Posts

Showing posts from July, 2014

WALAMIKIA MALIPO KIDUCHU HALMASHAURI YA MJI WA KIBAHA

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/7/28/2014 6:16:35 PM Watumishi wa kitengo cha mazingira halmashauri ya mji wa Kibaha wameendelea kulazimika kufanya kazi kwa kima cha mshahara wanacholalamikia ambacho wao hawakubaliani nao. Mwandishi wa habari hizi amewashuhudia watumishi hao wakifanya kazi hiyo jana ikiwa ni sehemu ya wajibu wao kuhakikisha kuwa nji wa Kibaha unakuwa safi muda wote sambamba na uwepo wa gari la kisasa la taka. Nimebahatika kuongea na watumishi hao wa mazingira ambao walikuwa na mambo kadhaa ya kuelezea, Mmoja wa BW.KASSIM MALIVI amesema wao wanalipwa shilingi 125,000/- kiwango ambacho hakitoshelezi mahitaji na kulinganisha na uzito wa kazi wanayofanya. BW.MALIVI   ameongeza wamepeleka malalamiko yao sehemu mbalimbali wakitaka kuboreshewa maslahi yao, Hatua ambyo iliwafikisha hadi ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Kibaha BI.HALIMA KIHEMBA ambaye aliaahidi kulishughulikia suala hilo kwa karibu. Naye mtumishi mwingine BW.JUMANNE KADALA amesema kuwa yeye anaipen

SHIRIKA LA ELIMU LAKABILIWA NA UKATA.

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/26-07-2014 Shirika la elimu Kibaha lipo katika changamoto kubwa ya kukabiliana na mahitaji ya hospitali iliyo chini yake kutokana na kukosekana kwa rasilimali fedha za kutosha kuweza kuwalipa wauuguzi stahili zao kama sheria za kazi zinavyoelekeza. Mkurugenzi wa Shirika la elimu Kibaha BW.CYPRIAN MPEMBA ameyazungumza hayo wakati wa maadhimisho ya siku ya wauguzi hospitalini hapo, amesema yeye kwa upande wake hana mtima nyongo na mtumishi yoyote linapokuja suala la maslahi yao. BW.MPEMBA amewahakikishia wauguzi kuwa waandike mapendekezo yao na kuyafikisha ofisini kwake ili kuweza kuyapitia na kuyafanyia kazi na hasa ikizingatiwa kuwa wauuguzi wanakabiliwa na changamoto kubwa kutokana na kuwa wachache kufuatia kustaafu kwa waliotangulia. Mkurugenzi huyo wa Shirika la elimu Kibaha BW.MPEMBA ameongeza kuwa hauwezi kuzungumzia maendeleo iwapo viashiria vya afya vina tatiza, na kwa uwepo wa wauguzi kunasaidia kuharakisha maendeleo kutokana na afya ya wananchi kuim

KAMISHNA MUSSA AKAGUA MIRADI POLISI JAMII PWANI

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/24-07-2014 Kamishna MUSSA ALI MUSSA wa Kamisheni ya Polisi jamii amehitimisha ziara kuzunguka mikoa 20 ya Tanzania katika mkoa wa Pwani kwa kukagua miradi ya Polisi jamii inayoendeshwa nchi nzima. Kamishna MUSSA katika ziara yake mkoani hapa, ameweza kukagua masuala ya usafiri salama wa bodaboda, mradi wa usalama wetu kwanza katika shule ya Msingi Miembesaba na kukagua gwaride la vikundi vya ulinzi shirikishi ya mjini Kibaha. Akizungumza katika ziara yake katika mkoa wa Pwani, Kamishna MUSSA ALLY MUSSA amewataka wananchi kujua tofauti ya Polisi jamii na Vikundi vya ulinzi shirikishi jamii ili kuweza kupata tafsiri sahihi ya mradi huo. KAMISHNA MUSSA amesema kuwa jamii imekuwa ikiamini vikundi vyua ulinzi shirikishi ndio Polisi jamii, jambo ambalo ni kinyume na falsafa ya uanzishwaji wa Polisi jamii, na akawaeleza wananchi maana halisi ya ulinzi shirikishi ni kwa kila mmoja wetu awe mwanamke au mwanaume, mzee au kijana na hata mto

MWENGE WA UHURU WAINGIA PWANI.

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/222-07-2014/10:20 Mbio za Mwenge uhuru umeingia katika Mkoa wa Pwani ukitokea mkoani Lindi ambako umemaliza mzunguko wake kwa kukagua, kuweka mawe ya msingi na kufungua miradi mbalimbali ya maendeleo. Mwenge huo ulikabidhiwa kwa Kaimu Katibu tawala,BI.SIMFROZA MMARI kutoka kwa Afisa Tawala wa Mkoa wa Lindi BW.ABDALLAH CHIKOTA, katika kijiji cha Kiwanga wilaya ya Rufiji mpakani mwa Mkoa wa Pwani na Lindi. Akiongea mara baada ya kupokelewa kwa Mwenge huo,Kaimu mkuu wa Mkoa wa Pwani, BI.HALIMA KIHEMBA amesema kuwa Katika mkoa wa Pwani mwenge unatarajiwa kufungua, kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi inayokadiriwa kufikia bilioni 15 na kati ya miradi hiyo wilaya ya Rufiji pekee ina miradi inayogharimu bilioni 5. Akizungumza katika sherehe hiyo ya makabidhiano ya Mwenge wa uhuru, Kiongozi wa mbio hizo kitaifa, BI RACHEL KASSANDA alitumia nafasi hiyo kukemea vitendo vya mauaji ya wanawake yanayoendelea katika wilaya ya Nachingwea.

