Posts

BODABODA WAPATIWA MAFUNZO

Ben Komba/Pwani-Tanzania/8/31/2015 4:55:15 PM Jeshi la Polisi mkoa wa Pwani limewatunuku vyeti madereva wa bodaboda ambao wamemaliza mafunzo ya usalama barabarani ambayo yametolewa na shirika lisilo la kiserikali la ANTI POVERTY AND ENVIROMENTAL CARE-APEC. Mkurugenzi wa shirika hilo, BW.RESPICIUS TIMANYWA ameeleza kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuhakikisha usalama wa vyombo hivyo linakuwa jambo la lazima kwa kutoa elimu ambayo ikizingatiwa itaweza kuokoa maisha ya wengi. Bw.TIMANYWA amefafanua kuwa mpaka sasa wameshafikia mikoa 15 katika kuhakikisha wanawajen gea uwezo madereva  kiuchumi na kijamii na kufanikiwa kupunguza ajali kwa asilimia 95 ya wale ambao wamepatiwa mafunzo. Mrakibu mwandamizi wa Jeshi la Polisi TABITHA MAKARANGA amewashukuru APEC kwa kutoa mafunzo hayo ambayo kwa njia moja au nyingine yataweza kupunguza ajali zinazosababishwa na bodaboda. Mrakibu mwandamizi MAKARANGA amesema kuwa takwimu mpaka sasa zinaonyesha waathirika wakubwa wa ajali za ...

YANGA KUJENGA UWANJA WA KISASA

Ben Komba/Pwani-Tanzania/8/30/2015 1:10:38 PM Klabu bingwa ligi kuu ya Vodacom, Yanga Dar African inaendelea na mchakato wa kujenga kiwanja cha kimataifa cha michezo katika eneo la Jangwani katika suala zima la kuhakikisha wanajitosheleza kwenye miundombinu ya michezo. Mwenyekiti wa matawi ya Yanga nchini, MOHAMED MSUMI amesema hayo wakati wa uzinduzi wa Tawi la Yanga Maili moja, Kibaha mjini ambapo amesema kuwa mpaka sasa hatua mbalimbali zimeshachukuliwa kuhakikisha mafanikio hayo yanafikiwa. MSUMI amebainisha kuwa mpaka sasa wameshawasiliana na mamlaka husika ili ikiwezekana waongezewe eneo la kiwanja chao ili waweze kujenga uwanja huo ambao unatarajiwa kuchukua mashabiki 40000 na kuwepo kwa vianja mbalimbali kwa ajili kuendeleza michezo. Naye mgeni rasmi katika hafla hiyo mfanyabiashara na mshabiki mkubwa wa Yanga, LLYOD ATANAKA ameelezea kufurahishwa kwake na hatua hiyo ya wanachama wa Yanga kujiunga na kufungua Tawi hilo. Shabiki huyo wa Yanga,ATANAKA amewasis...

VIDEO- HAMAHAMA YATIA FORA

Ben Komba/Pwani-Tanzania/8/22/2015 2:48:56 PM Katika hatua inayoashiria kuwa vuguvugu la wananchama kimoja kuhamia kingine bado linafukuta kufuatia kuendelea kwa wananchama na viongozi waandamizi katika vyama vya siasa kufanya mzunguko ambapo kuna walioenda mbali zaidi kuzunguka zaidi ya viwili kwa mpigo. Hali hiyo imeendelea pia wilayani Kibaha ambapo, Mwenyekiti wa CCM Wazazi BW. ALLY BAGO Kata ya Boko Mnemela kuamua kujivua nafasi yake na kujiunga na CHADEMA ikiwa hatua hiyo ameichukua kufuatia kuchukizwa na mambo yanavyoendeshwa katika chama hicho kwa hivi sasa. BW.BAGO amesema vijana ambao wamepewa vyeo katika chama hicho wamekuwa wapuuzi ambao hawaheshimi wanachama wakongwe ambao wamewakuta katika chama hicho, na amejipanga kufanya kazi na chama chake kipya katika kuhakikisha mabadiliko yanapatikana nchini. Sawa na tukio hilo la kurudisha Kadi ya chama cha Mapinduzi kwa kada ALLY BAGO ambapo amekabidhiwa kadi ya CHADEMA na Mwenyekiti wa Baraza la wazee wa CHAD...

