UHURU WA HABARI HATARINI,


Ben Komba- Katibu Chama Cha Waandishi Habari,Pwani
Hatua ya Rais Magufuli kuleta mabadiliko ya kijamii kwa Watanzania kwa sasa inaonyesha kuna baadhi ya watu wanapotosha dhana nzima ya kwa kuiga aina ya utendaji kazi ambayo sio asili yao na matokeo yake kuna wananchi maskini ambao ndio waliolengwa kusaidiwa na juhudi za Rais kuwaondolea adha ndio wanaoumizwa na waigizaji.

Tunashuhudia baadhi ya Mawaziri wa awamu ya tano wakipita huko na huko kuwajengea wananchi hofu kwa kutoa kauli ambazo zenyewe tu zinaonekana hazijaenda shule, kwa ajili tu labda kupitia mchakato wa kidemokrasia kandamizi wamebahatika kugawiwa vyeo ambavyo hawastahili.

Kwanza nikianzia suala la bomoabomoa ambalo wenyewe wanadai limelenga kuhakikisha maeneo ya wazi ambayo yamevamiwa na kujengwa nyumba kinyume cha taratibu linafanyika bila kufuata taratibu za kiutu na kuwasababishia wananchi umaskini zaidi, kutokana na baadhi ya watendaji kuingiza masuala binafsi wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo.

Binafsi nimeshangazwa sana na utaratibu uliotumika wa kuvunja soko ambalo jamii ya Picha ya ndege mjini Kibaha ilikuwa inalitegemea kupata huduma muhimu ya bidhaa mbalimbali, bila halmashauri kujenga soko jingine, hatua kama hizo hazimsaidii mwananchi wa kawaida ambaye hana uhakika wa kipato na badala yake imekuwa hukumu kwao.

Wananchi siku zote wamekuwa wahanga wa maamuzi ya viongozi ambao wanajidai wanawatakia mema ilihali wanawakandamiza na kurudisha nyuma maendeleo yao, Mpaka sasa wananchi kibao wameshaathirika na hatua kandamizi zinazofanywa na mawaziri wanaolazimisha umaarufu wa haraka haraka.

Basi  ni lini mwananchi wa kawaida atafaidika na uhuru wa nchi yake, Ingawa kuna hatua mbalimbali ambazo serikali ya awamu ya tano imezitekeleza ambazo zinaathari chanya moja kwa moja kwa mwananchi wa kawaida na kwa Taifa katika suala zima la kukuza uchumi wa Taifa ambalo ni upunguzaji wa tozo mbalimbali za umeme.

Lakini cha kusikitisha pamoja na upendeleo huo kwa  wananchi kuna tatizo kuhusiana na serikali ya awamu ya tano  inavyoshirikiana na sekta isiyo rasmi katika utoaji wa ajira kwa kuibua vikwazo mbalimbali ambavyo havina mashiko.

Mfano mzuri ni katika upande wa habari, ambayo watendaji wake wanakuambia ni kazi ya wito ambayo huwezi kuifananisha na udaktari wa uhandisi kitaaluma, ambapo kuna taarifa ya kutaka waandishi wote lazima wawe na digrii ili kuweza kufanya kazi hiyo.

Hatua hiyo inachukuliwa ni kama hatua ya makusudi ya kuhujumu uhuru wa habari ili kutoa fursa kwa siri mbaya za mafisadi wanaoila nchi hii kama walavyo mkate na kuwacheka pamoja na kuwahujumu wanaonyonywa na kuonewa kwa kutumia vyombo vya dola na sheria kandamizi ambazo hazina nia njema na maisha ya Watanzania walio wengi.

Inashangaza Waziri anatumia fedha za serikali kwa ajili ya kufanya ziara ya kutangaza vita dhidi ya vyombo vya habari bila kujali taratibu za kitaaluma kwa kulazimisha waandishi wote wawe na digrii,  hali ambayo huwezi kuikuta katika maeneo mengine yaani hospitali na serikalini kwenyewe kwenye utaratibu kama huo.

Tena sehemu zenyewe muhimu kwa maisha ya wanadamu, Lakini kwa waandishi lazima wawe na digrii wote, kwa upande wangu mimi naona hatua hiyo imekaa kisiasa zaidi kuliko kitaaluma ambapo kuna watumishi wa viwango tofauti vya kielimu katika upande wa sekta ambayo siyo rasmi ya habari, kulazimisha waandishi wote wawe na digrii bila kuwasaidia kuipata hiyo digrii huo ni udikteta ambao ushaanza kuota mizizi na kuathiri wananchi maskini walio wengi.

Ni vizuri watu wa kawaida wasichukuliwe kama mbuzi wa kafara, kwa ajili ya watu kujikweza juu yao ili waonekane wanachapakazi kwa kuharibu maisha ya walio wengi na huko ni kukiuka haki za binadamu mchana kweupe.

Huwezi kuwalazimisha waandishi wa habari wawe na digrii wakati kuna watendaji kibao ambao wanasemekana wana vyeti vya kufoji, tatizo ambalo ni kubwa sana upande huo, kiasi hata cha kuhatarisha ajira ya kipindi alipokuwa NECTA, Waziri Ndalichako kwa waliofoji kumfanyia vurugu alipotaka kufanya uhakiki wa vyeti vya wakubwa mbalimbali ambao wanamiliki vyeti vya kufoji.

Na tulishuhudia maandamano na upinzani kutoka kwa vigogo ambao wanasemekana kughushi vyeti na kuliletea Taifa hasara kutokana na kuwepo katika nafasi ambazo hawawezi kuzitumikia ipasavyo.

Mpaka sasa serikali ya awamu ya tano imefanikiwa kuongeza wimbi la wasio na ajira kutokana maamuzi ya kujionyesha yanayofanywa na baadhi ya mawaziri ambao kiuhalisia ni wapigaji tu na sio makini na ambao wengine wamepata nafasi hizo kwa kupora ushindi wa waliostahili na kujivisha wenyewe kwa kutumia nguvu kubwa za dola ambazo chama tawala inazo.

Ili suala la kuweka digrii mbele kuliko akili ya kawaida (common sense) ambayo inatolewa kama karama kwa baadhi ya wanadamu, Linatakiwa kupingwa kwa nguvu zote na ndio maana vidole vya mkono havifanani, hatuwezi wote kuwa na digrii ikiwa nchi haina hata mtaala wa uandishi wa habari ambao mi binafsi ninao kutoka Uingereza ambao WRITERS BUREAU walinipatia na kujisomea nyumbani ili niweze kupata mafanikio katika utekelezaji wa majukumu yangu ya kila siku, Kuleta makuzi katika masuala muhimu ya Kitaifa kutaathiri kwa njia moja au nyingine maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Kufanya maamuzi ya kukomoana hakutasaidia chochote badala yake kutaathiri juhudi ya serikali kuwaletea wananchi maendeleo yao na toka wanahabari wamekuwa wanafanya kazi kwa karibu na taasisi nyeti za serikali na kuheshimka maeneo hayo.
END


Comments

Popular posts from this blog

MAFUNZO YA UREFA

WANANCHI KIDIMU WAPINGA HATUA YA MKURUGENZI WA MJI KIBAHA.