Ben Komba/Pwani-Tanzania/10-Feb-13/13:42:54
Chama cha demokrasia na maendeleo kimewataka wananchi kutokubali kurubuniwa kwa kuwaambia CHADEMA ni chama cha kidini kunakosababishwa kwa baadhi ya vyama kutumia propaganda hiyo kutaka kuwagawa watanzania na baadaye kuwatawala kwa kufuata mifumo ya kurithishana kama inavyojidhihirisha hivi sasa.
Akiongea katika mkutano wa vuguvugu la mabadiliko inayoendelea nchi hivi sasakatika viwanja vya stendi ya Mzenga katika mamlaka ya mji mdogo wa Mlandizi yenye kulenga kutekeleza kauli ya mwaka wa nguvu ya umma inayoeendeshwa na chama cha demokrasia na kufanikiwa kuleta mitazamo chanya kwa wakazi wa wilaya ya Kibaha kutokana na kuwepo piga nikupige ya mikutano kati ya chama cha CHADEMA na CCM.
Kada wa chama cha demokrasia na maendeleo kutoka Arusha, BW.ALLY BANANGA amesema cha cha CCM kimekuwa chama cha kurithisha uongozi na kuyatupa kando malengo ya awali ya uanzishaji wa chama hicho ambayo yalikuwa hayana lengo la kujenga himaya za kisultani kwa baadhi ya viongozi na familia zao kama ilivyo hivi sasa kwa kuzusha mambo ambayo hayana ukweli wowote katika kujaribu kuwagawa watanzania kiimani.
BW. BANANGA amebainisha kumekuwepo na harakati kubwa katika kuhakikisha wanafanikiwa kukamata dola mwaka 2015 na kuwaasa wana Kibaha ambo wamechoka kunyanyaswa na kukandamizwa na chama tawala kuunga mkono harakati hizo za CHADEMA zenye lengo la kumkomboa mtanzania na mgogoro mkubwa wa kimfumo tunaokabiliana nao kutokana na baadhi ya watu kujiona kama wana hati miliki na Taifa hili.
INSERT ALLY BANANGA
IN:00:00
OUT:05:52
END.
ADHA YA MAJI BAGAMOYO.
ADHA YA MAJI KIJIJI CHA GONGO KATA YA MKANGE JIMBO LA CHALINZE WILAYA YA BAGAMOYO PWANI Na John Gagarini, Mkange WANANCHI wa Kijiji cha Gongo kata ya Mkange wilayani Bagamoyo wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji ambapo huweka foleni ya kuchota maji kwenye kisima kilichopo kijijini hapo baada ya wiki mbili. Kutokana na usosefu huo wa maji wananchi hao wamekuwa wakinunua maji ya bomba ndoo ya lita 20 kati ya shilingi 1,000 na shilingi 1,500 maji ambayo huuzwa kwenye magari au pikipiki hivyo kuwafanya wajikute hawapati maendeleo kutokana na gharama kubwa kuzitumia kununulia maji. Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mkutano wa kampeni wa mgombea Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ridhiwani Kikwete, kwenye kata ya Mkange mwananchi wa Kijiji hicho Hungilo Nyoka alisema kuwa maji yamewafanya washindwe kupata maendeleo. Nyoka alisema kila kaya inatakiwa ichote madumu manne ili angalau kila mmoja apate baada ya hapo maji hukatika ambapo in...
Comments
Post a Comment