cha sherehe za kinamama kwa ajili ya matumizi ya kushona mashati au kama kitenge kwa kinamama. Zaidi shuhudia na kusikiliza kinamama wanazungumziaje umuhimu wa wao kujiunga na ujasiriamali……