Posts

Showing posts from May, 2015

HOTUBA YA MH.EDWARD NGOYAY LOWASSA KUTANGAZA NI YA URAIS

HOTUBA YA MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA KWENYE MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI KWA AJILI YA KUTANGAZA NIA YA KUOMBA KUTEULIWA KUWA MGOMBEA WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) KWA NAFASI YA URAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA UTANGULIZI: Ndugu zangu wana-CCM na Watanzania wenzangu, Hii ni siku muhimu kwangu na kwa nchi yetu. Leo nimeamua kuwaita ili kuwatangazia rasmi Watanzania wenzangu azma yangu ya kutaka kuomba ridhaa ya chama chetu, Chama Cha Mapinduzi (CCM), niweze kuteuliwa kuwa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nasema hii ni siku muhimu kwangu kwa sababu naamini historia yangu itainakili kama ni siku ambayo kwa mara ya pili katika maisha yangu nimejitokeza kuwania kuiongoza nchi yetu kupitia chama chetu. Mara ya kwanza ilikuwa ni mwaka 1995 wakati wa uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi hapa nchini nilipojitokeza nikiwa pamoja na Rais Jakaya Kikwete; wakati ule sote tulikuwa wanasiasa vijana. Tulikwenda pamoja kuchukua fomu ndani ya Chama na baadaye tukafanya maz

VIDEO-WAHITIMU 15 MWAKA 2012 CHUO CHA UUGUZI SHIRIKA LA ELIMU WALILIA VYETI VYAO

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/5/30/2015 10:18 AM Wanafunzi 15 wa fani ya uuguzi waliomaliza mafunzo yao mwaka 2012  katika chuo cha uuguzi shirika la elimu Kibaha mpaka sasa hawajapatiwa vyeti vyao vya kuwahalalisha kufanya kazi hiyo na kuweza kutoa huduma kwa jamii. Akizungumza na mwandishi wa Habari hizi katika siku ya kuadhimisha sherehe ya wauuguzi Ulimwenguni, Muuguzi BW.IBRAHIM MSAFIR amesema kuwa wanaguswa sana kwa wenzao kuhitimu masomo ya uuguzi na baadaye kutopewa vyeti. BW.MSAFIR amebainisha kuwa kila baada ya muda Fulani wizara ya afya inakagua vyuo vyote vinavyotoa mafunzo ya afya na kuvitambua ambavyo vitakidhi matakwa ya Wizara, ingawa kwa sasa Chuo chao kinatambulika na kulitaka Shirika la Elimu kukaa kwa pamoja na wizara ya afya kuangalia uwezekano wa kuwasaidia wauguzi wenzao. Naye muuguzi mkuu, BI.ELIZABETH MLACHA amesema FLORENCE NIGHTANGELE ambaye amezaliwa 12 Mei 1928 na kuamua kujiunga na kazi ya uuguzi ambayo ilikuwa kinyume na matakwa ya wazazi w

WAHITIMU WAUGUZI 15 WALIOMALIZA MAFUNZO 2012 WA UUGUZI COTC WALILIA

Ben Komba/Pwani-Tanzania/5/30/2015 10:18 AM Wanafunzi 15 wa fani ya uuguzi waliomaliza mafunzo yao mwaka 2012  katika chuo cha uuguzi shirika la elimu Kibaha mpaka sasa hawajapatiwa vyeti vyao vya kuwahalalisha kufanya kazi hiyo na kuweza kutoa huduma kwa jamii. Akizungumza na mwandishi wa Habari hizi katika siku ya kuadhimisha sherehe ya wauuguzi Ulimwenguni, Muuguzi BW.IBRAHIM MSAFIR amesema kuwa wanaguswa sana kwa wenzao kuhitimu masomo ya uuguzi na baadaye kutopewa vyeti. BW.MSAFIR amebainisha kuwa kila baada ya muda Fulani wizara ya afya inakagua vyuo vyote vinavyotoa mafunzo ya afya na kuvitambua ambavyo vitakidhi matakwa ya Wizara, ingawa kwa sasa Chuo chao kinatambulika na kulitaka Shirika la Elimu kukaa kwa pamoja na wizara ya afya kuangalia uwezekano wa kuwasaidia wauguzi wenzao. Naye muuguzi mkuu, BI.ELIZABETH MLACHA amesema FLORENCE NIGHTANGELE ambaye amezaliwa 12 Mei 1928 na kuamua kujiunga na kazi ya uuguzi ambayo ilikuwa kinyume na matakwa ya wazazi wake.

