WALALAMIKA WATENDAJI KUWAIBIA


Ben Komba-Pwani-Tanzania-06/06/2016 10:10:11

Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo imetakiwa kuwasiliana na Ofisi ya mtendaji wa Kata inapotokea Mtendaji wa Kijiji ameamua kuhama kituo cha kazi kwa sababu mbalimbali.

Akizungumza katika kikao maalum cha Kijiji cha Kitonga kilichopo katika mji mdogo wa Chalinze, Afisa mtendaji wa Kata ya Vigwaza BW. MASKUZI MASKUZI ambapo amesema kuwa baadhi ya watendaji wanaohamishwa bila kuwasiliana naye wamekuwa wanaacha athari kubwa kwa vijiji walivyotoka.

BW.MASKUZI ameongeza halmashauri kwa kutomshirikisha katika suala uhamisho wa watendaji wa vijiji inasababisha kuwepo kwa migogoro isiyo na lazima ambayo inazorotesha maendeleo ya vijiji kwa kuacha makovu ambayo jamii inakuwa vigumu kuyasahau.

Mmoja wa wananchi KOMREDI NDALO amebainisha kuwa wananchi wanashindwa kuelewa kutokana na kuhama kiholela kwa watendaji wa kijiji ilihali wakiwa katika kipindi chao chote hawajawahi kusoma taarifa ya mapato na matumizi na ukiukaji wa taratibu za utumishi wa umma.


END

Comments

Popular posts from this blog

MAFUNZO YA UREFA

MAMLAK YA MJI MDOGO MLANDIZI HOI.