Ben Komba/Pwani-Tanzania/23-07-2013/10:03 Chama cha marefa wilayani Kibaha kinaendesha program maalum ya mafunzo kwa marefa wapya wenye kutaka kujiendeleza kuwa waamuzi katika ngazi mbalimbali za ligi za mchezo huo. Katibu wa Chama cha marefa wilayani Kibaha ambaye pia ndio refa bora wa ligi ya VODACOM msimu uliopita BW.SIMON MBELWA amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwezesha kuzalisha marefa wapya. BW.MBELWA amefafanua kuwa katika mambo ambayo yatazingatiwa katika mafunzo hayo ni ufundishaji wa sheria 17 za soka ambazo kila mwamuzi anapaswa kuzifahamu kwa ufasaha ili kuepusha malalamiko na wakati mwingine hata vurugu katika mchezo huo. Naye mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo, BW. GEORGE amesema kwa kupatiwa mafunzo hayo kutawasaidia kufanya maamuzi yaliyo sahihi wakati wakichezesha mechi za michuano mbalimbali. END.
Ben Komba/Pwani-Tanzania/ Wananchi katika mamlaka ya mji mdogo wa Mlandizi wamelalamika hatua ya uanzishaji wa mji huo na kuutelekeza bila kuiwezesha kifedha hali inayoathiri utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya kila siku. Nikiongea na mmoja wa wajumbe wa baraza la mamlaka ya mji mdogo wa Mlandizi ambaye alikataa jina lake kutajwa , amebaiinisha kuwa kumekuwepo na changamoto mbalimbali zinazoikabili mamlaka ya mji mdogo wa Mlandizi. Mjumbe huyo amesema kutokana na kukosekana kwa fedha kutoka halmashauri kunakosabishwa na baadhi ya watendaji ya halmashauri kuchelea wao kupunguza fedha za uendeshaji wa halmashauri kutokana na kutojiamini. Mjube huyo amebainisha kutokuwepo kwa vikao vya kisheria vya kila mwaka vinavyofanywa na baraza la mamlaka ya mji mdogo wa Mlandizi kwa madai ya kukosekana kwa fedha na kuhoji serikali inawezaje kupanga mipango ambayo haiwezi kuitekeleza. Naye Mwenyekiti wa mamalaka ya mji mdogo wa Mlandizi, BW. ABDALLAH KIDO amesema ni...
Ben Komba/Pwani-Tanzania/01/01/2013/15:03:22 Kampuni iliyopewa zabuni ya kujenga matanki ya maji katika kijiji cha Milo kata ya Vigwaza wilayani Bagamoyo imewatelekeza wafanyakazi wake wake bila kuwapatia stahili zao na kuwafanya kuishi katika maisha ya mashaka hali ambayo inatishia ubora wa kazi wanayofanya. Mwandishi wa habari hizi akizungumza na wafanyakazi wa mzabuni huyo ambaye amepewa kazi ya kujenga matanki katika kijiji hicho, kupitia mradi wa maji unaofadhiliwa na Benki ya Dunia wenye lengo la kusambaza maji maeneo ya vijijini ambapo kupitia fedha idara za maji za halmashauri wanasimamia utafutaji wa vyanzo vipya na maji na kusambaza.. Mwandishi ameshuhudia ujenzi wa kusuasua wa matenki makubwa ya kuhifadhia maji katika kijiji cha Milo, hali inayosababishwa na mkandarasi kutokuwa makini katika utekelezaji wa shughuli hiyo ambayo imenuia kumaliza tatizo la maji katika kijiji hicho kilichopo umbali wa kilometa 25 kutoka barabara ya Morogoro. Mmoja wa wafanyakazi wa kampu...
Comments
Post a Comment