LICHA KUPEWA KIPAUMBELE WAGONJWA WA UKIMWI WAKOSA HUDUMA MUHIMU


Ben Komba/Pwani-Tanzania/20/04/2016 13:06:37
Imegundulika mjini Kibaha kuwa mradi wa kuwasaidia wagonjwa walio majumbani ambao ulikuwa unasimamiwa na chama cha msalaba mwekundu Tanzania umeshindwa kukidhi mahitaji ya wagonjwa ambao walikuwa wanalengwa.
Kwa mujibu wa watoa huduma majumbani ambao mwandishi wa habari hizi amefanikiwa kuongea nao, Mmoja wao BW. RAJAB NGONJI ameeleza yeye amekuwa akifanya kazi hiyo kwa takriban miaka kumi lakini anachokiona sasa ni tofauti sana na awali.

Bw. NGONJI  amesema mradi huo unaofadhiliwa EGPAF na PATHFINDER na kusimamiwa na Chama cha Msalaba mwekundu umekuwa ukiendeshwa kwa kuangalia zaidi gharama za uendeshaji wa Ofisi na kujilipa mishahara na posho na kuwaacha wagonjwa wanaangamia majumbani kwa kukosa madawa na lishe.

BW. NGONJI ameongeza kuwa hapo awali wagonjwa walikuwa wanapatiwa misaada mbalimbali ikiwamo na madawa, kitu ambacho sasa hakuna na hivyo kuwafanya wagonjwa kunufaika kidogo na msaada unaotolewa kwao.

Naye  BW. MICHAEL BEDA mhudumu wa afya kutoka mtaa wa Kibondeni amesema kumekuwepo na usumbufu mkubwa linapokuja suala la kulipwa posho ambazo Shirika la Msalaba Mwekundu wanatumia M PESA kuwalipa na hivyo kusababisha usumbufu mkubwa.

BW. BEDA amefafanua kuwa wamekuwa wakisubiri mpaka miezi mitatu  bila kulipwa posho na hivyo kufanya zoezi la kutembelea wagonjwa kuwa gumu na hasa pale wagonjwa wanapohitaji misaada midogomidogo kama fedha za sabuni, chakula na madawa.
Naye mratibu wa mpango huo wa kuhudumia wagonjwa majumbani wilayani Kibaha BI. AGNES LIBOGA amejibu madai hayo kwa kudai kuwa wao hawahusiki na utoaji wa chakula kwa wagonjwa ambao wamesendeka, kuhusiana na suala kucheleweshwa kwa posho kwa watoa huduma majumbani amebainisha kuwa wameshaanza kulipwa posho zao za miezi mitatu.


END

Comments

Popular posts from this blog

MAFUNZO YA UREFA

WANANCHI KIDIMU WAPINGA HATUA YA MKURUGENZI WA MJI KIBAHA.