PCCB PWANI YATOA RIPOTI YA ROBO YA KWANZA 2016

Ben Komba/Pwani-Tanzania/13/04/2016 15:52:46
Ofisi ya TAKUKURU (M) Pwani katika kipindi cha robi ya kwanza ya mwaka 2016 imefanikiwa kutekeleza majukumu yake katika kuielimisha jamii na kufanya uchunguzi wa tuhumaa mbalimbali zinazohusiana na rushwa.

Kamanda wa TAKUKURU mkoa wa Pwani, BI. SUZAN RAYMOND amezungumza hayo wakati wa kikao na waandishi wa habari katika ofisi za taasisi hiyo mjini Kibaha, amesema katika mkipindi hicho taasisi hiyo imefanya uchunguzi na uchambuzi wa mifumo kwa lengo la kubaini mianya ya rushwa na kutoa ushauri wa namna ya kuiziba katika taasisoi na idara mbalimbali.

BI.SUZAN ameongeza kwamba katika kipindi hicho ofisi yake imepokea malalamiko 64 kati ya hayo 49 yanahusiana na vitendo bvya rushwa na uchunguzi wake unaendelea na malalamiko 15 hayakuhusiana na vitendo vya rushwa ambapo walalamikaji  walishauriwa kupeleka kero zao katika idara husika.

Kamanda huyo wa TAKUKURU Mkoa wa Pwani BI SUZAN RAYMOND ametaja kama serikali za mitaa ndio kinara wa rushwa na wilaya ambayo imeathirika zaidi ni Bagamoyo.


END.

Comments

Popular posts from this blog

MAFUNZO YA UREFA

WANANCHI KIDIMU WAPINGA HATUA YA MKURUGENZI WA MJI KIBAHA.