WANANCHI WAJITOLEA KUKARABATI KIPANDE CHA BARABARA MLANDIZI



Ben Komba/Pwani-Tanzania/28/05/2017 15:56:54
Wananchi katika mji wa Mlandizi wamejitolea kutengeneza miundombinu ya barabara iliyoharibika kufuatia mvua kubwa zilizonyesha kwa takriban miezi miwili  nchini.

Wakazi hao wa Mlandsizi Mtongani waliungana kwa  umoja kukarabati kipande hicho cha barabara ambacho kilikuwa na kalavati lililozidiwa nguvu na maji yaliyokuwa yananatiririka na kuzidi kiasi cha kupita pembeni na kusababisha  kumeguka kwa barabara hiyo inayounganisha vitongoji vya Msagasa na Mtongani.

Mmoja wa wakazi wa eneo BW.KONDO MGEGEDA amesema kipande hicho cha barabara kinachounganisha vijiji vya Mlandizi na kuelekea maeneo ya Disunyala na Mzenga kiliharibika katika kipindi cha mvua  na kusababisha usumbufu mkubwa kwa magari yaliyotaka kwenda maeneo hayo.

Hivyo kwa kuliona hilo wakaamua kuita msaragambo kwa ajili ya kukarabati eneo hilo ili kuwezesha usafiri wa pikipiki kupita maeneo hayo katika kupunguza  makali ya tatizo hilo.

BW. MGEGEDA ameonmgeza kuwa Diwani wa eneo hilo, BIBI.HABIBA MFALAMAGOHA alifika eneo hilo na kuahidi kulishughulikia tatizo hilo ili kuwezesha barabara hiyo kupitika.
INSERT:WANANCHI WALIOJITOLEA


END

Comments

Popular posts from this blog

MAFUNZO YA UREFA

WANANCHI KIDIMU WAPINGA HATUA YA MKURUGENZI WA MJI KIBAHA.