WENYE MABUCHA WAGOMA KUUZA NYAMA MJINI KIBAHA VIDEO

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/19-07/2014 Wafanyabiashara wa mabucha mjini Kibaha wamegoma kufanya shughuli hiyo kufuatia halmashauri ya mji wa Kibaha kuwahamisha kutoka machinjio ya awali na kuwapeleka katika machinjio mpya ambayo hawakuridhika nayo kutokana na kukosekana kwa miundombinu ya kutosha. Msemaji wa wafanyabiashara aliyejitambulisha kwa jina la BW.ATHUMAN MKANGA amesema wao wameamuamua kuchukua uamuzi huo kufuatia halmashauri kutoa tamko la lazima ambalo linawataka wao kuhamia eneo hilo na hawatarusiwas tena kuchinja katika machinjio hayo ya zamani. Msemaji huyo amesema kuwa wao hawakatai kuhamia katika machinjio hiyo inayoitwa ya kisasa kwa sababu miundombinu yake bado haijakamilika na hata mvua ikinyesha ina uwezekano mkubwa kulowesha nyama na hivyo kupoteza Thamani halisi. Aidha BW.MKANGA amebainisha kuna tatizo kubwa la maji ikiwa pamoja na kukosekana kwa umeme wa uhakika, na hivyo kuweza kusababisha nyama zao kuharibika na ng'ombe kuweza kutorokea porini k

WLAC YANOA WATENDAJI-video

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/15-07-2-14 Shirika lisilo la kiserikali linasaidia utetezi wa kisheria kwa wanawake na watoto nchini -WLAC- limetoa mafunzo maalum kwa watendaji wa mahaka, Polisi na Kata katika kuhakikisha wanapanua wigo wa wadau ambao inashirikiana nao katika kuhakikisha malengo yanafikiwa. Mwezeshaji BI.JANE MAGIGITA  shirika hilo limeona vyema kufanya kazi kwa karibu kati yake na watendaji hao muhimu ili kuweza kubadilishana uzoefu na uboreshaji wa utoaji huduma wa kisheria kwa makundi maalum katika jamii yaani wanawake na watoto. BI.MAGIGITA amefafanua kuwa wanawake na watoto wamekuwa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali katika maisha yao ya kila siku, ikiwa pamoja na kudhalilishwa kijinsia, uonevu na kudhaurauliwa katika jamii, hivi kuna ila sababu kwa makundi hayo kupatiwa misaada inayohitajika ya kisheria. Ambapo ameongeza wanawake ndio kundi kubwa linaloishi katika lindi la umaskini mkubwa kutokana na kutopatiwa fursa mbalimbali za kijamii, ikiwa pamoja n

WATENDAJI WANOLEWA KIBAHA

Ben Komba/Pwani-Tanzania/15-07-2-14 Shirika lisilo la kiserikali linasaidia utetezi wa kisheria kwa wanawake na watoto nchini -WLAC- limetoa mafunzo maalum kwa watendaji wa mahaka, Polisi na Kata katika kuhakikisha wanapanua wigo wa wadau ambao inashirikiana nao katika kuhakikisha malengo yanafikiwa. Mwezeshaji BI.JANE MAGIGITA  shirika hilo limeona vyema kufanya kazi kwa karibu kati yake na watendaji hao muhimu ili kuweza kubadilishana uzoefu na uboreshaji wa utoaji huduma wa kisheria kwa makundi maalum katika jamii yaani wanawake na watoto. BI.MAGIGITA amefafanua kuwa wanawake na watoto wamekuwa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali katika maisha yao ya kila siku, ikiwa pamoja na kudhalilishwa kijinsia, uonevu na kudhaurauliwa katika jamii, hivi kuna ila sababu kwa makundi hayo kupatiwa misaada inayohitajika ya kisheria. Ambapo ameongeza wanawake ndio kundi kubwa linaloishi katika lindi la umaskini mkubwa kutokana na kutopatiwa fursa mbalimbali za kijamii, ikiwa pamoja na mtoto wa k

LIGI YA DARAJA LA NNE KUANZA KIBAHA.

Ben Komba-Pwani-tanzania-10/07/2014 Ligi daraja la nne wilaya ya Kibaha inatarajiwa kuanza mara baada ya kukamilika mwezi mtukufu wa Ramadhani, kama kalenda ya michezo ya chama hicho inavyoonyesha. Mwandishi wa habari hizi akiongea na Katibu wa chama cha soka wilayani Kibaha, SEIF KIDODO amesema fomu kwa ajili ya kujiandikisha kushiriki ligi hiyo ya daraja la nne zimeshaanza kutolewa kwa timu ambazo zina lengo la kushiriki ligi hiyo. KIDODO ameongeza kuwa kila timu italazimika kulipa kiasi cha shilingi 30,000 ikiwa ni ada ya kiingilio ambayo itatumika katika masuala mbalimbali ya uendeshaji wa ligi hiyo. Zaidi Katibu wa KIBAFA anaongeza kuwa mwisho wa zoezi hilo ni tarehe 22 Julai mwaka huu. END