VIASHIRIA VYA VURUGU VYAANZA KUJITOKEZA- KIDEO.

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/5/25/2015 2:48:06 PM Viashiria ya kuwepo kwa vurugu katika uchaguzi mkuu ujao imeanza kujitokeza rasmi na hali ikiwa ya wasiwasi kutokana na baadhi ya wanaowania nafasi mbalimbali za uwakilishi wakiandaa vikundi vya vijana wahuni kwa ajili ya kuwatumia kipindi cha uchaguzi mkuu ujao wa Rais, Madiwani na wabunge unaotarajiwa kufanyika hapo Oktoba 25 mwaka huu. Hivi karibuni katika Mkutano wa hadhara ambao umefanywa na Mbunge wa Kibaha mjini,MH. SILVESTRY KOKA na kutokea kwa vurugu ambazo zimesababisha mtu mmoja kujeruhiwa kutokana na kupita na bango ambalo liliwakera wana CCM. Hali hiyo ambayo iliotewa toka mapema kabla ya mkutano, Baada ya Katibu wa Mbunge huyo, BW.METHOD MSEMBERE kumwambia mwandishi wa Habari hizi kuwa kuna kikundi cha vijana ambacho kimepanga kufanya vurugu katika mkutano mkuu wa mheshimiwa mbunge. BW.MSEMBERE ameongeza kuwa kuna watu wanataka kufanya fujo katika mkutano huo na kutuhumu moja ya kambi zilizo ndani ya chama hi

HATIMAYE VIDEO YA TASAF KUTUMIA SHILINGI BILIONI 1.6 KIBAHA HII HAPA

  Ben Komba/Pwani-Tanzania/5/22/2015 10:48:18 AM Zaidi  ya shilingi Bilioni 1,657102301/= zimetumika na TASAF halmashauri ya wilaya ya Kibaha na kupata mafanikio makubwa katika kuhakikisha jamii maskini zinapata mahitaji stahili ili kujenga jamii ambayo itakuwa na uwezo wa kujikimu na maisha yenye kukabiliwa na changamoto mbalimbali za kiuchumi. Mratibu wa TASAF halmashauri ya wilaya ya Kibaha, BW.GODSON HARRY amesema hayo ofisini kwake akizungumza na mwandishi wa Habari hizi, ambapo amesema kuwa mpaka sasa kwa upande wa zoezi la uhawilishaji fedha kaya zaidi ya 5000 zimefaidika na mpango huo. BW.HARRY ameongeza kupitia mpango huo wamefanikiwa kuwatambua na kuwaandikisha walengwa watakaohusika mpango huo wa uhawilishaji wa Fedha kwa kaya maskini, wenye lengo la kuinua uchumi wa jamii maskini zaidi. Amebainisha toka kuanzishwa kwa mpango mafanikio mbalimbali yamepatikana ikiwa pamoja na ongezeko la uandikishaji wa watoto mashuleni kutoka katika kaya lengwa ikiwa pamoj

MANIPULATION OF POWER aka ULAFI WA MADARAKA.

