Ben Komba/Pwani-Tanzania/3/24/2012 5:05:02 PM
Chama cha waandishi wa habari wa mazingira na za watu wenye ulemavu Mkoani Pwani, (PEDWA) wamekutana leo kwa mara ya kwanza katika kupanga mkakati wa kuanza baadhi ya shughuli zake kwa kutumia nguvu zake yenyewe ili kuonyesha umuhimu wa masuala ya mazingira na ya watu wenye ulemavu katika jamii.
Katika kikao cha pamoja na baadhi ya wadau wa masuala hayo, Mwenyekiti wa PEDWA- PWANI ENVIROMENTAL AND DISABLED WRITERS ASSOCIATION, BW. BERNARD KOMBA amesema lengo la kuanzishwa kwa asasi hiyo isiyo tengeneza faida, ni kuielimisha jamii juu ya umuhimu wa utunzaji wa mazingira na kuthamini watu wenye ulemavu.
BW. KOMBA amebainisha kuwa jamii bado inafanya dhihaka juu ya masuala hayo ambayo kuyatekeleza ni sawa na kutekeleza hqaki za msingi za binadamu, hasa ikizingatiwa binadamu wana haki ya kuishi katika mazingira yatakayomwezesha kufanya shughuli zake bila kusumbuliwa na majanga ya asili yanayosababishwa na ukataji misitu holela.
Aidha kwa upande wa walemavu kutekeleza haki zao ni kutekeleza haki za msingi za binadamu kwani nao wanastahili kuthaminiwa na kupatiwa huduma wanazostahili katika kuboresha maisha yao ya kila siku, hivyo ni juu ya serikali na jamii kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapatiwa haki zao.
Mmoja wa wadau ambaye amehudhurio kikao hicho cha utambulisho kutoka kampuni ya mafuta ya KOBIL ya Chalinze wilayani Bagamoyo, BW. RAJAB VARISANGA akizungumzia juu ya suala la mazingira, amewashauri watanzania wabadilike na kuanza kutumia gesi hasa kutokana nishati hiyo kuwa nafuu kulinganisha na mkaa, mtumiaji akielimishwa juu matumizi sahihi ya gesi.
BW. VARISANGA amebainisha katika utafiti alioufanya amegundua ukiwa na mtungi wa gesi wa shilingi elfu 28, unaweza kutumia kwa kipindi cha miezi mitatu, ambapo katika kipindi hicho kuna uwezekano mkubwa wa kutumia gunia 6 zenye thamani ya shilingi elfu 90, ambapo ametaka chama hicho kusaidia kutoa elimu hiyo kwa wananchi ili kuwezeshja kupunguza matumizi ya mkaa, na hasa ikizingatiwa nchi yetu ina gesi lukuki.
Naye Mdau mwingine BW. MAGID YAHYA OMARY kutoka kampuni ya mafuta ya KOBIL nayo inayotoa huduma zake maeneo ya Chalinze, ameitaka serikali kuzuia ukataji wa miti na wananchi ikiwezekana walazimishwe kupanda miti ili kuiokoa nchi isikumbwe na jangwa linalotunyemelea kwa kasi.
END
ADHA YA MAJI BAGAMOYO.
ADHA YA MAJI KIJIJI CHA GONGO KATA YA MKANGE JIMBO LA CHALINZE WILAYA YA BAGAMOYO PWANI Na John Gagarini, Mkange WANANCHI wa Kijiji cha Gongo kata ya Mkange wilayani Bagamoyo wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji ambapo huweka foleni ya kuchota maji kwenye kisima kilichopo kijijini hapo baada ya wiki mbili. Kutokana na usosefu huo wa maji wananchi hao wamekuwa wakinunua maji ya bomba ndoo ya lita 20 kati ya shilingi 1,000 na shilingi 1,500 maji ambayo huuzwa kwenye magari au pikipiki hivyo kuwafanya wajikute hawapati maendeleo kutokana na gharama kubwa kuzitumia kununulia maji. Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mkutano wa kampeni wa mgombea Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ridhiwani Kikwete, kwenye kata ya Mkange mwananchi wa Kijiji hicho Hungilo Nyoka alisema kuwa maji yamewafanya washindwe kupata maendeleo. Nyoka alisema kila kaya inatakiwa ichote madumu manne ili angalau kila mmoja apate baada ya hapo maji hukatika ambapo in...
Comments
Post a Comment