Ben Komba/Pwani=Tanzania/11:56 Umoja wa Wafanyabiashara wa nyumba za kulala wageni na mahoteli UGEHOKI mjini Kibaha wameilalamikia halmashauri ya mji wa Kibaha kwa kuendelea kutoza kodi ambayo imefutwa kisheria. Katibu wa UGEHOKI, BW.RICHARD NGELEJA amesema hayo katika mkutano wa wanachama wa umoja huo uliofanyika katika ukumbi wa COUNTRYSIDE,Ambapo amenukuu majadliano ya kikao cha nane cha bunge cha tarehe 22 juni 2012. BW.NGELEJA amebainisha kuwa katika kikao hicho cha bunge ambacho kilijadili kuhusu ushuru wa hotel levy ipunguzwe kutoka 20% hadi 18% au 16%,na serikali inakamilisha zoezi lakuhuisha sheria ya utalii ya mwaka 2008 iliyoanza kutumika mwezi Julai,2009. Naye Mwenyekiti wa UGEHOKI, BW.FABIAN MAJAGA amebainisha kuwa wao wana vielelezo vyote vinavyoonyesha kufutwa kwa ushuru huo wa nyumba za wageni na mahoteli ikiwa pamoja hansard ya Bunge ambayo inaeleza wazi kufutwa kwa ushuru huo. BW.MAJAGA ameongeza kuwa hatua mbali mbali wamechukua ikiwa ...
Comments
Post a Comment