▼👇👇 😕😕Friday, May 22, 2015 HABARI KUBWA LEO-VITA MPYAA YAIBUKA,TV ,REDIO NA SERIKALI,DK MENGI ASEMA TBC HAPANA,SOMA HAPA KUJUA pichani ni Rais Jakaya kikwete picha na Maktaba SERIKALI ya Chama cha Mapinduzi CCM ni kama imeiingia kwenye Ugomvi  mkubwa na Vyombo Vya Habari Binafsi ikiwemo Redio na TV baada Serikali hiyo  kukaribia kupitisha sheria Mbaya  zaidi kuwaitokea nchini hususani  kwenye Sekta ya  Vyombo vya Habari tangu nchini kupata Uhuru.Mtandao huu umeelezwa .Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.       Sheria hiyo ambayo imesukwa kwa ustadi mkubwa kwa shinikizo la Waziri Mmoja Mwandamizi wa  Serikali ya Kikwete  ni ile inayosema kwamba Vyombo vya Habari Binafsi ikiwemo TV na Redio ifikiapo saa 2 usiku ni lazima wajiunge moja kwa moja na Taarifa za Habari zitakazokuwa zinarushwa na TBC 1 kwa upande wa TV na Tbc Taifa kwa upande wa Redio.        Sheria hiyo ambayo teyari ipo mikononi mwa Bunge inatarajiwa kupitishwa haraka sana kabla ya uchaguzi mkuu unaofanyika ha

TASAF YATUMIA BILIONI.1.6 WILAYANI KIBAHA

Ben Komba/Pwani-Tanzania/5/22/2015 10:48:18 AM Zaidi  ya shilingi Bilioni 1,657102301/= zimetumika na TASAF halmashauri ya wilaya ya Kibaha na kupata mafanikio makubwa katika kuhakikisha jamii maskini zinapata mahitaji stahili ili kujenga jamii ambayo itakuwa na uwezo wa kujikimu na maisha yenye kukabiliwa na changamoto mbalimbali za kiuchumi. Mratibu wa TASAF halmashauri ya wilaya ya Kibaha, BW.GODSON HARRY amesema hayo ofisini kwake akizungumza na mwandishi wa Habari hizi, ambapo amesema kuwa mpaka sasa kwa upande wa zoezi la uhawilishaji fedha kaya zaidi ya 5000 zimefaidika na mpango huo. BW.HARRY ameongeza kupitia mpango huo wamefanikiwa kuwatambua na kuwaandikisha walengwa watakaohusika mpango huo wa uhawilishaji wa Fedha kwa kaya maskini, wenye lengo la kuinua uchumi wa jamii maskini zaidi. Amebainisha toka kuanzishwa kwa mpango mafanikio mbalimbali yamepatikana ikiwa pamoja na ongezeko la uandikishaji wa watoto mashuleni kutoka katika kaya lengwa ikiwa pamoja na

VIDEO-VURUGU ZAZUKA MKUTANO WA MBUNGE KIBAHA MJINI.

Image
Ben Komba/Pwani-Kibaha/5/18/2015 2:40:05 PM Mkutano wa hadhara ambao umefanywa na Mbunge wa Kibaha mjini,MH. SILVESTRY KOKA kutokea kwa vurugu ambazo zimesababisha mtu mmoja kujeruhiwa kutokana na kupita na bango ambalo liliwakera wana CCM. Hali hiyo ambayo iliotewa toka mapema kabla ya mkutano, Baada ya Katibu wa Mbunge huyo, BW.METHOD MSEMBERE kumnwambia mwandishi wa Habari hizi kuwa kuna kikundi cha vijana ambacho kimepanga kufanya vurugu katika mkutano mkuu wa mheshimiwa mbunge. BW.MSEMBERE ameongeza kuwa kuna watu wanataka kufanya fujo katika mkutano huo na kutuhumu moja ya kambi zilizo ndani ya chama hicho ambazo zinawania nafasi ya Bunge. Na kweli ilipofika muda wa mkutano baada ya MH.KOKA kumaliza kufungua mashina ya CCM na kurudi kwa ajili ya mkutano ndipo vijana kadhaa wa CHADEMA  walipojitokeza na mabango ambapo moja ya bango hilo ambalo lilisema TUNASHUKURU MBUNGE WETU KWA KUJA KUTUAGA, BYEBYE, na ndipo mmoja wa viongozi wa CCM wilaya akachukuwa mabango

VIDEO-WAZEE WAPAATIWA VITAMBULISHO VYA KUPATIWA TIBA BURE.

