Ben Komba/Pwani-Tanzania/23-07-2013/10:03 Chama cha marefa wilayani Kibaha kinaendesha program maalum ya mafunzo kwa marefa wapya wenye kutaka kujiendeleza kuwa waamuzi katika ngazi mbalimbali za ligi za mchezo huo. Katibu wa Chama cha marefa wilayani Kibaha ambaye pia ndio refa bora wa ligi ya VODACOM msimu uliopita BW.SIMON MBELWA amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwezesha kuzalisha marefa wapya. BW.MBELWA amefafanua kuwa katika mambo ambayo yatazingatiwa katika mafunzo hayo ni ufundishaji wa sheria 17 za soka ambazo kila mwamuzi anapaswa kuzifahamu kwa ufasaha ili kuepusha malalamiko na wakati mwingine hata vurugu katika mchezo huo. Naye mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo, BW. GEORGE amesema kwa kupatiwa mafunzo hayo kutawasaidia kufanya maamuzi yaliyo sahihi wakati wakichezesha mechi za michuano mbalimbali. END.
Ben Komba/Pwani-Tanzania/ Wananchi katika mamlaka ya mji mdogo wa Mlandizi wamelalamika hatua ya uanzishaji wa mji huo na kuutelekeza bila kuiwezesha kifedha hali inayoathiri utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya kila siku. Nikiongea na mmoja wa wajumbe wa baraza la mamlaka ya mji mdogo wa Mlandizi ambaye alikataa jina lake kutajwa , amebaiinisha kuwa kumekuwepo na changamoto mbalimbali zinazoikabili mamlaka ya mji mdogo wa Mlandizi. Mjumbe huyo amesema kutokana na kukosekana kwa fedha kutoka halmashauri kunakosabishwa na baadhi ya watendaji ya halmashauri kuchelea wao kupunguza fedha za uendeshaji wa halmashauri kutokana na kutojiamini. Mjube huyo amebainisha kutokuwepo kwa vikao vya kisheria vya kila mwaka vinavyofanywa na baraza la mamlaka ya mji mdogo wa Mlandizi kwa madai ya kukosekana kwa fedha na kuhoji serikali inawezaje kupanga mipango ambayo haiwezi kuitekeleza. Naye Mwenyekiti wa mamalaka ya mji mdogo wa Mlandizi, BW. ABDALLAH KIDO amesema ni...
Ben Komba /Pwani-Tanzania/4/25/2015 11:28:27 PM Chama cha Walimu mkoa wa Pwani Kimefanya uchaguzi wake mkuu wa kuchagua viongozi watakawaongoza katika kipindi kijacho cha uongozi katika uchaguzi uliofanyika mjini Kibaha. Akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake K atibu wa CWT mkoa wa Pwani, BW.NEHEMIAH JOSEPH amesema uchaguzi huo ulikuwa huru na haki na wajumbe wamefanikiwa kutumia nafasi kuwapata viongozi ambao watawaongoza teanaa katika kipindi cha miaka mitano ijayo. BW.NAHEMIAH amewataja washindi katika nafasi ya Mwenyekiti wa CWT mkoa wa Pwani imechukuliwa na BW.JOHN KIRUMBI waakati BI.STELLA KIYABO amepata na ujumbe a kamati ya utendaji ya CWT, nafasi ya mweka hazina ikichukuliwa na BW.ABOUBAKAR ALAWI. Nafasi Nyingine Zilizogombaniwa Katika uchaguzi huo kwa mujibu wa Katibu wa CWT mkoa wa Pwaani BW. NEHEMIAH JOSEPH ni pamoja na mjumbe atakayewakilisha CWT,Baraza la TUCTA ambapo BW.RAJAB NGAMBAGE alishinda na upande mwakilishi katika mkut...
Comments
Post a Comment