Ben Komba/Pwani-Tanzania/3/23/2012 5:19:44 PM
Halmashauri ya wilaya ya Kibaha kwa mara ya kwanza imezindua Baraza lake la wafanyakazi lenye jukumu la kuwashirikisha wafanyakazi wa halmashauri katika utekelezaji wa shughuli za halmashauri kwa kushirikiana na uongozi.
Akizungumza katika uzinduzi wa baraza hilo katibu tawala wilaya ya Kibaha, BW. JUSSEIM MWAKIPESILE akimwakilisha mkuu wa wilaya HAJAT HALIMA KIHEMBA, amesema baraza hili ni mwanzo mpya wa kihistoria kwa halmashauri ya wilaya ya Kibaha ikiwa kama sehemu ya sera ya kushirikisha wafanyakazi katika kila Nyanja ya halmashauri.
Na lengo kubwa likiwa ni kuongeza ufanisi mahali pa kazi ikiwa pamoja na kuboreha utendaji wa utumishi wa umma kwa kutoa huduma stahili kwa mteja anapohitaji kwa kuzingatia maadili na sheria za kazi zinazomzunguka mfanyakazi.
Aidha BW. MWAKIPESILE amebainisha kuwa baraza la wafanyakazi lina wajumbe wa kuteuliwa, wajumbe wa kuchaguliwa na wajumbe ambao wanaingia barazani kwa nyadhifa zao, hivyo amesisitiza umoja na mshikamano kama nguzo pekee ya kuiwezesha halmashauri kutimiza malengo iliyojiwekea.
Naye Afisa elimu kazi kutoka tume usluhishi na uamuzi –CMA- , BI. MODESTA NGOLI amesema baraza la wafanyakazi ni chombo ambacho kinatoa fursa kwa wafanyakazi kushirikishwa kikamilifu katika maamuzi mbalimbali yanayofanyika mahali pa kazi ambayo kwa njia mojq au nyingine yanaweza kugusa maslahi yake kama mfanyakazi.
BI. NGOLI ameongeza mabaraza ya wafanyakazi yalianza kuundwa kufuatia mapinduzi ya viwanda yaliyofanyika katika nchi za Magharibi ambapo waajiri kwa ajili ya kujipenda waliwanyonya wafanyakazi kiasi cha kuanzisha migomo ambayo baadaye iliuleta majadilano na kuanza kuonekana umuhimu wa kuwepo kwa mabaraza ya wafanyakazi, ili kero zote sehemu za kazi zifikishwe hapo mkwa ajili ya kufanyiwa kazi.
END.
ADHA YA MAJI BAGAMOYO.
ADHA YA MAJI KIJIJI CHA GONGO KATA YA MKANGE JIMBO LA CHALINZE WILAYA YA BAGAMOYO PWANI Na John Gagarini, Mkange WANANCHI wa Kijiji cha Gongo kata ya Mkange wilayani Bagamoyo wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji ambapo huweka foleni ya kuchota maji kwenye kisima kilichopo kijijini hapo baada ya wiki mbili. Kutokana na usosefu huo wa maji wananchi hao wamekuwa wakinunua maji ya bomba ndoo ya lita 20 kati ya shilingi 1,000 na shilingi 1,500 maji ambayo huuzwa kwenye magari au pikipiki hivyo kuwafanya wajikute hawapati maendeleo kutokana na gharama kubwa kuzitumia kununulia maji. Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mkutano wa kampeni wa mgombea Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ridhiwani Kikwete, kwenye kata ya Mkange mwananchi wa Kijiji hicho Hungilo Nyoka alisema kuwa maji yamewafanya washindwe kupata maendeleo. Nyoka alisema kila kaya inatakiwa ichote madumu manne ili angalau kila mmoja apate baada ya hapo maji hukatika ambapo in...
Comments
Post a Comment