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/5/14/2015 11:20:28 AM Jimbo la uchaguzi Sumbawanga mjini linatarajiwa kuwaka moto katika uchaguzi mkuu ujao baada ya watia nia mbalimbali kujitokeza kutaka mkupata nafasi ya uwakilishi wa Jimbo hilo ambalo kwa sasa linashikiliwa na Mheshimiwa AESHI MOHAMED kwa tikiti ya CCM. Mmoja wa waliojitokeza kutia nia kutaka nafasi ya uwakilishi Bungeni ni Mtumishi wa Idara ya ardhi halmashauri ya wilaya ya Kibaha, BW.FRANK MWALEMBE ambaye yeye ni mzaliwa wa manispaa ya mji wa Sumbawanga. BW.MWALEMBE kabla ya kujiunga na halmashauri ya mji wa Kibaha kama mtumishi, Alipata elimu yake katika shule ya msingi Malagano, elimu ya sekondari ya Seminari ya Kahengesa na “A level” Katika shule ya Pugu High School na baadaye alifanya kazi ya Ualimu katika shule ya sekondari ya Makuzani na Rukwa high school kwa muda wa mwaka mmoja na nusu kama Mwalimu wa nidhamu. Na ilipofika mwaka 2005-2006, BW.FRANK MWALEMBE alijiunga na chuo kikuu cha ardhi cha Dar es Saalam na

TIBA YA BURE KWA WAZEE YAZINDULIWA KIBAHA.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/5/13/2015 10:01:45 AM Mpango wa Tiba bure kwa wazee wa umri wa miaka 60 na kuendelea umeziinduliwa mjini Kibaha kwa wazee 4672 kupatiwa vitambulisho vya kuwawezesha kupatiwa tiba bure inapotokea kuwa wameugua. Mganga wa mkuu wa halmashauri ya mji wa Kibaha, DKT.ISSA KANIKI akisoma taarifa maalum kwa Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya mji wa Kibaha kwa niaba ya Mkuu wa wilaya ya Kibaha, BI.JENIFA CHRISTIAN amesema halmashauri ya mji wa Kibaha katika kutekeleza sera ya Taifa ya wazee, imeamua kuweka suala hilo kwa vitendo. DKT.KANIKI amebainisha kuwa ambapo halmashauri ilianza kwa kufanya tathimini ya utekelezaji wa sera hiyo,kwa kufanya uhamasishaji katika ngazi ya jamii na kutoa elimu ya ufahamu juu ya uwepo wa mpango huo, Kwa kutumia takwimu ya sensa ya wakazi katika halmashauri ya Mji wa Kibaha aambapo inakadiriwa kuwa na wazee 5,111. Ameongeza DKT.KANIKI kuwa Jumla ya fedha zilizotumika kutengeneza vitambulisho hivyo 4672 ni shilling mil

AJITOKEZA KUTIA NIA UBUNGE SUMBAWANGA MJINI.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/5/14/2015 11:20:28 AM Jimbo la uchaguzi Sumbawanga mjini linatarajiwa kuwaka moto katika uchaguzi mkuu ujao baada ya watia nia mbalimbali kujitokeza kutaka mkupata nafasi ya uwakilishi wa Jimbo hilo ambalo kwa sasa linashikiliwa na Mheshimiwa AESHI MOHAMED kwa tikiti ya CCM. Mmoja wa waliojitokeza kutia nia kutaka nafasi ya uwakilishi Bungeni ni Mtumishi wa Idara ya ardhi halmashauri ya wilaya ya Kibaha, BW.FRANK MWALEMBE ambaye yeye ni mzaliwa wa manispaa ya mji wa Sumbawanga. BW.MWALEMBE kabla ya kujiunga na halmashauri ya mji wa Kibaha kama mtumishi, Alipata elimu yake katika shule ya msingi Malagano, elimu ya sekondari ya Seminari ya Kahengesa na “A level” Katika shule ya Pugu High School na baadaye alifanya kazi ya Ualimu katika shule ya sekondari ya Makuzani na Rukwa high school kwa muda wa mwaka mmoja na nusu kama Mwalimu wa nidhamu. Na ilipofika mwaka 2005-2006, BW.FRANK MWALEMBE alijiunga na chuo kikuu cha ardhi cha Dar es Saalam na k

VIDEO-MCHANGE ATEMA CHECHE DHIDI YA MADAI DHIDI YAKE KUHUSU RUSHWA.

Image