VIDEO - HAMAHAMA YA VYAMA KIBAHA NAYO HAIPO NYUMANAYO

Image
Ben Komba/Pwani-Tanzania/8/22/2015 2:48:56 PM Katika hatua inayoashiria kuwa vuguvugu la wananchama kimoja kuhamia kingine bado linafukuta kufuatia kuendelea kwa wananchama na viongozi waandamizi katika vyama vya siasa kufanya mzunguko ambapo kuna walioenda mbali zaidi kuzunguka zaidi ya viwili kwa mpigo. Hali hiyo imeendelea pia wilayani Kibaha ambapo, Mwenyekiti wa CCM Wazazi BW. ALLY BAGO Kata ya Boko Mnemela kuamua kujivua nafasi yake na kujiunga na CHADEMA ikiwa hatua hiyo ameichukua kufuatia kuchukizwa na mambo yanavyoendeshwa katika chama hicho kwa hivi sasa. BW.BAGO amesema vijana ambao wamepewa vyeo katika chama hicho wamekuwa wapuuzi ambao hawaheshimi wanachama wakongwe ambao wamewakuta katika chama hicho, na amejipanga kufanya kazi na chama chake kipya katika kuhakikisha mabadiliko yanapatikana nchini. Sawa na tukio hilo la kurudisha Kadi ya chama cha Mapinduzi kwa kada ALLY BAGO ambapo amekabidhiwa kadi ya CHADEMA na Mwenyekiti wa Baraza la wazee wa CH...

SHULE YA JUMUIYA YA WAZAZI CCM KIBAHA HATARINI KUPIGWA MNADA.

Ben Komba/Pwani-Tanzania/8/23/2015 11:22:24 AM Iliyokuwa shule ya Jumuiya ya wazazi ya Chama Cha Mapinduzi ipo hatarini kupigwa mnada kwa kudaiwa shilingi milioni 12, ambazo inaelekea Jumuiya hiyo imeshindwa kuzilipa. Katibu wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM, Kibaha mjini, BI.ZAITUNI KIOBYA amesema wao wameshangazwa kusikia kuna gari linapita mitaani likitangaza upigaji mnada wa shule hiyo ambayo ilijifunga bila utaratibu kutokana na kukosekana kwa usimamizi madhubuti. BI.KIOBYA ameongeza hatua ya kutaka kupiga mnada shule hiyo ulifanyika bila Jumuiya ya wazazi wilaya kushirikishwa hususan Kamati ya utekelezaji ambayo ndiyo yenye jukumu la kusimamia shule zote zinazomilikiwa na Jumuiya ya wazazi wa chama cha mapinduzi. Amefafanua baada ya kusikia uamuzi huo wa kutaka kuuzwa kwa njia yam nada kwa shule hiyo, Jumuiya ya wazazi ikaamua kufuata taratibu za kisheria kuweka pingamizi kuendeshwa kwa zoezi hilo ambalo lilikuwa liendeshwe na TAMBAZA AUCTION MART, ambao tayari walikuwa...

HAMA YA KUTOKA CHAMA KIMOJA KINGINE YAENDELEA

Ben Komba/Pwani-Tanzania/8/22/2015 2:48:56 PM Katika hatua inayoashiria kuwa vuguvugu la wananchama kimoja kuhamia kingine bado linafukuta kufuatia kuendelea kwa wananchama na viongozi waandamizi katika vyama vya siasa kufanya mzunguko ambapo kuna walioenda mbali zaidi kuzunguka zaidi ya viwili kwa mpigo. Hali hiyo imeendelea pia wilayani Kibaha ambapo, Mwenyekiti wa CCM Wazazi BW. ALLY BAGO Kata ya Boko Mnemela kuamua kujivua nafasi yake na kujiunga na CHADEMA ikiwa hatua hiyo ameichukua kufuatia kuchukizwa na mambo yanavyoendeshwa katika chama hicho kwa hivi sasa. BW.BAGO amesema vijana ambao wamepewa vyeo katika chama hicho wamekuwa wapuuzi ambao hawaheshimi wanachama wakongwe ambao wamewakuta katika chama hicho, na amejipanga kufanya kazi na chama chake kipya katika kuhakikisha mabadiliko yanapatikana nchini. Sawa na tukio hilo la kurudisha Kadi ya chama cha Mapinduzi kwa kada ALLY BAGO ambapo amekabidhiwa kadi ya CHADEMA na Mwenyekiti wa Baraza la wazee wa CHADEM...

PCCB WAJIPANGA KUDHIBITI RUSHWA YA UCHAGUZI

Ben Komba/Pwani-Tanzania/8/13/2015 10:01:51 PM Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa mkoani Morogoro imesisitiza kukomesha vitendo vya rushwa kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu. Akiongea na waandishi wa habari ambao walifika   ofisini kwake mjini Morogoro kamanda wa PCCB wa mkoa huo,BW.EMMANUEL KIYABO amebainisha mpaka wamechukua hatua mbalimbali za kukabiliana na rushwa kipindi cha uchaguzi. Kamanda KIYABO amesema moja ya hatua ambazo wamechukua nikuandaa katazo kuhusiana na utoaji na upokeaji wa rushwa kipindi cha uchaguzi,amebainisha kuwa sababu kubwa ya kuwepo na rushwa katika kipindi hicho tama ya kupata kitu chochote bila kufuata taratibu. Aidha ameongeza kuwa uelewa mdogo wa wapiga kura kuhusu rushwa na athari zake kipindi cha uchaguzi na hasa kutokana na wananchi kutojua nafasi na wajibu wao katika uchaguzi na umuhimu wa kura zao. Kamanda huyo wa PCCB mkoa wa Morogoro, BW.EMMANUEL KIYABO ameongeza suala la umaskini...