BEN KOMBA/PWANI-TANZANIA/3/22/2012 8:35:45 PM
Suala la maji safi na mazingira ni miongoni mwa maeneo ambayo yamo katika nguzo kuu katika kuboresha maisha na ustawi wa jamii katika utekelezaji wa MKUKUTA.
Katibu tawala wilaya ya Kibaha BW. JUSSEIM MWAKIPESILE ameyasema hayo wakati wa maadhimisho ya wiki ya maji ambayo kiwilaya yamefanyika katika mji mdogo wa Mlandizi.
Ambapo BW. MWAKIPESILE amesema serikali katika kuhakikisha inakabiliana na uhaba wa maji na kuboresha usafi wa mazingira kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo imeanzisha program ya maji na usafi wa mazingira kwenye vijiji ambavyo vinakabiliwa na uhaba wa mkubwa wa maji.
Amefafanua kuwa program hiyo imeanza toka mwaka 2006 na inatarajiwa kukamilika mwaka 2025 na lengo kuu ni kuhakikisha wananchi wote wanapata maji safi na salama karibu na makazi yao ifikapo mwaka 2025 sambamba na dira ya maendeleo.
Awali mhandisi wa maji katika halmashauriWilayani Kibaha, BW. CHRISTOPHER MDUMA amebainisha kuwa maadhimisho ya wiki ya maji wilyanai Kibaha yameadhimishwa kwa kufanya shughuli mbalimbali, ikiwemo warsha kwa wadau wa maji kwa kujadili na kuweka mikakati kuhusiana na utunzwaji wa vyanzo vya maji, uanziushwaji wa sera wa jumuiya za watumiaji maji,
Ikiwa pamoja na kupitia sera ya maji na sheria ya maji na pia kamati ya maji na usafi wa mazingira imefanya mikutano ya awali na serikali za vijiji na kamati za maji za vijiji vya Kitomondo, Minazi Mikinda,, Ruvu Stesheni na Soga katika kipindi cha maadhimisho ya weiki ya maji Kauli Mbiu ya maadhimiosho ya wiki ya maji ni”MAJI KWA USALAMA WA CHAKULA”.
END.
ADHA YA MAJI BAGAMOYO.
ADHA YA MAJI KIJIJI CHA GONGO KATA YA MKANGE JIMBO LA CHALINZE WILAYA YA BAGAMOYO PWANI Na John Gagarini, Mkange WANANCHI wa Kijiji cha Gongo kata ya Mkange wilayani Bagamoyo wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji ambapo huweka foleni ya kuchota maji kwenye kisima kilichopo kijijini hapo baada ya wiki mbili. Kutokana na usosefu huo wa maji wananchi hao wamekuwa wakinunua maji ya bomba ndoo ya lita 20 kati ya shilingi 1,000 na shilingi 1,500 maji ambayo huuzwa kwenye magari au pikipiki hivyo kuwafanya wajikute hawapati maendeleo kutokana na gharama kubwa kuzitumia kununulia maji. Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mkutano wa kampeni wa mgombea Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ridhiwani Kikwete, kwenye kata ya Mkange mwananchi wa Kijiji hicho Hungilo Nyoka alisema kuwa maji yamewafanya washindwe kupata maendeleo. Nyoka alisema kila kaya inatakiwa ichote madumu manne ili angalau kila mmoja apate baada ya hapo maji hukatika ambapo in...
Comments
Post a Comment